1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
1Aga lähenes hapnemata leibade püha, mida hüütakse paasaks,
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
2ning ülempreestrid ja kirjatundjad otsisid võimalust, kuidas Jeesust hukata, sest nad kartsid rahvast.
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
3Aga saatan oli läinud Juuda sisse, keda hüüti Iskariotiks, kes oli nende kaheteistkümne hulgast,
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
4ja Juudas läks ja rääkis kokku ülempreestrite ja templivalvuritega selles, kuidas ta saaks Jeesuse ära anda nende kätte.
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
5Ja nad said rõõmsaks ja leppisid temaga kokku, et nad annavad talle raha.
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
6Ja Juudas nõustus ning hakkas otsima Jeesuse äraandmiseks parajat aega, mil rahvahulka pole ta ümber.
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
7Saabus hapnemata leibade püha, mil paasatall pidi tapetama,
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
8ja Jeesus läkitas Peetruse ja Johannese ning ütles: 'Minge ja valmistage meile paasa, et me seda sööksime!'
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
9Nemad küsisid temalt: 'Kuhu sa tahad, et me selle valmistaksime?'
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
10Tema ütles neile: 'Vaata, kui te lähete linna sisse, siis te kohtate veekruusi kandvat inimest. Minge temaga kaasa sinna majja, kuhu ta sisse astub,
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
11ja ütelge selle maja peremehele: 'Õpetaja ütleb sulle: Kus on võõrastetuba, kus ma võiksin süüa paasat oma jüngritega?'
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
12Siis too näitab teile suurt vaipadega kaetud ülemist tuba, seal valmistage!'
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
13Nad läksid ja leidsid nõnda, nagu Jeesus neile oli öelnud. Ja nad valmistasid paasasöömaaja.
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
14Ja kui tund tuli, istus Jeesus maha ja apostlid koos temaga.
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
15Ja ta ütles neile: 'Ma olen südamest igatsenud seda paasat süüa teiega enne oma kannatamist,
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
16sest ma ütlen teile, ma ei söö seda enam, kuni kõik on läinud täide Jumala riigis.'
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
17Ja ta võttis karika, tänas ning ütles: 'Võtke see ning jagage eneste vahel!
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
18Sest ma ütlen teile, mina ei joo nüüdsest peale viinapuu viljast, kuni Jumala riik on tulnud.'
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
19Ja ta võttis leiva, tänas ja murdis ja andis neile, öeldes: 'See on minu ihu, mis teie eest antakse. Seda tehke minu mälestuseks!'
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
20Selsamal kombel võttis ta ka karika pärast õhtusöömaaega ja ütles: 'See karikas on uus leping minu veres, mis teie eest valatakse.
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
21Siiski, vaata, minu äraandja käsi on minuga lauas,
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
22sest Inimese Poeg läheb küll ära, nii nagu see on määratud, ometi häda sellele inimesele, kes ta ära annab!'
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
23Ja nemad hakkasid omavahel arutama, kes see küll võiks nende seast olla, kes seda kavatseb teha.
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
24Aga nende seas tõusis ka vaidlus, keda nendest tuleks arvata teistest suuremaks.
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
25Ent Jeesus ütles neile: 'Rahvaste kuningad peremehetsevad nende üle ja neid, kes nende kallal meelevallatsevad, hüütakse 'heategijaiks'.
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
26Nõnda ei tohi olla teie seas, vaid suurim teie seas olgu nagu noorim, ja juht nagu see, kes teenib.
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
27Sest kumb on suurem, kas see, kes istub lauas, või see, kes teenib? Eks see, kes istub lauas? Ent mina olen teie seas nõnda nagu see, kes teenib.
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
28Aga teie olete need, kes minu juures on püsinud mu kiusatustes,
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
29ja mina sean teile kuningriigi, nõnda nagu minu Isa mulle on seadnud,
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
30et te sööksite ja jooksite minu lauas minu riigis ja istuksite troonidel, mõistes kohut Iisraeli kaheteistkümnele suguharule.
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
31Siimon, Siimon, vaata, saatan on väga püüdnud sõeluda teid nagu nisu!
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
32Aga mina olen sinu pärast Jumalat palunud, et su usk ei lõpeks. Ja kui sa ükskord pöördud, siis kinnita oma vendi!'
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
33Peetrus ütles talle: 'Issand, ma olen valmis minema sinuga niihästi vangi kui surma!'
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
34Jeesus aga ütles: 'Ma ütlen sulle, Peetrus, kukk ei laula täna enne, kui sa oled kolm korda salanud, et sa mind tunned!'
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
35Ja Jeesus ütles neile: 'Kui ma läkitasin teid kukruta ja paunata ja jalatsiteta, kas teil oli midagi puudu?' Nemad ütlesid: 'Ei midagi.'
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
36Siis ta ütles neile: 'Kuid nüüd, kellel on kukkur, võtku see kaasa, nõndasamuti ka paun, ja kellel ei ole, see müügu ära oma kuub ja ostku mõõk!
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
37Sest ma ütlen teile, minus peab minema täide, mis on kirjutatud: Ta on ülekohtuste sekka arvatud. Sest ka see, mis minu kohta käib, on lõpul.'
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
38Aga nemad ütlesid: 'Issand, ennäe, siin on kaks mõõka.' Tema ütles neile: 'Sellest on küllalt.'
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
39Ja Jeesus läks välja ning tuli harjumuspäraselt Õlimäele, ja jüngrid järgnesid talle.
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
40Ja kui ta sinna paika jõudis, siis ta ütles neile: 'Palvetage, et te ei satuks kiusatusse!'
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
41Ta ise läks neist eemale kiviviske kaugusele, langes põlvili maha ja palvetas:
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
42'Isa, kui sa tahad, võta see karikas minult ära! Ometi ärgu sündigu minu tahtmine, vaid sinu oma!'
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
43[Siis ilmus talle ingel taevast teda kinnitama.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
44Ja raskesti heideldes palvetas ta veelgi pingsamalt, ja ta higi muutus nagu maha tilkuvateks verepiiskadeks.]
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
45Ja palvetamast tõustes tuli Jeesus oma jüngrite juurde ja leidis nad magamas kurbuse pärast.
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
46Ja ta ütles neile: 'Miks te magate? Tõuske üles ja palvetage, et te ei satuks kiusatusse!'
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
47Kui Jeesus alles rääkis, vaata, tuli rahvajõuk, ja see, keda hüüti Juudaks - üks neist kaheteistkümnest -, käis nende ees ja astus Jeesuse juurde talle suud andma.
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
48Aga Jeesus ütles talle: 'Juudas, kas sa annad Inimese Poja suudlusega ära?'
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
49Kui tema jüngrid nägid, mis on tulemas, ütlesid nad: 'Issand, kas me lööme nüüd mõõgaga sekka?'
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
50Ja üks neist lõigi ülempreestri sulast ning raius ära tema parema kõrva.
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
51Aga Jeesus kostis: 'Jätke see!' Ja ta puudutas tema kõrva ja tegi ta terveks.
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
52Aga Jeesus ütles ülempreestritele ja templivalvuritele ja vanematele, kes tema vastu olid tulnud: 'Kas te olete nagu teeröövli kallale tulnud mõõkade ja nuiadega?
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
53Kui ma olin päevast päeva teie juures pühakojas, siis te ei pannud käsi mu külge. Kuid see on teie tund ja pimeduse meelevald.'
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
54Aga nad võtsid Jeesuse kinni ja viisid ära ja tõid ülempreestri majja. Ent Peetrus järgnes eemalt.
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
55Ja kui nad keset õue tule süütasid ja üheskoos maha istusid, istus ka Peetrus nende sekka.
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
56Aga üks teenijatüdruk nägi teda tule valgel istuvat ja ütles ainiti tema peale vaadates: 'Ka tema oli koos Jeesusega.'
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
57Peetrus aga salgas: 'Naine, ma ei tunne teda.'
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
58Natukese aja pärast lausus üks mees Peetrust nähes: 'Ka sina oled nende seast.' Peetrus aga lausus: 'Inimene, ma ei ole.'
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
59Ja umbes tund aega hiljem kinnitas seda keegi teine: 'Tõepoolest, ka tema oli Jeesusega, ta on ju galilealane.'
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
60Peetrus aga ütles: 'Inimene, ma ei mõista, mida sa räägid.' Ja otsekohe, kui ta alles rääkis, laulis kukk.
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
61Ning Issand pöördus ja vaatas Peetrusele otsa ja Peetrusele tuli meelde Issanda sõna, kuidas ta temale oli öelnud: 'Enne kui täna kukk laulab, salgad sina mu kolm korda ära.'
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
62Ja sealt välja minnes puhkes ta kibedasti nutma.
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
63Aga mehed, kes Jeesust kinni pidasid, teotasid teda ja peksid.
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
64Nad katsid kinni ta silmad ja küsisid temalt: 'Ütle prohvetlikult, kes see on, kes sind lõi?'
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
65Ja nad teotasid teda paljude pilkesõnadega.
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
66Ja kui valgeks läks, kogunes rahva vanematekogu, ülempreestrid ja ka kirjatundjad, ning nad viisid Jeesuse Suurkohtu ette
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
67ja ütlesid: 'Kui sina oled Messias, siis ütle meile!' Aga tema ütles neile: 'Kui ma teile ütleksin, ei usuks te mitte,
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
68ja kui ma küsiksin, ei vastaks te mitte.
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
69Ent nüüdsest peale istub Inimese Poeg Jumala väe paremal käel.'
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
70Aga nad kõik ütlesid: 'Sina oled siis Jumala Poeg?' Aga Jeesus lausus neile: 'Need on teie sõnad, et mina olen.'
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."
71Nemad aga ütlesid: 'Mis tunnistust meil veel on vaja? Oleme ju ise seda kuulnud tema suust!'