Swahili: New Testament

Estonian

Luke

12

1Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, "Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
1Sel ajal, kui rahvast oli kokku tulnud tuhandete kaupa, nii et üksteist tallati, hakkas Jeesus rääkima esmalt oma jüngritele: 'Hoidke end variseride haputaigna, see tähendab silmakirjalikkuse eest!
2Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
2Ei ole midagi varjatut, mis ei tuleks ilmsiks, ega peidetut, mida ei saadaks teada.
3Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
3Seepärast kõik, mida te ütlete pimedas, saab kuuldavaks valges, ja mida te üksteisele kõrva sosistate kambrites, seda kuulutatakse katustelt.
4"Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
4Teile aga, oma sõpradele, ma ütlen: Ärge kartke neid, kes ihu tapavad ja pärast seda ei saa midagi rohkemat teha!
5Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo.
5Ma näitan teile, keda teil tuleb karta: kartke teda, kellel on meelevald pärast tapmist heita põrgusse! Jah, ma ütlen teile, teda kartke!
6Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
6Eks müüda viis varblast kahe veeringu eest? Ja ükski neist ei ole unustatud Jumala ees.
7Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
7Isegi teie juuksekarvad on kõik ära loetud. Ärge kartke, te olete enam väärt kui hulk varblasi!
8"Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
8Aga ma ütlen teile, igaüht, kes mind tunnistab inimeste ees, teda tunnistab ka Inimese Poeg Jumala inglite ees,
9Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
9aga see, kes minu ära salgab inimeste ees, salatakse ära Jumala inglite ees.
10"Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
10Igaüks, kes ütleb midagi Inimese Poja kohta, võib saada andeks, aga kes teotab Püha Vaimu, sellele ei anta andeks.
11"Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
11Aga kui teid viiakse sünagoogidesse ja ülemate ja võimumeeste ette, ärge siis muretsege, kuidas või mida enese eest kosta või mida öelda,
12Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema."
12sest selsamal tunnil õpetab Püha Vaim teile, mida te peate ütlema.'
13Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, "Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba."
13Aga keegi rahva seast ütles Jeesusele: 'Õpetaja, ütle mu vennale, et ta jagaks päranduse minuga!'
14Yesu akamjibu, "Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?"
14Jeesus ütles talle: 'Inimene, kes mind on seadnud teie üle kohtumõistjaks või jagajaks?'
15Basi, akawaambia wote, "Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo."
15Ja ta ütles neile: 'Vaadake ette ja hoiduge igasuguse ahnuse eest, sest külluseski ei olene kellegi elu sellest, mis tal on!'
16Kisha akawaambia mfano: "Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
16Ja Jeesus rääkis neile ka tähendamissõna: 'Ühe rikka mehe põllumaa oli hästi vilja kandnud.
17Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
17Ja ta arutas endamisi: 'Mis ma pean tegema? Mul ei ole kohta, kuhu oma vilja koguda.'
18Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
18Ja ta ütles: 'Seda ma teen: ma lõhun maha oma aidad ja ehitan suuremad ning kogun sinna kõik oma vilja ja muu vara
19Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
19ning ütlen oma hingele: Hing, sul on tagavaraks palju vara mitmeks aastaks, puhka, söö, joo ja ole rõõmus!'
20Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?"
20Aga Jumal ütles talle: 'Sina arutu! Selsamal ööl nõutakse sinult su hing. Aga kellele jääb siis see, mis sa oled soetanud?'
21Yesu akamaliza kwa kusema "Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu."
21Nõnda on lugu sellega, kes kogub tagavara iseenese jaoks, kuid ei ole rikas Jumalas.'
22Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
22Aga Jeesus ütles jüngritele: 'Seepärast ma ütlen teile, ärge muretsege elu pärast, mida süüa, ega ihu pärast, millega rõivastuda,
23Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
23sest elu on enam kui toidus ja ihu enam kui rõivas.
24Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
24Vaadake kaarnaid - nad ei külva ega lõika, neil ei ole varakambrit ega aita, ning Jumal toidab neid. Kui palju enamat väärt olete teie lindudest!
25Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
25Aga kes teie seast suudab muretsemisega oma elueale küünra lisada?
26Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
26Kui te nüüd kõige vähematki ei suuda, mis te siis muu pärast muretsete?
27Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
27Vaadake lilli, kuidas nad ei ketra ega koo, aga ma ütlen teile, isegi Saalomon kogu oma hiilguses ei olnud nõnda ehitud kui igaüks neist.
28Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
28Kui aga Jumal nõnda rüütab väljal rohtu, mis täna on ja homme visatakse ahju, kui palju enam teid, te nõdrausulised!
29"Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
29Ja teiegi ärge küsige, mida süüa või mida juua, ja ärge olge kärsitud,
30Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
30sest kõike seda taotlevad maailma rahvad. Teie Isa ju teab, et te seda vajate.
31Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
31Pigem otsige tema kuningriiki, siis antakse kõik see teile pealegi!
32"Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
32Ära karda, sa pisike karjake, sest teie Isal on hea meel anda teile kuningriik!
33Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
33Müüge ära, mis teil on, ja andke see almusteks! Tehke enesele kulumatud kukrud ja muretsege enesele kahanematu aare taevas, kuhu varas ei saa ligi ja kus koi pole rikkumas,
34Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
34sest kus on teie aare, seal on ka teie süda.
35"Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
35Teie niuded olgu vöötatud ja lambid põlegu
36muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
36ja teie olge inimeste sarnased, kes ootavad oma isandat pulmapeolt koju, et kui ta tulles koputab, võiksid nad kohe talle ukse avada.
37Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
37Õndsad on need sulased, keda isand tulles leiab valvamas. Tõesti, ma ütlen teile, ta vöötab oma riided ja paneb nad lauda istuma ning tuleb ja teenib neid.
38Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
38Ja kui ta tuleks ka teisel või kolmandal öövalvekorral ja leiaks nad nõnda - õndsad on need!
39Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
39Küllap te mõistate, et kui peremees teaks, mil tunnil varas tuleb, siis ta ei laseks oma kotta sisse murda.
40Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
40Ka teie olge valmis, sest Inimese Poeg tuleb tunnil, mil te ei arvagi!'
41Petro akamwambia, "Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?"
41Aga Peetrus küsis: 'Issand, kas sa räägid selle tähendamissõna meile või kõikidele?'
42Bwana akajibu, "Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
42Ja Issand ütles: 'Kes küll on ustav ja arukas majapidaja, kelle isand seab oma pererahva üle neile parajal ajal andma määratud moona?
43Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
43Õnnis on see teener, kelle ta isand tulles leiab nõnda tegevat.
44Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
44Tõesti, ma ütlen teile, ta seab tema kogu oma vara üle.
45Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
45Aga kui see teener mõtleb oma südames: 'Mu isand viibib tulles', ning hakkab peksma sulaseid ja tüdrukuid, sööma ja jooma ning purjutama,
46bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
46siis selle teenri isand tuleb päeval, mil ta ei oota, ja tunnil, mida ta ei tea, ning raiub ta pooleks ja annab talle sama osa nendega, keda ei saa usaldada.
47Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
47Too teener, kes küll teadis oma isanda tahtmist, ent ei valmistanud ega teinud tema tahtmise järgi, saab palju peksa,
48Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
48kes aga ei teadnud, kuid tegi, mis on hoope väärt, saab peksa vähem. Igaühelt, kellele on antud palju, nõutakse palju, ja kelle hoolde on jäetud palju, sellelt küsitakse veel rohkem.
49"Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
49Tuld olen ma tulnud viskama maa peale, ja mida muud ma tahaksin, kui et see oleks juba süttinud!
50Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
50Aga mul on ees ristimine, millega mind ristitakse, ja kuidas mul on kitsas käes, kuni see on viidud lõpule!
51Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
51Kas te arvate, et ma olen tulnud rahu andma maa peale? Ma ütlen teile, ei sugugi, vaid hoopis lahkmeelt.
52Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
52Sest nüüdsest peale on viis ühes kojas lahkmeeles, kolm kahe vastu ja kaks kolme vastu,
53Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake."
53isa poja vastu ja poeg isa vastu, ema tütre vastu ja tütar ema vastu, ämm minia ja minia ämma vastu.'
54Yesu akayaambia tena makundi ya watu, "Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
54Aga Jeesus ütles ka rahvahulkadele: 'Kui te näete pilve tõusvat lääne poolt, siis te ütlete kohe: 'Raske sadu tuleb.' Ja nõnda sünnibki.
55Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
55Ja kui puhub lõunatuul, siis te ütlete: 'Kuum ilm tuleb.' Ja nõnda sünnib.
56Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
56Te silmakirjatsejad! Maa ja taeva nägu te oskate ära arvata, kuidas te siis seda aega ära ei arva?
57"Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
57Miks te siis iseeneste kohta ei otsusta, mis on õige?
58Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
58Sest see on nii: kui sa oma vastasega lähed ülema ette, püüa siis temaga asi lahendada teel, et ta sind ei veaks kohtuniku ette ja kohtunik ei annaks sind kohtuteenri kätte ja kohtuteener ei heidaks sind vangi.
59Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho."
59Ma ütlen sulle, sa ei pääse sealt enne välja, kui oled tagasi maksnud viimsegi leptoni.'