Swahili: New Testament

Estonian

Luke

8

1Baada ya hayo, Yesu alipitia katika miji na vijiji akitangaza Habari Njema za Ufalme wa Mungu. Wale kumi na wawili waliandamana naye.
1Mõni aeg hiljem rändas Jeesus linnast linna ja külast külla ning jutlustas ning kuulutas evangeeliumi Jumala riigist. Ja need kaksteist olid temaga
2Pia wanawake kadhaa ambao Yesu alikuwa amewatoa pepo wabaya na kuwaponya magonjwa, waliandamana naye. Hao ndio akina Maria (aitwaye Magdalene), ambaye alitolewa pepo wabaya saba;
2ja mõned naised, keda ta oli teinud terveks kurjadest vaimudest ja haigustest: Maarja, keda hüütakse Magdaleenaks, kellest seitse kurja vaimu oli välja läinud,
3Yoana, mke wa Kuza, mfanyakazi mkuu wa Herode; Susana na wengine kadhaa. Hao wanawake walikuwa wakiwatumikia kwa mali yao wenyewe.
3ja Johanna, Heroodese varahoidja Kuusase naine, ja Susanna ja palju teisi, kes neid aitasid oma varaga.
4Kundi kubwa la watu lilikuwa linakusanyika, na watu walikuwa wanamjia Yesu kutoka kila mji. Naye akawaambia mfano huu:
4Aga kui rahvahulki kogunes ja kõigist linnadest Jeesuse juurde tuli, rääkis ta neile tähendamissõnaga:
5"Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akipanda zile mbegu, nyingine zilianguka njiani, na wapita njia wakazikanyaga, na ndege wakazila.
5'Külvaja läks välja oma seemet külvama. Ja külvamisel pudenes osa seemet tee äärde ning tallati ära ja taeva linnud nokkisid selle.
6Nyingine zilianguka penye mawe, na baada ya kuota zikanyauka kwa kukosa maji.
6Ja osa kukkus kaljule, ja see kuivas tärgates, sest sel ei olnud niiskust.
7Nyingine zilianguka kati ya miti ya miiba. Ile miti ya miiba ilipoota ikazisonga.
7Ja osa kukkus ohakate keskele, ja samal ajal tärganud ohakad lämmatasid selle.
8Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikaota na kuzaa asilimia mia." Baada ya kusema hayo, akapaaza sauti, akasema, "Mwenye masikio na asikie!"
8Ja osa kukkus heasse mulda, ja kui see tärkas, kandis see sajakordselt vilja.' Seejärel ta hüüdis: 'Kel kõrvad on kuulda, kuulgu!'
9Wanafunzi wake wakamwuliza Yesu maana ya mfano huo.
9Jeesuse jüngrid küsisid temalt, mida see tähendamissõna tähendab.
10Naye akajibu, "Ninyi mmejaliwa kujua siri za Ufalme wa Mungu, lakini hao wengine sivyo; ila hao huambiwa kwa mifano, ili wakitazama wasiweze kuona, na wakisikia wasifahamu.
10Jeesus ütles: 'Teile on antud ära tunda Jumala riigi saladusi, aga muudele inimestele on kõik tähendamissõnades, et nad vaadates ei näeks ja kuuldes ei mõistaks.
11"Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu.
11See tähendamissõna aga tähendab: seeme on Jumala sõna.
12Zile zilizoanguka njiani zinaonyesha watu wale wanaosikia lile neno, halafu Ibilisi akaja na kuliondoa mioyoni mwao wasije wakaamini na hivyo wakaokoka.
12Teeäärsed on need, kes kuulevad, aga pärast tuleb kurat ja võtab sõna ära nende südamest, et nad ei usuks ega pääseks.
13Zile zilizoanguka penye mawe zinaonyesha watu wale ambao wanaposikia juu ya lile neno hulipokea kwa furaha. Hata hivyo, kama zile mbegu, watu hao hawana mizizi maana husadiki kwa kitambo tu, na wanapojaribiwa hukata tamaa.
13Kaljupealsed on need, kes kuuldes võtavad sõna rõõmuga vastu, ent neil ei ole juurt, üürikest aega nad usuvad, ent kiusatuse ajal taganevad ära.
14Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni watu wale wanaosikia lile neno, lakini muda si muda, wanapokwenda zao, husongwa na wasiwasi, mali na anasa za maisha, na hawazai matunda yakakomaa.
14Mis ohakate sekka kukkus, on aga need, kes sõna küll kuulsid, ent edaspidi lämmatavad neid muretsemised ja rikkus ja elulõbud ning nende vili ei saa küpseks.
15Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale wanaolisikia lile neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na wa utii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda.
15Aga mis on heas mullas, on need, kes sõna kuuldes seda kaunis ja heas südames säilitavad ja kannatlikkuses vilja kannavad.
16"Watu hawawashi taa na kuifunika kwa chombo au kuiweka mvunguni. Lakini huiweka juu ya kinara ili watu wanapoingia ndani wapate kuona mwanga.
16Aga ükski, kes on süüdanud lambi, ei kata seda astjaga kinni ega pane voodi alla, vaid paneb selle lambijalale, et tuppa astujad näeksid valgust.
17"Chochote kilichofichwa kitafichuliwa na siri yoyote itagunduliwa na kujulikana hadharani.
17Sest midagi ei ole peidetut, mis ei saaks avalikuks, ei ole ka midagi varjul, mis ei saaks teatavaks ega tuleks ilmsiks.
18"Kwa hiyo, jihadharini jinsi mnavyosikia; maana aliye na kitu ataongezewa, lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani kuwa anacho, kitachukuliwa."
18Pidage siis silmas, kuidas te kuulete! Sest kellel on, sellele antakse, ja kellel ei ole, sellelt võetakse seegi, mis ta arvab enesel olevat.'
19Hapo mama na ndugu zake Yesu wakamjia, lakini hawakuweza kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu.
19Siis tulid Jeesuse juurde tema ema ja ta vennad, kuid ei saanud temaga rahvahulga tõttu kokku.
20Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumwona.
20Ja talle teatati: 'Sinu ema ja su vennad seisavad väljas ja tahavad sind näha.'
21Lakini Yesu akawaambia watu wote, "Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika."
21Aga Jeesus kostis: 'Minu ema ja mu vennad on need, kes Jumala sõna kuulevad ja selle järgi teevad.'
22Siku moja, Yesu alipanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, "Tuvuke ziwa twende mpaka ng'ambo." Basi, wakaanza safari.
22Ühel päeval aga sündis, et Jeesus ja ta jüngrid astusid paati ja tema ütles neile: 'Sõitkem üle järve vastaskaldale!' Ja nad asusid teele.
23Walipokuwa wanasafiri kwa mashua, Yesu alishikwa na usingizi, akalala. Dhoruba kali ikaanza kuvuma, maji yakaanza kuingia ndani ya mashua, wakawa katika hatari.
23Aga purjetamise ajal jäi ta magama. Ja järvel tõusis tuulispea ja uhtis paadi vett täis ning nad olid hädaohus.
24Wale wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwamsha wakisema, "Bwana, Bwana! Tunaangamia!" Yesu akaamka, akaikemea dhoruba na mawimbi, navyo vikatulia, kukawa shwari.
24Siis nad astusid tema juurde, äratasid ta üles ja ütlesid: 'Õpetaja, Õpetaja, me hukkume!' Tema tõusis, sõitles tuult ja veemöllu ja need vaibusid ning järv jäi vaikseks.
25Kisha akawaambia, "Iko wapi imani yenu?" Lakini wao walishangaa na kuogopa huku wakiambiana, "Huyu ni nani basi, hata anaamuru dhoruba na mawimbi, navyo vinamtii?"
25Jeesus ütles neile: 'Kus on teie usk?' Aga nemad lõid kartma ja imestasid, öeldes üksteisele: 'Kes küll tema on, et ta käsutab ka tuuli ja vett ning need kuulavad tema sõna?'
26Wakaendelea na safari, wakafika pwani ya nchi ya Wagerase inayokabiliana na Galilaya, ng'ambo ya ziwa.
26Ja nad purjetasid gerasalaste maale, mis on Galilea vastaskaldal.
27Alipokuwa anashuka pwani, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo alimjia kutoka mjini. Kwa muda mrefu mtu huyo, hakuwa anavaa nguo, wala hakuwa anaishi nyumbani bali makaburini.
27Aga kui Jeesus astus maale, juhtus talle vastu üks linnast tulnud mees, kel oli kuri vaim. Ammust ajast ei kandnud ta enam riideid ega elanud majas, vaid surnuhaudades.
28Alipomwona Yesu, alipiga kelele na kujitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kubwa "We, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu una shauri gani nami? Ninakusihi usinitese!"
28Aga Jeesust nähes hakkas ta karjuma, heitis tema ette maha ja hüüdis valju häälega: 'Mis on mul sinuga asja, Jeesus, Kõigekõrgema Jumala Poeg? Ma anun sind, ära mind piina!'
29Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikwishamwambia huyo pepo mchafu amtoke mtu huyo. Pepo huyo mchafu alikuwa anamvamia mtu huyo mara nyingi, na ingawa watu walimweka ndani na kumfunga kwa minyororo na pingu, lakini kila mara alivivunja vifungo hivyo, akakimbizwa na pepo huyo mchafu hadi jangwani.
29Jeesus oli käskinud rüvedat vaimu inimesest välja minna. See oli ju teda kaua aega vaevanud, ja meest oli ahelatega seotud ja pandud jalaraudu, aga iga kord oli ta kiskunud köidikud katki ja kuri vaim oli teda kihutanud tühermaile.
30Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Yeye akajibu, "Jina langu ni Jeshi" --kwa sababu pepo wengi walikuwa wamempagaa.
30Jeesus aga küsis temalt: 'Mis su nimi on?' Tema ütles: 'Leegion.' Sest temasse oli läinud palju kurje vaime.
31Hao pepo wakamsihi asiwaamuru wamtoke na kwenda kwenye shimo lisilo na mwisho.
31Ja need palusid Jeesust, et ta ei käsiks neid sügavikku minna.
32Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha mlimani. Basi, hao pepo wakamsihi awaruhusu wawaingie. Naye Yesu akawapa ruhusa.
32Aga seal oli suur seakari mäe peal söömas. Ja nad palusid teda, et ta annaks neile loa minna nende sisse, ja Jeesus andis neile loa.
33Kwa hiyo pepo hao wakamtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nao wakaporomoka kwenye ule mteremko mkali, wakatumbukia ziwani, wakazama majini.
33Kui kurjad vaimud sellest inimesest olid välja läinud, läksid nad sigadesse. Ja kari sööstis järsakult järve ning uppus.
34Wale wachungaji walipoona yote yaliyotokea walikimbia, wakaenda kuwapa watu habari, mjini na mashambani.
34Aga kui karjased nägid, mis oli sündinud, põgenesid nad ja kuulutasid sellest linnas ja maal.
35Watu wakaja kuona yaliyotokea. Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo ameketi karibu na Yesu, amevaa nguo, ana akili zake, wakaogopa.
35Siis inimesed tulid juhtunut vaatama. Kui nad tulid Jeesuse juurde ja leidsid inimese, kellest kurjad vaimud olid välja läinud, rõivastatult ja selge aruga Jeesuse jalgade ees istumas, lõid nad kartma.
36Wale watu walioshuhudia tukio hilo waliwaeleza hao jinsi yule mtu alivyoponywa.
36Ja pealtnägijad kuulutasid neile, kuidas kurjadest vaimudest vaevatu oli pääsenud.
37Wakazi wa nchi ya Gerase walishikwa na hofu kubwa. Kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke, aende zake. Hivyo Yesu alipanda tena mashua, akaondoka.
37Ja kõik Gerasa ümbruskonna elanikud palusid Jeesust, et ta läheks ära nende juurest, sest suur kartus oli neid vallanud. Siis astus Jeesus paati ning pöördus tagasi.
38Yule mtu aliyetokwa na wale pepo akamsihi aende pamoja naye. Lakini Yesu hakumruhusu, bali akamwambia,
38Mees aga, kellest kurjad vaimud olid välja läinud, anus Jeesust, et ta tohiks jääda temaga. Ent Jeesus saatis ta minema ja ütles:
39"Rudi nyumbani ukaeleze yote Mungu aliyokutendea." Basi, yule mtu akaenda akitangaza kila mahali katika mji ule mambo yote Yesu aliyomtendea.
39'Pöördu tagasi oma koju ja jutusta, mida kõike Issand sulle on teinud!' Ja mees läks ja kuulutas mööda kogu linna, mida kõike Jeesus temale oli teinud.
40Yesu aliporudi upande mwingine wa ziwa, kundi la watu lilimkaribisha, kwa maana wote walikuwa wanamngojea.
40Aga kui Jeesus tagasi pöördus, võttis teda vastu rahvahulk, sest nad kõik ootasid teda.
41Hapo akaja mtu mmoja aitwaye Yairo, ofisa wa sunagogi. Alijitupa miguuni pa Yesu, akamwomba aende nyumbani kwake,
41Ja vaata, tuli mees, nimega Jairus, ta oli sünagoogi ülem. Ja ta langes Jeesuse jalge ette ning palus teda tulla oma koju,
42kwa kuwa binti yake wa pekee, mwana wa pekee mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa mahututi. Yesu alipokuwa akienda, watu wakawa wanamsonga kila upande.
42sest tal oli üksainus tütar, umbes kaksteist aastat vana, ja see oli suremas. Aga Jeesuse sinnaminekul tungles rahvahulk tema ümber.
43Kulikuwa na mwanamke mmoja kati ya lile kundi la watu, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote kwa waganga, hakuna aliyefaulu kumponya.
43Ja üks naine, kes oli veritõves olnud kaksteist aastat ja arstide peale ära kulutanud kogu oma vara, ning keda ükski ei olnud suutnud terveks teha,
44Huyo mwanamke alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake. Papo hapo akaponywa ugonjwa wake wa kutokwa damu.
44see tuli Jeesuse selja taha ja puudutas ta kuue palistust. Ja otsekohe lakkas ta verejooks.
45Yesu akasema, "Ni nani aliyenigusa?" Wote wakasema kwamba hapakuwa na mtu aliyemgusa. Naye Petro akasema, "Mwalimu, umati wa watu umekuzunguka na kukusonga!"
45Ja Jeesus küsis: 'Kes puudutas mind?' Aga kui kõik eitasid, ütles Peetrus: 'Õpetaja, rahvahulgad lausa tungivad su peale ja rõhuvad sind.'
46Lakini Yesu akasema, "Kuna mtu aliyenigusa, maana nimehisi nguvu imenitoka."
46Aga Jeesus ütles: 'Keegi puudutas mind, sest ma tundsin väge enesest välja minevat.'
47Yule mwanamke alipoona kwamba hawezi kujificha, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa mbele ya Yesu. Hapo akaeleza mbele ya wote kisa cha kumgusa Yesu na jinsi alivyoponyeshwa mara moja.
47Kui naine nägi, et ta ei saa varjule jääda, tuli ta värisedes ja langes Jeesuse ette maha ja kuulutas kogu rahva ees, mis põhjusel ta oli Jeesust puudutanud ja kuidas ta otsekohe oli paranenud.
48Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani."
48Jeesus aga ütles naisele: 'Tütar, sinu usk on su päästnud, mine rahuga!'
49Alipokuwa bado akiongea, Yairo akaletewa habari kutoka nyumbani: "Binti yako ameshakufa, ya nini kumsumbua Mwalimu zaidi?"
49Kui ta alles rääkis, tuli keegi sünagoogi ülema perest ja ütles: 'Su tütar on surnud, ära tülita enam Õpetajat!'
50Yesu aliposikia hayo akamwambia Yairo, "Usiogope; amini tu, naye atapona."
50Aga seda kuuldes Jeesus vastas Jairusele: 'Ära karda, usu ainult, ja ta pääseb!'
51Alipofika nyumbani hakumruhusu mtu kuingia ndani pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohane, Yakobo na wazazi wa huyo msichana.
51Kui ta siis läks majja, ei lasknud ta kedagi endaga koos sisse tulla peale Peetruse ja Johannese ja Jaakobuse ning lapse isa ja ema.
52Watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili yake. Lakini Yesu akawaambia, "Msilie, kwa maana mtoto hajafa, amelala tu!"
52Kõik nutsid ja halisesid tütarlapse pärast. Aga Jeesus ütles: 'Ärge nutke, ta ei ole surnud, vaid magab!'
53Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.
53Ja nad naersid tema üle, teades, et tütarlaps on surnud.
54Lakini Yesu akamshika mkono akasema, "Mtoto amka!"
54Aga Jeesus hüüdis tüdruku käest kinni võttes: 'Tütarlaps, ärka üles!'
55Roho yake ikamrudia, akaamka mara. Yesu akaamuru wampe chakula.
55Ja vaim pöördus tüdrukusse tagasi ja ta tõusis otsekohe üles. Ja Jeesus käskis talle süüa anda.
56Wazazi wake walishangaa, lakini Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote hayo yaliyotendeka.
56Ja tütarlapse vanemad olid jahmunud; aga Jeesus keelas neid kellelegi seda rääkimast, mis oli sündinud.