Swahili: New Testament

Estonian

Mark

2

1Baada ya siku kadhaa, Yesu alirudi Kafarnaumu, watu wakapata habari kwamba alikuwa nyumbani.
1Ja kui Jeesus tuli mõni päev hiljem taas Kapernauma, saadi kuulda, et ta on kodus.
2Basi, wakaja watu wengi sana hata nafasi yoyote ikakosekana mlangoni. Yesu alikuwa akiwahubiria ujumbe wake,
2Ja paljud tulid kokku, nii et isegi ukse ees ei olnud enam ruumi. Ja Jeesus kõneles neile Jumala sõna.
3wakati mtu mmoja aliyepooza alipoletwa kwake akiwa amechukuliwa na watu wanne.
3Ja neli meest tuli tema juurde, kandes halvatut.
4Kwa sababu ya huo umati wa watu, hawakuweza kumpeleka karibu na Yesu. Basi, wakatoboa sehemu ya dari iliyokuwa juu ya mahali alipokuwa Yesu. Walipokwisha pata nafasi, wakamteremsha huyo mtu akiwa amelala juu ya mkeka.
4Ja kui nad rahvahulga tõttu ei saanud teda tuua Jeesuse lähedale, võtsid nad katuse sealt kohalt lahti, kus ta oli, ja teinud augu, lasksid alla kanderaami, millel halvatu lamas.
5Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Mwanangu, umesamehewa dhambi zako."
5Ja nende usku nähes ütles Jeesus halvatule: 'Poeg, sinu patud on sulle andeks antud!'
6Baadhi ya walimu wa Sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao,
6Aga seal olid mõned kirjatundjad istumas, kes mõtlesid oma südames:
7"Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake."
7'Mida see räägib nõnda? Ta teotab Jumalat! Kes muu võib patte andeks anda kui Jumal üksi?'
8Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
8Aga Jeesus tundis kohe oma vaimus ära, et nood nõnda mõtlevad iseeneses, ja ta ütles neile: 'Miks te seda kõike arutate oma südames?
9Ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia mtu huyu aliyepooza, Umesamehewa dhambi zako, au kumwambia, Inuka! Chukua mkeka wako utembee?
9Kumb on kergem, kas öelda halvatule: 'Sinu patud on andeks antud!' või öelda talle: 'Tõuse püsti, võta oma kanderaam ja kõnni!'?
10Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza,
10Aga et te teaksite, et Inimese Pojal on meelevald patte andeks anda maa peal,' - ta ütles halvatule -
11"Nakwambia simama, chukua mkeka wako uende nyumbani!"
11'sinule ma ütlen: Tõuse püsti, võta oma kanderaam ja mine koju!'
12Mara, watu wote wakiwa wanamtazama, huyo mtu akainuka, akauchukua mkeka wake, akaenda zake. Watu wote wakashangaa na kumtukuza Mungu wakisema, "Hatujapata kamwe kuona jambo kama hili."
12Ja kohe tõusis too püsti, võttis oma kanderaami ja läks välja kõigi silma all, nii et kõik hämmastusid ja ülistasid Jumalat, öeldes: 'Sellist asja pole me eluilmaski näinud!'
13Yesu alikwenda tena kando ya ziwa. Umati wa watu ukamwendea, naye akaanza kuwafundisha.
13Ja Jeesus läks taas välja järve äärde ja ta juurde tuli suur hulk rahvast ja ta õpetas neid.
14Alipokuwa akipita, akamwona Lawi mwana wa Alfayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Yesu akamwambia, "Nifuate!" Lawi akasimama, akamfuata.
14Ja edasi minnes nägi Jeesus Leevit, Alfeuse poega, tollihoone juures istuvat ja ütles talle: 'Järgne mulle!' Ja too tõusis ja järgnes talle.
15Baadaye, Yesu alikuwa amekaa mezani, nyumbani kwa Lawi, kula chakula. Watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuwa wamemfuata Yesu na wengi wao wakawa wamekaa mezani pamoja naye na wanafunzi wake.
15Ja sündis, et Jeesus istus lauas tema kodus ning palju tölnereid ja muid patuseid istus koos Jeesuse ja tema jüngritega. Sest neid oli palju, kes temaga kaasas käisid.
16Basi, baadhi ya walimu wa Sheria ambao walikuwa Mafarisayo walipomwona Yesu akila pamoja na watu wenye dhambi na watoza ushuru, wakawauliza wanafunzi wake, "Kwa nini anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
16Ja kui variseride kirjatundjad nägid, et Jeesus sööb koos patuste ja tölneritega, ütlesid nad tema jüngritele: 'Mis, kas ta sööb koos tölnerite ja patustega!'
17Yesu alipowasikia, akawaambia, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi."
17Seda kuuldes ütles Jeesus neile: 'Ei vaja arsti terved, vaid haiged. Ma ei ole tulnud kutsuma õigeid, vaid patuseid.'
18Wakati mmoja wanafunzi wa Yohane na wanafunzi wa Mafarisayo walikuwa wanafunga. Basi, watu wakaja, wakamwuliza Yesu, "Kwa nini wanafunzi wa Yohane na wa Mafarisayo wanafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?"
18Johannese jüngritel ja variseridel oli tavaks paastuda. Nüüd tuldi ja öeldi Jeesusele: 'Miks Johannese jüngrid ja variseride jüngrid paastuvad, aga sinu jüngrid ei paastu?'
19Yesu akajibu, "Walioalikwa harusini wanawezaje kufunga kama bwana harusi yupo pamoja nao? Wakati wote wawapo pamoja na bwana harusi hawawezi kufunga.
19Ja Jeesus ütles neile: 'Ega peiupoisid või paastuda sel ajal, kui peigmees on nende juures!? Niikaua kui peigmees on nende juures, nad ei või paastuda.
20Lakini wakati utafika ambapo bwana harusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
20Ent päevad tulevad, mil peigmees neilt ära võetakse, küll nad siis paastuvad tol päeval.
21"Hakuna mtu anayekata kiraka kutoka katika nguo mpya na kukishonea katika nguo kuukuu. Kama akifanya hivyo, hicho kiraka kipya kitararuka kutoka hilo vazi kuukuu, nalo litaharibika zaidi.
21Keegi ei paika vanutamata riidetükiga vana kuube, muidu paik rebeneb selle küljest, uus vanast, ja auk läheb veel suuremaks.
22Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai itavipasua hivyo viriba, nayo divai pamoja na hivyo viriba vitaharibika. Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!"
22Ja keegi ei kalla värsket veini vanadesse nahklähkritesse, muidu vein rebestab lähkrid ning vein ja lähkrid muutuvad kõlbmatuks, vaid värske vein kallatakse uutesse lähkritesse.'
23Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano. Walipokuwa wanatembea, wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano.
23Ja ühel hingamispäeval juhtus Jeesus minema läbi viljapõldude ning tema jüngrid hakkasid teed käies viljapäid katkuma.
24Mafarisayo wakawaambia, "Tazama! Kwa nini wanafanya jambo ambalo si halali kufanya wakati wa Sabato?"
24Ja variserid ütlesid talle: 'Vaata, nad teevad hingamispäeval, mida ei tohi!'
25Yesu akawajibu, "Je, hamjapata kusoma juu ya kile alichofanya Daudi wakati alipohitaji chakula? Yeye pamoja na wenzake waliona njaa,
25Ja tema ütles neile: 'Kas te pole kunagi lugenud, mida tegi Taavet, kui tal oli puudus ning tema ja ta mehed olid näljas?
26naye akaingia ndani ya Nyumba ya Mungu, akala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Jambo hili lilifanyika wakati Abiathari alikuwa Kuhani Mkuu. Na ni makuhani tu peke yao waliokuwa wameruhusiwa kula mikate hiyo. Lakini Daudi aliila, tena akawapa na wenzake."
26Kuidas ta läks Jumala kotta ülempreester Ebjatari ajal ning sõi ära ohvrileivad, ehkki neid ei tohi süüa keegi peale preestrite, ja andis ka oma meestele?'
27Basi, Yesu akawaambia, "Sabato iliwekwa kwa ajili ya binadamu na si binadamu kwa ajili ya Sabato!
27Ja ta ütles neile: 'Hingamispäev on seatud inimese jaoks, mitte inimene hingamispäeva jaoks;
28Kwa hiyo, Mwana wa Mtu ni Bwana hata wa Sabato."
28nõnda on Inimese Poeg ka hingamispäeva isand.'