1Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.
1Maarja Magdaleena tuli hauale nädala esimese päeva varahommikul, kui oli alles pime, ja nägi, et kivi oli haualt ära tõstetud.
2Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, "Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka."
2Ta jooksis siis ja tuli Siimon Peetruse ja selle teise jüngri juurde, keda Jeesus armastas, ja ütles neile: 'Nad on Issanda hauast ära viinud ja me ei tea, kuhu nad on ta pannud.'
3Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.
3Peetrus läks nüüd välja ja see teine jünger ka ning tulid haua juurde.
4Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
4Nad jooksid mõlemad koos, ent teine jünger jooksis Peetrusest kiiremini ning jõudis haua juurde esimesena.
5Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.
5Ja kummargil sisse vaadates nägi ta surilinu. Ometi ei astunud ta sisse.
6Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,
6Siis tuli ka Siimon Peetrus temale järele ja astus hauda sisse ja nägi maas olevaid surilinu
7na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.
7ja higirätikut, mis oli Jeesuse pea ümber olnud, et see ei olnud koos surilinadega, vaid eraldi kokkumässituna teises kohas.
8Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
8Nüüd siis läks hauda sisse ka see teine jünger, kes esimesena oli hauale tulnud, ning nägi ja uskus.
9(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
9Sest nad ei teadnud veel Kirjast, et ta peab surnuist üles tõusma.
10Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
10Jüngrid läksid nüüd taas ära kodu poole.
11Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,
11Maarja seisis aga haua kõrval väljas ja nuttis. Kui ta nõnda nuttis, vaatas ta kummargil hauda
12akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.
12ja nägi kahte valges riides inglit istuvat seal, kuhu oli pandud Jeesuse ihu, ühte peatsis ja teist jalutsis,
13Hao malaika wakamwuliza, "Mama, kwa nini unalia?" Naye akawaambia, "Wamemwondoa Bwana wangu, na wala sijui walikomweka!"
13ja need ütlesid talle: 'Naine, miks sa nutad?' Tema vastas neile: 'Nad on mu Issanda ära viinud ja ma ei tea, kuhu nad on ta pannud.'
14Baada ya kusema hayo, aligeuka nyuma, akamwona Yesu amesimama hapo, lakini asitambue ya kuwa ni Yesu.
14Kui ta seda oli öelnud, pöördus ta ümber ja nägi Jeesust seismas, aga ta ei teadnud, et see on Jeesus.
15Yesu akamwuliza, "Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?" Maria, akidhani kwamba huyo ni mtunza bustani, akamwambia, "Mheshimiwa, kama ni wewe umemwondoa, niambie ulikomweka, nami nitamchukua."
15Jeesus ütles talle: 'Naine, miks sa nutad? Keda sa otsid?' Maarja arvas ta aedniku olevat ja ütles talle: 'Isand, kui sina oled ta ära kandnud, siis ütle mulle, kuhu sa ta panid, ja ma ise toon ta ära.'
16Yesu akamwambia, "Maria!" Naye Maria akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, "Raboni" (yaani "Mwalimu").
16Ja Jeesus ütles talle: 'Maarja!' Too pöördus ümber ja ütles talle heebrea keeles: 'Rabbuuni', see tähendab 'Õpetaja'.
17Yesu akamwambia, "Usinishike; sijakwenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu."
17Jeesus ütles talle: 'Ära puuduta mind, ma ei ole veel üles Isa juurde läinud. Aga mine mu vendade juurde ja ütle neile: Ma lähen üles oma Isa ja teie Isa ning oma Jumala ja teie Jumala juurde.'
18Hivyo Maria Magdalene akaenda akawapa habari wale wanafunzi kuwa amemwona Bwana, na kwamba alikuwa amemwambia hivyo.
18Maarja Magdaleena tuli ja kuulutas jüngritele: 'Ma olen näinud Issandat ja seda kõike ta ütles mulle.'
19Ilikuwa jioni ya siku hiyo ya Jumapili. Wanafunzi walikuwa wamekutana pamoja ndani ya nyumba, na milango ilikuwa imefungwa kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Basi, Yesu akaja, akasimama kati yao, akawaambia, "Amani kwenu!"
19Kui nüüd selsamal nädala esimesel päeval oli õhtuaeg ja seal, kuhu jüngrid olid kogunenud, olid uksed lukus, sest nad kartsid juute, tuli Jeesus, jäi seisma nende keskele ja ütles neile: 'Rahu teile!'
20Alipokwisha sema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi, hao wanafunzi wakafurahi mno kumwona Bwana.
20Kui ta seda oli öelnud, näitas ta neile oma käsi ja külge. Siis said jüngrid rõõmsaks Issandat nähes.
21Yesu akawaambia tena, "Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi."
21Jeesus ütles nüüd neile taas: 'Rahu teile! Nõnda nagu Isa on läkitanud minu, nõnda saadan ka mina teid.'
22Alipokwisha sema hayo, akawapulizia na kuwaambia, "Pokeeni Roho Mtakatifu.
22Kui ta seda oli öelnud, puhus ta nende peale ja ütles neile: 'Võtke vastu Püha Vaim!
23Mkiwasamehe watu dhambi zao, wamesamehewa; msipowaondolea, hawasamehewi."
23Kellele te iganes patud andeks annate, neile on need andeks antud, kellele te patud kinnitate, neile on need kinnitatud.'
24Thoma mmoja wa wale kumi na wawili (aitwaye Pacha), hakuwa pamoja nao wakati Yesu alipokuja.
24Aga Toomas, keda nimetatakse Kaksikuks, üks kaheteistkümnest, ei olnud nendega, kui Jeesus tuli.
25Basi, wale wanafunzi wengine wakamwambia, "Tumemwona Bwana." Thoma akawaambia, "Nisipoona mikononi mwake alama za misumari, na kutia kidole changu katika kovu hizo, na kutia mkono wangu ubavuni mwake, sitasadiki."
25Teised jüngrid ütlesid nüüd talle: 'Meie oleme näinud Issandat.' Aga tema ütles neile: 'Kui ma ei näe tema käte sees naelajälgi ning ei pista oma sõrme naelte asemeisse ega oma kätt tema külje sisse, ei usu ma mitte!'
26Basi, baada ya siku nane hao wanafunzi walikuwa tena pamoja mle ndani, na Thoma alikuwa pamoja nao. Milango ilikuwa imefungwa, lakini Yesu akaja, akasimama kati yao, akasema, "Amani kwenu!"
26Ja kaheksa päeva pärast olid ta jüngrid taas kodus ja Toomas nendega. Uksed olid lukus, aga Jeesus tuli, jäi seisma nende keskele ja ütles: 'Rahu teile!'
27Kisha akamwambia Thoma, "Lete kidole chako hapa uitazame mikono yangu; lete mkono wako ukautie ubavuni mwangu. Usiwe na mashaka, ila amini!"
27Seejärel ta ütles Toomale: 'Pane oma sõrm siia ja vaata minu käsi ning pane oma käsi ja pista mu külje sisse ning ära ole uskmatu, vaid usklik!'
28Thoma akamjibu, "Bwana wangu na Mungu wangu!"
28Toomas vastas talle: 'Minu Issand ja minu Jumal!'
29Yesu akamwambia, "Je, unaamini kwa kuwa umeniona? Heri yao wale ambao hawajaona, lakini wameamini."
29Jeesus ütles talle: 'Kas sa usud seepärast, et sa oled mind näinud? Õndsad on need, kes ei näe, kuid usuvad.'
30Yesu alifanya mbele ya wanafunzi wake ishara nyingine nyingi ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki.
30Jeesus tegi jüngrite ees veel palju muid tunnustähti, mida ei ole sellesse raamatusse kirja pandud,
31Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mpate kuwa na uzima kwa nguvu ya jina lake.
31aga need on kirja pandud, et te usuksite, et Jeesus on Kristus, Jumala Poeg, ja et teil uskudes oleks elu tema nimes.