1Baada ya hayo Yesu aliwatokea tena wanafunzi wake kando ya ziwa Tiberia. Aliwatokea hivi:
1Pärast seda ilmus Jeesus jüngritele veel Tibeeriase järve ääres. Aga ta ilmus nõnda:
2Simoni Petro, Thoma (aitwaye Pacha), na Nathanieli mwenyeji wa Kana Galilaya, wana wawili wa Zebedayo na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa wote pamoja.
2Siimon Peetrus ja Toomas, keda nimetatakse Kaksikuks, ja Naatanael, kes oli Galilea Kaanast, ja Sebedeuse pojad ja veel kaks tema jüngritest olid seal koos.
3Simoni Petro aliwaambia, "Nakwenda kuvua samaki." Nao wakamwambia, "Nasi tutafuatana nawe." Basi, wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakupata chochote.
3Siimon Peetrus ütles neile: 'Ma lähen kalale.' Nad ütlesid talle: 'Me tuleme sinuga kaasa.' Nad läksid välja ja astusid paati. Ent sellel ööl ei püüdnud nad midagi.
4Kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya ziwa, lakini wanafunzi hawakujua kwamba alikuwa yeye.
4Aga koidu ajal seisis Jeesus kaldal. Ent jüngrid ei teadnud, et see on Jeesus.
5Basi, Yesu akawauliza, "Vijana, hamjapata samaki wowote sio?" Wao wakamjibu, "La! Hatujapata kitu."
5Jeesus ütles siis neile: 'Lapsed, on teil midagi leivakõrvaseks?' Nad vastasid talle: 'Ei ole.'
6Yesu akawaambia, "Tupeni wavu upande wa kulia wa mashua nanyi mtapata samaki." Basi, wakatupa wavu lakini sasa hawakuweza kuuvuta tena kwa wingi wa samaki.
6Aga tema ütles neile: 'Heitke noot paremale poole paati, siis te leiate!' Nad heitsidki, ja ei jaksanud seda enam tõmmata kalade hulga tõttu.
7Hapo yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, "Ni Bwana!" Simoni Petro aliposikia ya kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa), akarukia majini.
7Nüüd ütles jünger, keda Jeesus armastas, Peetrusele: 'See on Issand!' Siimon Peetrus, kuulnud, et see on Issand, võttis kuue ümber, sest ta oli alasti, ja hüppas järve.
8Lakini wale wanafunzi wengine walikuja pwani kwa mashua huku wanauvuta wavu uliojaa samaki; hawakuwa mbali na nchi kavu, ila walikuwa yapata mita mia moja kutoka ukingoni.
8Aga teised jüngrid tulid paadiga - nad ei olnud ju kaldast kaugemal kui umbes kakssada küünart - ja vedasid noota kaladega.
9Walipofika nchi kavu waliona moto wa makaa umewashwa na juu yake pamewekwa samaki na mkate.
9Kui nad nüüd tulid mäele, nägid nad valmis lõket ja selle peal kala ning leiba.
10Yesu akawaambia, "Leteni hapa baadhi ya samaki mliovua."
10Jeesus ütles neile: 'Tooge neid kalu, mida te praegu püüdsite!'
11Basi, Simoni Petro akapanda mashuani, akavuta hadi nchi kavu ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa mia moja na hamsini na watatu. Na ingawa walikuwa wengi hivyo wavu haukukatika.
11Siimon Peetrus läks üles ja tõmbas mäele nooda täis suuri kalu, arvult sada viiskümmend kolm. Ja noot ei rebenenud, kuigi neid oli nii palju.
12Yesu akawaambia, "Njoni mkafungue kinywa." Hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumwuliza: "Wewe ni nani?" Maana walijua alikuwa Bwana.
12Jeesus ütles neile: 'Tulge sööma!' Ükski jüngritest ei julgenud temalt küsida: 'Kes sa oled?', sest nad teadsid, et ta on Issand.
13Yesu akaja, akatwaa mkate akawapa; akafanya vivyo hivyo na wale samaki.
13Jeesus tuli ja võttis leiva ja andis neile, ja samuti kala.
14Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada ya kufufuka kutoka wafu.
14See oli Jeesusel juba kolmas kord jüngritele ilmuda pärast surnuist ülestõusmist.
15Walipokwisha kula, Yesu alimwuliza Simoni Petro, "Simoni, mwana wa Yohane! Je, wanipenda mimi zaidi kuliko hawa?" Naye akajibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza wana kondoo wangu."
15Kui nad nüüd olid einet võtnud, ütles Jeesus Siimon Peetrusele: 'Siimon, Johannese poeg, kas sa armastad mind rohkem kui need?' Peetrus ütles talle: 'Jah, Issand, sina tead, et sa oled mulle armas.' Jeesus ütles talle: 'Sööda mu tallesid!'
16Kisha akamwambia mara ya pili, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Petro akamjibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu."
16Tema ütles talle veel teist korda: 'Siimon, Johannese poeg, kas sa armastad mind?' Ta vastas talle: 'Jah, Issand, sina tead, et sa oled mulle armas.' Jeesus ütles talle: 'Hoia mu lambaid kui karjane!'
17Akamwuliza mara ya tatu, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Hapo Petro akahuzunika kwa sababu alimwuliza mara ya tatu: "Wanipenda?" akamwambia, "Bwana, wewe wajua yote; wewe wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu!
17Tema ütles talle kolmandat korda: 'Siimon, Johannese poeg, kas ma olen sulle armas?' Peetrus jäi kurvaks, et Jeesus küsis temalt kolmandat korda: 'Kas ma olen sulle armas?' Ja ta ütles temale: 'Issand, sina tead kõik, sina tead, et sa oled mulle armas.' Jeesus ütles talle: 'Sööda mu lambaid!
18Kweli nakwambia, ulipokuwa kijana ulizoea kujifunga mshipi na kwenda kokote ulikotaka. Lakini utakapokuwa mzee utanyosha mikono yako, na mtu mwingine atakufunga na kukupeleka usikopenda kwenda."
18Tõesti, tõesti, ma ütlen sulle, kui sa olid noor, vöötasid sa end ise ning läksid, kuhu sa tahtsid, aga kui sa vanaks saad, siis sa sirutad oma käed välja ja keegi teine vöötab sind ning viib sind, kuhu sa ei taha.'
19(Kwa kusema hivyo, alionyesha jinsi Petro atakavyokufa na kumtukuza Mungu.) Kisha akamwambia, "Nifuate."
19Aga seda ta ütles vihjates, missuguse surmaga Peetrus pidi Jumalat austama. Aga kui Jeesus seda oli öelnud, ütles ta talle: 'Järgne mulle!'
20Hapo Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda, anafuata (Huyu mwanafunzi ndiye yule ambaye wakati wa chakula cha jioni, alikaa karibu sana na Yesu na kumwuliza: "Bwana ni nani atakayekusaliti?")
20Peetrus pöördus ja nägi kaasa tulemas jüngrit, keda Jeesus armastas, kes ka õhtusöömaajal oli nõjatunud tema rinnale ja küsinud: 'Issand, kes on su äraandja?'
21Basi, Petro alipomwona huyo akamwuliza Yesu, "Bwana, na huyu je?"
21Teda nähes ütles Peetrus nüüd Jeesusele: 'Issand, aga kuidas on temaga?'
22Yesu akamjibu, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini? Wewe nifuate mimi."
22Jeesus ütles talle: 'Kui ma tahan, et ta jääb minu tulekuni - mis see sinusse puutub? Sina järgne mulle!'
23Basi, habari hiyo ikaenea miongoni mwa wale ndugu kwamba mwanafunzi huyo hafi. Lakini Yesu hakumwambia kwamba mwanafunzi huyo hafi, ila, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini?"
23Siis levis kuuldus vendade seas, et too jünger ei surevatki. Aga Jeesus ei olnud öelnud talle, et ta ei sure, vaid: 'Kui ma tahan, et ta jääb minu tulekuni - mis see sinusse puutub?'
24Huyo ndiye yule aliyeshuhudia mambo haya na kuyaandika. Nasi twajua kwamba aliyoyasema ni kweli.
24Tema on see jünger, kes tunnistab neist asjust ja on selle kirjutanud; ja me teame, et tema tunnistus on õige.
25Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.
25On veel palju muudki, mida Jeesus tegi. Kui need kõik ükshaaval üles kirjutataks, siis, ma arvan, ei suudaks kogu maailmgi mahutada raamatuid, mis tuleks kirjutada.