Swahili: New Testament

Estonian

Mark

3

1Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
1Ja Jeesus läks taas sünagoogi. Ja seal oli inimene, kellel oli kuivanud käsi.
2Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
2Ja Jeesust varitseti, kas ta peaks tervendama hingamispäeval, et saaks tema peale kaevata.
3Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, "Njoo hapa katikati."
3Ja tema ütles inimesele, kellel oli kuivanud käsi: 'Tõuse meie keskele püsti!'
4Kisha, akawauliza, "Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?" Lakini wao hawakusema neno.
4Ja ta ütles neile: 'Kas hingamispäeval tohib teha head või halba, hinge päästa või tappa?' Aga nemad jäid vait.
5Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, "Nyosha mkono wako!" Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
5Ja vaadates neid vihaga ja tundes meelehärmi nende südamekanguse pärast, ütles Jeesus inimesele: 'Siruta käsi!' Ja too sirutas, ja ta käsi sai jälle terveks.
6Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
6Ja variserid läksid kohe välja ning langetasid koos Heroodese meestega Jeesuse kohta otsuse, et ta tuleb hukata.
7Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
7Ja Jeesus läks koos oma jüngritega eemale järve poole. Ja talle järgnes suur rahvahulk Galileast ja Juudamaalt
8Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
8ja Jeruusalemmast ja Idumeast ja sealtpoolt Jordanit ja Tüürose ja Siidoni ümbrusest - suur rahvahulk tuli ta juurde, kui saadi kuulda, mida kõike Jeesus teeb.
9Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
9Ja ta ütles oma jüngritele, et talle hoitaks väike paat valmis rahvahulga pärast, et see tema peale ei tungiks,
10Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
10sest ta tegi terveks paljusid, nii et tema peale rõhusid kõik need, keda vaevas mingi häda, püüdes teda puudutada.
11Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, "Wewe ni Mwana wa Mungu!"
11Ja rüvedad vaimud, kui nad nägid Jeesust, langesid ta ette maha ja kisendasid: 'Sina oled Jumala Poeg!'
12Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
12Ja ta hoiatas neid kõvasti, et nad ei teeks teda tuntuks.
13Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
13Ja Jeesus läks üles mägedesse ja kutsus enese juurde, keda ta ise tahtis, ja need tulid tema juurde.
14naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
14Ja ta seadis kaksteist, keda ta ka nimetas apostliteks, et need oleksid temaga ja et ta võiks nad läkitada kuulutama
15na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
15ja et neil oleks meelevald kurje vaime välja ajada.
16Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
16Ja ta seadis need kaksteist: Siimona, ja pani talle nimeks Peetrus,
17Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake "wanangurumo"),
17ja Jaakobuse, Sebedeuse poja, ning Jaakobuse venna Johannese, ja pani neile nimeks Boanerges, see on Kõuepojad,
18Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
18ja Andrease ja Filippuse ja Bartolomeuse ja Matteuse ja Tooma ja Jaakobuse, Alfeuse poja, ja Taddeuse ja Siimon Kananaiose
19Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
19ja Juudas Iskarioti, kes tema ära andis.
20Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
20Ja Jeesus tuli koju ja taas kogunes rahvahulk, nii et nad ei saanud leibagi süüa.
21Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
21Ja seda kuuldes tulid ta omaksed teda kinni võtma, sest räägiti, et ta on arust ära.
22Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, "Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo."
22Ent kirjatundjad, kes olid tulnud Jeruusalemmast, ütlesid: 'Temas on Peltsebul!' ja 'Ta ajab kurje vaime välja kurjade vaimude ülema abil!'
23Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, "Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
23Ja Jeesus kutsus nad enese juurde ja rääkis neile mõistu: 'Kuidas saab saatan ajada välja saatanat?
24Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
24Ja kui kuningriik on omavahelises riius lõhenenud, siis ei saa see kuningriik püsida.
25Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
25Ja kui pere on omavahelises riius lõhenenud, siis ei saa see pere püsida.
26Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
26Ja kui saatan tõuseb iseenese vastu ja on lõhenenud, siis ei saa ta püsida, vaid tal on lõpp käes.
27"Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
27Ometi, keegi ei saa minna vägimehe majja ta asju röövima, kui ta esmalt ei köida vägimeest kinni, ja alles siis saab ta tema maja röövida.
28"Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
28Tõesti, ma ütlen teile, inimlastele antakse andeks kõik patud ja pühaduseteotused, kuidas nad iganes ka oleksid teotanud,
29lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele."
29kes aga peaks teotama Püha Vaimu, sellele ei ole andeksandmist iialgi, vaid ta on süüdi igaveses patus!'
30(Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, "Ana pepo mchafu.")
30Nad ju ütlesid: 'Tal on rüve vaim!'
31Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
31Siis tulid Jeesuse ema ja ta vennad, ja väljas seistes lasksid nad teda kutsuda.
32Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, "Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona."
32Ja rahvahulk istus Jeesuse ümber, kui talle öeldi: 'Vaata, su ema ja su vennad ja su õed otsivad sind väljas.'
33Yesu akawaambia, "Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?"
33Ent Jeesus vastas neile: 'Kes on mu ema ja vennad?'
34Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, "Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
34Ja silmitsedes neid, kes istusid ringis ta ümber, ütles ta: 'Ennäe, mu ema ja mu vennad!
35Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu."
35Sest kes iganes teeb Jumala tahtmist, see on mu vend ja õde ja ema.'