1Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
1Kui nüüd Issand sai teada, et variserid olid kuulnud, et Jeesus teeb jüngriteks ja ristib rohkem inimesi kui Johannes -
2(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
2kuigi Jeesus ise ei ristinud, vaid tema jüngrid -,
3Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
3jättis ta Juudamaa ja läks tagasi Galileasse.
4na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
4Ta pidi aga minema läbi Samaaria.
5Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
5Ta tuli Samaaria küla juurde, mida hüütakse Sühhariks, maatüki lähedale, mille Jaakob oli andnud oma pojale Joosepile;
6Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
6seal oli Jaakobi allikas. Teekäimisest väsinuna istus Jeesus nüüd allika äärde. Oli keskpäeva aeg.
7Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, "Nipatie maji ninywe."
7Samaaria külast tuli naine vett ammutama. Jeesus ütles talle: 'Anna mulle juua!'
8(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
8Aga tema jüngrid olid läinud külasse toitu ostma.
9Lakini huyo mwanamke akamwambia, "Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?" (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
9Siis Samaaria naine ütles talle: 'Kuidas! Sina, kes oled juut, küsid juua minult, Samaaria naiselt?' Juudid väldivad ju iga kokkupuudet samaarlastega.
10Yesu akamjibu, "Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai."
10Jeesus vastas: 'Kui sa ainult teaksid Jumala kinki ja kes see on, kes sulle ütleb: Anna mulle juua!, siis sa paluksid teda ning tema annaks sulle elavat vett.'
11Huyo mama akasema, "Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
11Naine ütles talle: 'Isand, ämbrit sul ei ole ja kaev on sügav. Kust sa siis saad selle 'elava vee'?
12Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki."
12Ega siis sina ole suurem kui meie isa Jaakob, kes andis meile kaevu ning jõi sellest ise, samuti ta pojad ja ta kariloomad!?'
13Yesu akamjibu, "Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
13Jeesus kostis: 'Igaüks, kes joob seda vett, januneb jälle,
14Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele."
14aga kes iganes joob vett, mida mina talle annan, ei janune enam iialgi, vaid vesi, mille mina talle annan, saab tema sees igavesse ellu voolavaks allikaks.'
15Huyo mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji."
15Naine ütles talle: 'Isand, anna mulle seda vett, et ma ei januneks enam ega peaks aina käima siit ammutamas!'
16Yesu akamwambia, "Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa."
16Jeesus ütles talle: 'Mine kutsu oma mees ning tule siia tagasi!'
17Huyo mwanamke akamwambia, "Mimi sina mume." Yesu akamwambia, "Umesema kweli, kwamba huna mume.
17Naine vastas: 'Mul ei ole meest.' Jeesus ütles talle: 'Sul on õigus, kui sa ütled: 'Mul ei ole meest',
18Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli."
18sest kuigi sul on olnud viis meest, ei ole see, kellega sa praegu elad, sinu mees. Seda sa oled õigesti ütelnud.'
19Huyo Mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
19Naine ütles temale: 'Isand, ma näen, et sa oled prohvet.
20Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu."
20Meie esiisad kummardasid Jumalat sellel mäel, ja teie ütlete, et Jeruusalemm olevat paik, kus peab kummardama.'
21Yesu akamwambia, "Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
21Jeesus ütles talle: 'Naine, usu mind, et tuleb tund, mil te ei kummarda Isa sellel mäel ega Jeruusalemmas!
22Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
22Teie kummardate, mida te ei tea, meie kummardame, mida me teame, sest pääste tuleb juutidelt.
23Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
23Kuid tuleb tund ja see ongi juba käes, et tõelised kummardajad kummardavad Isa vaimus ja tões, sest Isa otsib neid, kes teda nõnda kummardavad.
24Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake."
24Jumal on Vaim ja kes teda kummardavad, peavad teda vaimus ja tões kummardama.'
25Huyo mama akamwambia, "Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu."
25Naine ütles temale: 'Ma tean, et tuleb Messias, keda nimetatakse Kristuseks. Kui tema tuleb, siis ta kuulutab meile kõik.'
26Yesu akamwambia, "Mimi ninayesema nawe, ndiye."
26Jeesus ütles talle: 'Mina, kes ma sinuga räägin, olengi see.'
27Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: "Unataka nini?" au, "Kwa nini unaongea na mwanamke?"
27Ja sel hetkel tulid ta jüngrid tagasi ja panid imeks, et Jeesus kõneles naisega. Ometi ei öelnud keegi: 'Mis sa temalt tahad?' või 'Mida sa temaga räägid?'
28Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
28Siis jättis naine oma veekannu sinna ning läks tagasi külla ja ütles inimestele:
29"Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?"
29'Tulge vaadake inimest, kes ütles mulle kõik, mis ma olen teinud! Kas mitte tema pole Messias?'
30Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
30Ja nad tulid külast välja Jeesuse juurde.
31Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: "Mwalimu, ule chakula."
31Vahepeal palusid jüngrid teda: 'Rabi, söö!'
32Lakini Yesu akawaambia, "Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi."
32Aga tema ütles neile: 'Minul on süüa rooga, mida teie ei tea.'
33Wanafunzi wake wakaulizana, "Je, kuna mtu aliyemletea chakula?"
33Siis arutasid jüngrid omavahel: 'Kas keegi on talle süüa toonud?'
34Yesu akawaambia, "Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
34Jeesus ütles neile: 'Minu roog on see, et ma teen selle tahtmist, kes mu on läkitanud, ja lõpetan tema töö.
35Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
35Eks te ise ütle, et veel on neli kuud, ja siis tuleb lõikus? Vaata, mina ütlen teile: Tõstke silmad ja vaadake põlde: need on juba valged lõikuseks!
36Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.
36Nüüd saab lõikaja palka ja kogub vilja igaveseks eluks, et niihästi külvaja kui lõikaja ühtlasi saaksid rõõmustada.
37Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
37Jah, siin on tõsi see ütlus: 'Üks on, kes külvab, ja teine, kes lõikab.'
38Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao."
38Mina olen teid läkitanud lõikama seda, mille kallal teie pole vaeva näinud. Teised on näinud vaeva, ja teie olete tulnud nende vaeva vilja lõikama.'
39Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: "Ameniambia mambo yote niliyofanya."
39Aga palju samaarlasi sellest külast uskus Jeesusesse naise sõnade tõttu, kes tunnistas: 'Tema ütles mulle kõik, mis ma olen teinud.'
40Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
40Kui siis samaarlased tulid tema juurde, palusid nad teda jääda nende juurde. Ja Jeesus viibis seal kaks päeva.
41Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
41Ja Jeesuse enda sõnade tõttu hakkas temasse uskuma veel palju enam inimesi.
42Wakamwambia yule mama, "Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu."
42Aga naisele nad ütlesid: 'Me ei usu mitte enam sinu kõne tõttu, vaid me oleme teda ise kuulnud ning teame nüüd, et tema on tõesti maailma Päästja.'
43Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
43Aga kahe päeva möödudes rändas Jeesus sealt edasi Galileasse.
44Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, "Nabii hapati heshima katika nchi yake."
44Jeesus ise ju tunnistas, et 'prohvetist ei peeta lugu ta oma kodukohas'.
45Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
45Ometi, kui ta nüüd tuli Galileasse, võtsid galilealased tema hästi vastu, sest nad olid näinud, mida kõike ta oli teinud pühade ajal Jeruusalemmas; nemadki olid ju käinud nendel pühadel.
46Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
46Nii tuli Jeesus taas Galilea Kaanasse, kus ta oli muutnud vee veiniks. Ja seal oli üks kuninga ametimees, kelle poeg oli Kapernaumas haige.
47Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
47Kui ta kuulis, et Jeesus on tulnud Juudamaalt Galileasse, läks ta tema juurde ja palus, et Jeesus tuleks alla ja teeks terveks tema poja, sest see oli suremas.
48Yesu akamwambia, "Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!"
48Siis Jeesus ütles talle: 'Te usute mind ainult siis, kui näete tunnustähti ja imetegusid.'
49Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa."
49Ametimees ütles talle: 'Issand, tule alla, enne kui mu laps sureb!'
50Yesu akamwambia, "Nenda tu, mwanao yu mzima." Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
50Jeesus ütles talle: 'Mine, sinu poeg elab!' Ja inimene uskus sõna, mis Jeesus talle ütles, ning läks.
51Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
51Aga juba koduteel tulid ta sulased talle vastu teatega, et ta laps elab.
52Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, "Jana saa saba mchana, homa ilimwacha."
52Siis ta päris neilt tundi, mil pojal hakkas kergem. Nad ütlesid talle: 'Eile päeval kella ühe ajal lahkus temast palavik.'
53Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: "Mwanao yu mzima." Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
53Nüüd märkas isa, et see oli juhtunud täpselt sel ajal, mil Jeesus oli talle öelnud: 'Sinu poeg elab!' Ja tema uskus, samuti kogu ta pere.
54Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.
54Selle teise tunnustähe tegi Jeesus pärast Juudamaalt Galileasse tulekut.