1Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
1Neil päevil sündis, et keiser Augustus andis käsu kirjutada üles kogu riigi rahvas.
2Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
2See esmakordne üleskirjutus toimus ajal, kui Küreenius oli Süüria maavalitseja.
3Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
3Ja kõik läksid ennast kirja panema igaüks oma linna.
4Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
4Nii läks ka Joosep Galileamaalt Naatsaretist üles Juudamaale Taaveti linna, mida hüütakse Petlemmaks, sest ta oli Taaveti soost ja pärusmaalt,
5Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
5et lasta end üles kirjutada koos Maarjaga, oma kihlatuga, kes oli lapseootel.
6Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
6Aga nende sealoleku aegu said päevad täis ja Maarja pidi sünnitama.
7akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
7Ta tõi ilmale oma esimese poja ning mähkis ta mähkmetesse ja asetas sõime, sest nende jaoks polnud majas kohta.
8Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
8Karjased olid seal paigus õitsil ja valvasid öösel oma karja.
9Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
9Issanda ingel seisatas nende juures ja Issanda kirkus säras nende ümber ja nad kartsid üliväga.
10Malaika akawaambia, "Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
10Aga ingel ütles neile: 'Ärge kartke! Sest vaata, ma kuulutan teile suurt rõõmu, mis saab osaks kogu rahvale,
11Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
11et teile on täna sündinud Taaveti linnas Päästja, kes on Issand Kristus.
12Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini."
12Ja see on teile tunnustäheks: te leiate lapsukese mähitud ja sõimes magavat.'
13Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
13Äkitselt olid koos ingliga taevased väed Jumalat kiitmas:
14"Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!"
14'Au olgu Jumalale kõrges ja maa peal rahu, inimestest hea meel!'
15Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: "Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha."
15Ja sündis, kui inglid olid nende juurest ära läinud taevasse, et karjased ütlesid üksteisele: 'Läki nüüd Petlemma, et näha saada seda, mis on sündinud, mis Issand on teatanud meile!'
16Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
16Ja nad läksid rutates ja leidsid Maarja ja Joosepi ja lapsukese, kes magas sõimes.
17Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
17Aga nähes teda teatasid nad sõnumist, mis neile oli räägitud selle lapse kohta.
18Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
18Kõik, kes kuulsid, panid seda imeks, mida karjased olid neile kõnelnud.
19Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
19Ent Maarja jättis kõik need lood meelde, mõtiskledes nende üle oma südames.
20Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
20Karjased pöördusid tagasi, ülistades ja kiites Jumalat kõige eest, mis nad olid kuulnud ja näinud. Kõik oli olnud nii, nagu neile oli räägitud.
21Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
21Kui kaheksa päeva sai täis ja tuli aeg lapse ümberlõikamiseks, siis pandi talle nimeks Jeesus, mille oli ütelnud ingel, enne kui laps sai ema ihusse.
22Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
22Ja kui nende puhastuspäevad Moosese Seaduse järgi said täis, viisid nad lapse üles Jeruusalemma, et teda seada Issanda ette,
23Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: "Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana."
23nõnda nagu on kirjutatud Issanda Seaduses: 'Iga poeglast, kes on avanud lapsekoja, hüütagu Issandale pühaks',
24Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
24ja et tuua Issanda Seaduses öeldu järgi ohvriks 'paar turteltuvi või kaks tuvipoega'.
25Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
25Ja vaata, Jeruusalemmas oli mees, Siimeon nimi. See mees oli õiglane ja vaga ning ootas Iisraeli lohutust, ja Püha Vaim oli tema peal.
26Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
26Püha Vaim oli talle ennustanud, et ta ei sure enne, kui ta on näinud Issanda Messiat.
27Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
27Ta tuli Vaimu ajel pühakotta. Ja kui vanemad tõid sinna lapse Jeesuse, et toimida temaga Seaduse sätte järgi,
28Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
28siis ta võttis tema sülle, ülistas Jumalat ja ütles:
29"Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
29'Issand, nüüd sa lased oma sulasel lahkuda rahus oma ütlust mööda,
30Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
30sest mu silmad on näinud sinu päästet,
31ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
31mille sa oled valmistanud kõigi rahvaste silme ees:
32Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli."
32valgust, mis on ilmutuseks paganaile, ja kirkust sinu rahvale Iisraelile.'
33Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
33Jeesuse isa ja ema panid seda imeks, mida tema kohta räägiti.
34Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, "Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
34Ja Siimeon õnnistas neid ja ütles Maarjale, tema emale: 'Vaata, see laps on seatud languseks ja tõusuks paljudele Iisraelis ja tähiseks, mille vastu räägitakse -
35na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako."
35ja sinu endagi hinge läbistab mõõk -, et tuleksid ilmsiks paljude südamete mõtted.'
36Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
36Seal oli ka prohvet Hanna, Penueli tütar, Aaseri suguharust, kes oli kõrgesse ikka jõudnud. Ta oli mehega elanud seitse aastat pärast oma neitsipõlve
37Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
37ja lesk olnud kuni kaheksakümne neljanda eluaastani. Tema ei lahkunud pühakojast, vaid teenis Jumalat ööd ja päevad paastumiste ja palvetamistega.
38Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
38Tema tuli sel tunnil sinna ja ülistas Jumalat ning kõneles Jeesusest kõigile, kes ootasid Jeruusalemma lunastust.
39Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
39Kui nad olid täitnud kõik, mis tuli teha Issanda Seaduse järgi, siis nad pöördusid tagasi Galileasse oma külla Naatsaretti.
40Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
40Laps aga kasvas ja sai tugevaks ning täitus tarkusega. Ja Jumala arm oli tema peal.
41Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
41Tema vanemad käisid igal aastal paasapühadel Jeruusalemmas.
42Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
42Kui Jeesus oli saanud kaheteistkümneaastaseks, läksid nad üheskoos pühadeaja kombe järgi üles Jeruusalemma.
43Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
43Kui nad olid pärast nende päevade möödumist teel kodu poole, jäi Jeesus Jeruusalemma, ent tema vanemad ei teadnud seda.
44Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
44Aga et nad arvasid tema olevat teekaaslaste seas, käisid nad ära ühe päeva tee ja hakkasid alles siis otsima teda sugulaste ja tuttavate juurest.
45Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
45Ja kui nad teda ei leidnud, pöördusid nad teda otsides tagasi Jeruusalemma.
46Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
46Kolme päeva pärast sündis, et nad leidsid Jeesuse pühakojas istumas õpetajate keskel neid kuulamas ja küsitlemas.
47Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
47Kõik, kes teda kuulsid, olid hämmastunud tema mõistusest ja ta vastustest.
48Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, "Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni."
48Ja Jeesuse vanemad olid teda nähes jahmunud ning ta ema ütles talle: 'Poeg, miks sa oled meile nõnda teinud? Vaata, su isa ja mina oleme sind südamevaluga otsinud.'
49Yeye akawajibu, "Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?"
49Ent tema ütles neile: 'Miks te siis olete mind otsinud? Kas te ei teadnud, et ma pean olema neis paigus, mis on mu Isa päralt?'
50Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
50Aga nemad ei mõistnud neid sõnu, mis ta neile rääkis.
51Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
51Jeesus läks koos nendega ja tuli Naatsaretti ning oli neile allaheitlik. Tema ema hoidis kõik need lood oma südames alal.
52Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
52Ja Jeesus kasvas tarkuses ja pikkuses ja armus Jumala ja inimeste juures.