Swahili: New Testament

Estonian

Acts

1

1Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
1Esimese raamatu, Teofilos, ma kirjutasin kõigest sellest, mida Jeesus algusest peale tegi ja õpetas
2mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
2kuni selle päevani, mil ta võeti üles taevasse pärast seda, kui ta apostlitele, keda ta oli valinud Püha Vaimu kaudu, oli andnud korraldusi.
3Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
3Neile ta oli pärast oma kannatamist näidanud ennast elavana, tõendades seda mitmel viisil, ilmudes neile neljakümne päeva jooksul ja kõneldes Jumala riigist.
4Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: "Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
4Kui siis Jeesus viibis koos nendega, keelas ta neil Jeruusalemmast lahkuda, käskides jääda ootama Isa tõotust, 'mis teie olete minult kuulnud.
5Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu."
5Johannes on küll ristinud veega, aga teid ristitakse Püha Vaimuga üsna varsti pärast neid päevi.'
6Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, "Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?"
6Siis küsisid temalt need, kes olid kokku tulnud: 'Issand, kas sa sel ajal taastad Iisraeli kuningriigi?'
7Lakini Yesu akawaambia, "Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
7Tema aga ütles neile: 'Ei ole teie osa teada aegu ja tunde, mis Isa on iseenese meelevallaga seadnud,
8Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia."
8vaid te saate väe Pühalt Vaimult, kes tuleb teie üle, ja te peate olema minu tunnistajad Jeruusalemmas ja kogu Juuda- ja Samaariamaal ning ilmamaa äärteni.'
9Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
9Kui Jeesus seda oli öelnud, tõsteti ta nende nähes üles ja pilv varjas ta nende silme eest.
10Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
10Kui nad taevasse vaatasid tema minekut, vaata, siis seisis nende juures kaks valgeis rõivais meest,
11wakasema, "Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni."
11kes ütlesid: 'Galilea mehed, mis te seisate siin ja vaatate üles taevasse? See Jeesus, kes teilt võeti üles taevasse, tuleb samal kombel, nagu te nägite teda taevasse minevat.'
12Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
12Siis nad pöördusid tagasi Jeruusalemma mäelt, mida kutsutakse Õlimäeks ja mis on Jeruusalemma lähedal ühe hingamispäeva teekonna kaugusel.
13Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
13Ja kui nad linna tulid, läksid nad ülemisse tuppa, kus neil oli tavaks viibida: Peetrus ja Johannes ja Jaakobus ja Andreas ja Filippus ja Toomas, Bartolomeus ja Matteus, Jaakobus, Alfeuse poeg, ja seloot Siimon ja Juudas, Jaakobuse poeg.
14Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
14Nemad kõik olid püsivalt ühel meelel palvetamas koos Jeesuse ema Maarja ning naistega ja Jeesuse vendadega.
15Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
15Neil päevil tõusis Peetrus vendade keskel püsti - rahvast oli koos umbes sada kakskümmend inimest - ning ütles:
16akasema, "Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
16'Mehed-vennad! Täide pidi minema kirjasõna, mis Püha Vaim on Taaveti suu läbi ette kuulutanud Juuda kohta, kellest sai Jeesuse kinnivõtjate teejuht.
17Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
17Ta oli ju meie sekka arvatud ja sama teenimine oli temagi osa.
18("Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
18Just tema hankis ülekohtu palgast enesele põllu, aga ta ise kukkus ülepeakaela alla, lõhkes keskelt ja kogu ta sisikond valgus välja.
19Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
19See on saanud teatavaks kõigile Jeruusalemma elanikele, nii et seda põldu nende murdes kutsutakse Hakeldamaks, see tähendab Verepõlluks.
20Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
20Laulude raamatusse on ju kirjutatud: 'Tema elupaik saagu tühermaaks ja ärgu elagu selles keegi', ja 'Tema ülevaatajaamet saagu teisele!'
21Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
21Niisiis peab saama Jeesuse ülestõusmise tunnistajaks koos meiega üks neist meestest, kes on meie hulgas olnud kogu selle aja, mil Issand Jeesus meie juures käis sisse ja välja,
22Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni."
22alates Johannese ristimisest kuni päevani, mil ta meilt võeti üles.'
23Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
23Ja nad esitasid kaks meest: Joosepi, keda kutsutakse Barsabaseks, hüüdnimega Justus, ning Mattiase.
24Kisha wakasali: "Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
24Siis nad palvetasid: 'Sina, Issand, kõikide südametundja - näita, kumma neist kahest sina oled valinud
25ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe."
25saama selle teenimiskoha ja apostliameti, kust Juudas on tagasi astunud, et minna paika, kuhu ta kuulub.'
26Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.
26Ja nad heitsid liisku ja liisk langes Mattiase peale, ja tema arvati ühena kaheteistkümne apostli hulka.