Swahili: New Testament

Estonian

Acts

3

1Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
1Peetrus ja Johannes läksid üles pühakotta palvusele, mida peeti pärastlõunal kella kolme ajal.
2Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao "Mlango Mzuri", palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
2Ja sinna kanti mees, kes oli sündimisest saadik jalutu. Ta pandi päevast päeva pühakoja selle ukse ette, mida nimetatakse Ilusaks väravaks, pühakotta minejailt almuseid paluma.
3Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
3Kui ta nägi Peetrust ja Johannest pühakotta astumas, palus ta neilt almust.
4Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, "Tutazame!"
4Siis Peetrus vaatas koos Johannesega teda ainiti ning ütles: 'Vaata meie peale!'
5Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
5Too jäigi neile otsa vaatama, lootes neilt midagi saada.
6Kisha Petro akamwambia, "Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!"
6Aga Peetrus ütles: 'Hõbedat ega kulda mul ei ole, aga mis mul on, seda ma annan sulle: Jeesuse Kristuse, Naatsaretlase nimel - tõuse ja kõnni!'
7Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
7Ja ta haaras kinni jalutu paremast käest ning aitas ta üles. Ja otsekohe said selle jalapöiad ja pahkluud tugevaks
8Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
8ning ta hüppas püsti, seisis ja kõndis ning läks koos nendega pühakotta sisse, käies ja hüpeldes ning Jumalat kiites.
9Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
9Ja kogu rahvas nägi teda kõndimas ja Jumalat kiitmas.
10Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule "Mlango Mzuri" wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
10Nad tundsid temas ära sama mehe, kes oli istunud almuse saamiseks pühakoja Ilusa värava ees, ja nad olid imestunud ja kohkunud sellest, mis temaga oli sündinud.
11Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa "Ukumbi wa Solomoni," ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
11Aga kui jalutu, kes oli terveks saanud, jäi Peetruse ja Johannese järel käima, jooksis kogu rahvahulk nende juurde kokku paika, mida kutsutakse Saalomoni sammaskäiguks.
12Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, "Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
12Seda nähes hakkas Peetrus rahvale kõnelema: 'Iisraeli mehed, miks te imestate selle üle või miks te ainiti vahite meid, otsekui meie oleksime oma erilise väe või jumalakartlikkusega selle mehe pannud kõndima?
13Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
13Aabrahami Jumal ja Iisaki Jumal ja Jaakobi Jumal, meie isade Jumal, on kirgastanud oma sulase Jeesuse, kelle teie olete reetnud ja ära salanud Pilaatuse palge ees, kui see oli otsustanud tema vabaks lasta.
14Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
14Teie salgasite ära Püha ja Õige ning palusite, et teile kingitaks mees, kes oli mõrtsukas.
15Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
15Teie tapsite Elu Juhi, aga Jumal on ta surnuist üles äratanud; selle tunnistajad oleme meie.
16Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
16Ja kuna tema siin, keda te näete ja tunnete, on uskunud Jeesuse nimesse, siis on see nimi teinud ta tugevaks, ja usk, mis tuleb Jeesuse läbi, on talle andnud täie tervise teie kõikide silma all.
17"Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
17Ja nüüd, vennad, ma tean, et te olete seda teinud teadmatusest just nagu teie ülemadki.
18Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
18Jumal on aga sel kombel täide saatnud kõigi oma prohvetite suu kaudu ennustatu, et tema Võitu peab kannatama.
19Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
19Parandage siis meelt ja pöörduge, et teie patud kustutataks,
20Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
20nii et Issandalt tuleksid kosumisajad ja ta läkitaks teie jaoks määratud Messia Jeesuse.
21Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani.
21Tema peab jääma taevasse kuni selle ajani, kui uuendatakse kõik, millest Jumal on rääkinud oma pühade prohvetite suu kaudu maailma algusest peale.
22Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
22Mooses on ju öelnud: 'Issand, teie Jumal, tõstab teile Prohveti teie vendade seast, seesuguse nagu mina. Teda kuulake kõiges, mida ta iial teile ütleb.
23Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
23Aga iga inimene, kes seda Prohvetit ei kuula, kaotatakse rahva seast ära.'
24Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
24Kõik prohvetid Saamuelist peale ja hiljem, niipalju kui nad on rääkinud, on ka neid päevi ette kuulutanud.
25Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
25Teie olete prohvetite ja selle lepingu lapsed, mille Jumal sõlmis teie isadega, kui ta Aabrahamile ütles: 'Ja sinu soos õnnistatakse kõiki maailma suguvõsasid.'
26Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake."
26Jumal on esmalt teile oma sulase Jeesuse üles äratanud ja teie juurde läkitanud teid õnnistama, kui te igaüks pöördute oma tigedusest.'