1Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
1Kui nelipühapäev kätte jõudis, olid nad kõik koos ühes paigas.
2Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
2Ja äkitselt tuli taevast kohin, otsekui tugev tuul oleks puhunud, ja täitis kogu koja, kus nad istusid.
3Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
3Ja nad nägid otsekui hargnevaid tulekeeli, mis laskusid iga üksiku peale nende seas.
4Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
4Ja nad kõik täideti Püha Vaimuga ning hakkasid rääkima teisi keeli, nõnda nagu Vaim neile andis rääkida.
5Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
5Jeruusalemmas oli aga elamas juute, vagasid mehi kõigi rahvaste keskelt, kes on taeva all.
6Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
6Kui nüüd see hääl kostis, tuli kokku nende kogukond, ja kõiki valdas hämmastus, sest igaüks kuulis räägitavat oma murret.
7Walistaajabu na kushangaa, wakisema, "Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
7Nad jahmusid ja panid imeks, öeldes: 'Ennäe, eks need kõik, kes räägivad, ole galilealased?
8Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
8Kuidas siis meist igaüks kuuleb oma sünnimaa murret?
9Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
9Meie, partlased ja meedlased ja eelamlased ja kes me elame Mesopotaamia-, Juuda- ja Kappadookiamaal, Pontoses ja Aasias,
10Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
10Früügias ja Pamfüülias, Egiptuses ja Liibüa maades Küreene pool, ja siia elama asunud roomlased,
11Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu."
11juudid ja nende usku pöördunud kreetlased ja araablased - kuidas me kuuleme räägitavat meie endi keeles Jumala suuri asju?'
12Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, "Hii ina maana gani?"
12Nad kõik olid jahmunud ja kahevahel ning ütlesid üksteisele: 'Mis see küll peab olema?'
13Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, "Watu hawa wamelewa divai mpya!"
13Mõned aga ütlesid pilgates: 'Nad on täis magusat veini!'
14Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: "Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
14Siis tõusis Peetrus koos nende üheteistkümnega püsti, tõstis häält ja kõneles neile: 'Juuda mehed ja kõik Jeruusalemma elanikud! Olgu see teil teada - pange tähele mu sõnu!
15Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
15Nemad ei ole sugugi joobnud, nagu te arvate, on ju alles kell üheksa hommikul.
16Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
16Vaid see on, mida prohvet Joel on öelnud:
17Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
17'Ja viimseil päevil sünnib, ütleb Jumal, et ma valan oma Vaimust välja kõigi inimeste peale ja teie pojad ja teie tütred ennustavad ja teie noored näevad nägemusi ja teie vanad näevad unenägusid,
18Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
18ning oma teenrite ja teenijate peale ma valan neil päevil välja oma Vaimust ja nad ennustavad,
19Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
19ning ma annan märke ülal taevas ja tunnustähti all maa peal: verd ja tuld ja suitsusambaid.
20jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
20Päike muutub pimedaks ja kuu vereks, enne kui tuleb Issanda päev, suur ja ülev.
21Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
21Ja sünnib, et igaüks, kes hüüab appi Issanda nime, päästetakse.'
22"Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
22Iisraeli mehed, kuulge neid sõnu: Jeesuse Naatsaretlase, mehe, kellele Jumal on tunnistuse andnud vägevate tegude ja märkide ja tunnustähtedega, mis Jumal tema läbi teie keskel tegi, nõnda kui te isegi teate,
23Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
23tema enda, kui ta oli Jumala määratud nõu ja etteteadmise järgi loovutatud, olete teie ülekohtuste inimeste kätega risti naelutades hukanud.
24Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
24Aga Jumal on tema üles äratanud, päästes ta surmavaludest, seepärast et surmal ei olnud väge teda pidada oma võimuses.
25Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
25Taavet ütleb tema kohta: 'Ma näen Issandat alati enese silme ees, sest ta on mu paremal pool, et ma ei kõiguks.
26Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
26Seepärast mu meel rõõmustab ja mu keel hõiskab, mu ihugi võib hingata lootuses,
27kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze.
27sest sa ei jäta mu hinge surmavalda ega anna oma Vagale näha kõdunemist.
28Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
28Sa oled mulle andnud teada elu tee, sa täidad mind rõõmuga oma palge ees.'
29"Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
29Mehed-vennad! Tohib ju avalikult teile öelda peavanem Taavetist, et ka tema on surnud ja maha maetud ja tema haud on meie juures tänini.
30Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
30Et ta oli prohvet ja teadis, et Jumal oli talle vandega tõotanud tema troonile seada istuma järglase ta niuete viljast,
31Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza.
31siis ta nägi ette ning rääkis Messia ülestõusmisest: 'Ei teda jäeta surmavalda ega näe ta liha kõdunemist.'
32Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
32Sellesama Jeesuse on Jumal üles äratanud surnuist, meie kõik oleme selle tunnistajad.
33Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
33Et ta nüüd Jumala parema käega on ülendatud, siis ta on saanud Isalt Püha Vaimu, nagu oli tõotatud, ning on selle välja valanud; seda teie nüüd näete ja kuuletegi.
34Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
34Taavet ei ole ju läinud taevasse, aga ta ütleb: 'Issand ütles mu Issandale: Istu mu paremale käele,
35hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
35kuni ma panen su vaenlased su jalajäriks!'
36"Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo."
36Kogu Iisraeli sugu teadku nüüd kindlasti, et Jumal on tema teinud Issandaks ja Messiaks, sellesama Jeesuse, kelle teie risti lõite!'
37Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: "Ndugu zetu, tufanye nini?"
37Seda kuuldes lõikas see neile südamesse ja nad ütlesid Peetrusele ja teistele apostlitele: 'Mida me peame tegema, mehed-vennad?'
38Petro akajibu, "Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
38Aga Peetrus ütles neile: 'Parandage meelt ja igaüks teist lasku ennast ristida Jeesuse Kristuse nimesse oma pattude andekssaamiseks, ning siis te saate Püha Vaimu anni.
39Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake."
39Sest see tõotus on antud teile ja teie lastele ning kõikidele, kes on eemal, keda iganes Jumal, meie Issand, enese juurde kutsub.'
40Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, "Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu."
40Veel paljude muudegi sõnadega veenis Peetrus neid ja manitses: 'Laske end päästa sellest sõgedast sugupõlvest!'
41Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
41Kes nüüd tema sõna vastu võtsid, need ristiti, ning sel päeval lisati nende hulka umbes kolm tuhat inimest.
42Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
42Aga nemad püsisid apostlite õpetuses ja osaduses, leivamurdmises ja palvetes.
43Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
43Ent igale inimesele tuli kartus, sest palju imetegusid ja tunnustähti sündis apostlite läbi.
44Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
44Kõik usklikud olid üheskoos ja kõik oli neil ühine.
45Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
45Omandi ja vara nad müüsid ära ning jagasid raha igaühele sedamööda, kuidas keegi vajas.
46Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
46Nad viibisid päevast päeva ühel meelel pühakojas, murdsid leiba kodudes ja võtsid rooga juubeldades ning siira südamega,
47Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.
47kiites Jumalat ja leides armu kogu rahva silmis. Issand aga lisas päästetuid päevast päeva nende hulka.