1Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
1Keiser Tibeeriuse valitsemise viieteistkümnendal aastal, kui Pontius Pilaatus oli Judea maavalitseja ja Heroodes Galilea nelivürst, tema vend Filippus aga Iturea ja Trahhoniitisemaa nelivürst ja Lüsaanias Abileene nelivürst,
2na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
2kui Hannas ja Kaifas olid ülempreestrid, sai Jumala sõna Sakariase poja Johannese kätte kõrbes.
3Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
3Ta käis läbi kogu Jordani ümberkaudse maa ja kuulutas meeleparandusristimist pattude andeksandmiseks,
4Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
4nagu on kirjutatud prohvet Jesaja sõnade raamatusse: 'Hüüdja hääl on kõrbes: Valmistage Issandale tee, tehke tasaseks tema teerajad!
5Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
5Kõik kuristikud täidetagu ning kõik mäed ja kingud tasandatagu, ja kõverikud saagu sirgeks, ja mis konarlik, siledaks teeks,
6Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."
6siis saavad kõik inimesed näha Jumala päästet!'
7Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
7Johannes ütles nüüd rahvale, kes oli tulnud, et lasta ennast temal ristida: 'Rästikute sugu, kes teid on hoiatanud põgenema tulevase viha eest?
8Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
8Kandke nüüd meeleparandusele kohaseid vilju ja ärge hakake iseenestes ütlema: 'Meie isa on ju Aabraham.' Sest ma ütlen teile: Jumal võib neist kividest äratada Aabrahamile lapsi.
9Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni."
9Kirves on juba pandud puude juurte külge. Iga puu nüüd, mis ei kanna head vilja, raiutakse maha ja visatakse tulle.'
10Umati wa watu ukamwuliza, "Tufanye nini basi?"
10Rahvahulgad küsisid Johanneselt: 'Mis meil siis tuleb teha?'
11Akawajibu, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."
11Aga tema kostis: 'Kellel on kaks särki, jagagu sellele, kellel ei ole, ning kellel on toitu, tehku niisamuti!'
12Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, "Mwalimu, tufanye nini?"
12Ent ka tölnereid tuli, et lasta ennast ristida, ja nemad ütlesid: 'Õpetaja, mis meil tuleb teha?'
13Naye akawaambia, "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."
13Tema ütles neile: 'Ärge nõudke rohkem, kui teie jaoks on seatud!'
14Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?" Naye akawajibu, "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."
14Aga temalt küsisid ka sõjamehed: 'Ja meie, mis meil tuleb teha?' Tema ütles neile: 'Ärge tehke kellelegi liiga, ärge olge väljapressijad, leppige oma palgaga!'
15Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
15Rahvas oli täis ootust ja kõik mõtlesid oma südames, et ehk Johannes ongi Messias.
16Hapo Yohane akawaambia wote, "Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
16Siis vastas Johannes kõikidele: 'Mina ristin teid veega, aga on tulemas minust vägevam, kelle jalatsipaelagi ei kõlba ma lahti päästma. Tema ristib teid Püha Vaimu ja tulega.
17Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika."
17Temal on visklabidas käes, et puhastada oma rehealust ja koguda nisud oma aita, kuid aganad põletab ta ära kustumatu tulega.'
18Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
18Ka veel paljude muude asjade pärast manitsedes kuulutas Johannes rahvale rõõmusõnumit.
19Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
19Aga kui nelivürst Heroodes sai Johannese käest noomida oma venna Filippuse naise Heroodiase ja kõigi pahategude pärast, mida Heroodes oli teinud,
20Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
20sai ta hakkama veel sellega, et pani Johannese vangi.
21Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
21Ent sündis, kui kogu rahvast ristiti ja ka Jeesus oli ristitud ja palvetas, et taevas avanes
22na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
22ja Püha Vaim laskus ihulikul kujul Jeesuse peale kui tuvi, ja taevast kostis hääl: 'Sina oled mu armas Poeg, sinust on mul hea meel!'
23Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
23Ja Jeesus oli oma tegevust alustades umbes kolmkümmend aastat vana, ja oli, nagu oletati, Joosepi poeg, see oli Eeli,
24Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
24see oli Mattati, see oli Leevi, see oli Malki, see oli Jannai, see oli Joosepi,
25mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
25see oli Mattitjahu, see oli Aamose, see oli Nahumi, see oli Hesli, see oli Naggai,
26mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
26see oli Mahati, see oli Mattitjahu, see oli Simei, see oli Jooseki, see oli Jooda,
27mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
27see oli Joohanani, see oli Reesa, see oli Serubbaabeli, see oli Sealtieli, see oli Neeri,
28mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
28see oli Melki, see oli Addi, see oli Koosami, see oli Elmadami, see oli Eeri,
29mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
29see oli Jeesuse, see oli Elieseri, see oli Joorimi, see oli Mattati, see oli Leevi,
30mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
30see oli Siimeoni, see oli Juuda, see oli Joosepi, see oli Joonami, see oli Eljakimi,
31mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
31see oli Melea, see oli Menna, see oli Mattata, see oli Naatani, see oli Taaveti,
32mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
32see oli Iisai, see oli Oobedi, see oli Boase, see oli Salma, see oli Nahsoni,
33mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
33see oli Amminadabi, see oli Admini, see oli Arni, see oli Hesroni, see oli Peretsi, see oli Juuda,
34mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
34see oli Jaakobi, see oli Iisaki, see oli Aabrahami, see oli Terahi, see oli Naahori,
35mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
35see oli Serugi, see oli Reu, see oli Pelegi, see oli Eeberi, see oli Selahi,
36mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
36see oli Keenani, see oli Arpaksadi, see oli Seemi, see oli Noa, see oli Lemeki,
37mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
37see oli Metuusala, see oli Eenoki, see oli Jeredi, see oli Mahalaleli, see oli Keenani,
38mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.
38see oli Enose, see oli Seti, see oli Aadama, see oli Jumala poeg.