1Wakati huo, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano siku ya Sabato. Basi, wanafunzi wake wakaona njaa, wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakala punje zake.
1Tolsamal ajal läks Jeesus hingamispäeval läbi viljapõldude. Tema jüngrid tundsid aga nälga ja hakkasid katkuma viljapäid ning sööma.
2Mafarisayo walipoona hayo, wakamwambia Yesu, "Tazama, wanafunzi wako wanafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato."
2Aga seda nähes ütlesid variserid talle: 'Vaata, sinu jüngrid teevad, mida ei tohi teha hingamispäeval!'
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
3Tema aga ütles neile: 'Kas te ei ole lugenud, mida tegi Taavet, kui tema ja ta mehed olid näljas?
4Yeye aliingia katika Nyumba ya Mungu pamoja na wenzake, wakala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Yeye wala hao wenzake hawakuruhusiwa kula mikate hiyo isipokuwa tu makuhani peke yao.
4Kuidas ta läks Jumala kotta ja nad sõid ära ohvrileivad, mida ei tohtinud süüa ei tema ega ta mehed, vaid ainult preestrid üksi?
5Au je, hamjasoma katika Sheria kwamba kila siku ya Sabato makuhani huivunja Sheria Hekaluni, lakini hawafikiriwi kuwa na hatia?
5Või kas te ei ole lugenud Seadusest, et preestrid rikuvad pühakojas hingamispäeva ja on siiski ilma süüta?
6Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko Hekalu.
6Ent mina ütlen teile, siin on see, kes on suurem kui pühakoda!
7Kama tu mngejua maana ya maneno haya: Nataka huruma wala si dhabihu, hamngewahukumu watu wasio na hatia.
7Kui te oleksite mõistnud, mida tähendab: Ma ei taha ohvrit, vaid halastust, siis te ei oleks mõistnud hukka süütuid,
8Maana Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
8sest Inimese Poeg on hingamispäeva isand.'
9Yesu alitoka hapo, akaenda katika sunagogi lao.
9Ja Jeesus läks sealt edasi ning tuli ühte nende sünagoogi.
10Kulikuwa na mtu mmoja mwenye mkono uliopooza. Basi, watu wakamwuliza Yesu, "Je, ni halali kumponya mtu siku ya Sabato?" Walimwuliza hivyo wapate kisa cha kumshtaki.
10Ja vaata, seal oli kuivanud käega inimene. Ja nad küsisid temalt: 'Kas hingamispäeval tohib teha terveks?' - et nad võiksid tema peale kaevata.
11Lakini Yesu akawaambia, "Tuseme mmoja wenu ana kondoo wake ambaye ametumbukia shimoni; je, hatamshika na kumtoa humo siku ya Sabato?
11Aga tema ütles neile: 'Kes on teie seast inimene, kellel on üksainus lammas ja kui see kukub auku hingamispäeval, et ta ei haara temast kinni ega tõmba teda välja?
12Mtu ana thamani kuliko kondoo! Basi, ni halali kutenda mema siku ya Sabato."
12Kui palju tähtsam lambast on nüüd inimene! Tähendab, hingamispäeval tohib teha head.'
13Kisha akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Akaunyosha, nao ukawa mzima kabisa kama ule mwingine.
13Siis ta ütles inimesele: 'Siruta oma käsi!' Ja too sirutas ning ta käsi sai jälle terveks nagu teinegi.
14Basi, Mafarisayo wakatoka nje, wakashauriana jinsi watakavyomwangamiza Yesu.
14Aga variserid läksid välja ning võtsid Jeesuse kohta vastu otsuse, et ta tuleb hukata.
15Lakini Yesu alipojua jambo hilo, akatoka mahali pale. Watu wengi walimfuata, akawaponya wagonjwa wote,
15Aga kui Jeesus sai seda teada, eemaldus ta sealt. Ja paljud läksid temaga kaasa, ja tema tegi nad kõik terveks.
16akawaamuru wasiwaambie watu habari zake,
16Ja ta hoiatas neid, et nad ei teeks teda tuntuks,
17ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie:
17et läheks täide, mida on räägitud prohvet Jesaja kaudu:
18"Hapa ni mtumishi wangu niliyemteua, mpendwa wangu anipendezaye moyoni. Nitaiweka Roho yangu juu yake, naye atatangaza hukumu yangu kwa mataifa yote.
18'Vaata, see on mu sulane, kelle ma olen valinud, mu armastatu, kellest mu hingel on hea meel. Ma panen oma Vaimu tema peale ja ta kuulutab paganaile õigust.
19Hatakuwa na ubishi wala kupiga kelele, wala sauti yake haitasikika barabarani.
19Ta ei riidle ega kisenda ega kuule tänavail keegi ta häält,
20Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi ufukao moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya hukumu ya haki itawale.
20rudjutud roogu ei murra ta katki ja hõõguvat tahti ei kustuta ta ära, kuni ta on õigusele võidu saatnud,
21Katika jina lake mataifa yatakuwa na tumaini."
21ja paganad loodavad tema nime peale.'
22Hapo watu wakamletea Yesu kipofu mmoja ambaye alikuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo. Yesu akamponya hata, akaweza kusema na kuona.
22Siis toodi Jeesuse juurde kurjast vaimust vaevatu, kes oli pime ja tumm, ning Jeesus tegi ta terveks, nii et tumm rääkis ja nägi.
23Umati wote wa watu ulishangaa ukasema, "Je, huenda ikawa huyu ndiye Mwana wa Daudi?"
23Ja kõik rahvahulgad hämmastusid ning ütlesid: 'Egas see ometi ole Taaveti Poeg?'
24Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, wakasema, "Mtu huyu anawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo."
24Aga variserid ütlesid sellest kuulda saades: 'See ei aja kurje vaime välja kellegi muu kui Peltsebuli, kurjade vaimude ülema abil.'
25Yesu, akiwa anayajua mawazo yao, akawaambia, "Ufalme wowote uliogawanyika makundimakundi yanayopingana, hauwezi kudumu, na mji wowote au jamaa yoyote iliyogawanyika makundimakundi yanayopingana, itaanguka.
25Ent Jeesus, teades nende mõtteid, ütles neile: 'Iga kuningriik, mis on omavahelises riius lõhenenud, laastatakse, ja ükski linn või pere, mis on omavahel riius, ei jää püsima.
26Ikiwa Shetani anamfukuza Shetani, anajipinga mwenyewe. Basi, ufalme wake utasimamaje?
26Ja kui saatan ajab välja saatana, siis on ta iseenesega riius. Kuidas võib tema kuningriik siis püsida?
27Ninyi mnasema ati nawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli; je, watoto wenu huwafukuza kwa uwezo wa nani? Kwa sababu hiyo wao ndio watakaowahukumu ninyi.
27Ja kui mina peaksin kurje vaime välja ajama Peltsebuli abiga, kelle abiga siis teie pojad ajavad neid välja? Järelikult saavad nendest teile kohtumõistjad.
28Lakini ikiwa ninawafukuza pepo kwa nguvu ya Roho wa Mungu, basi jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekwisha fika kwenu.
28Aga kui mina Jumala Vaimu abil ajan kurje vaime välja, küllap siis on Jumala riik jõudnud teie juurde.
29"Au, anawezaje mtu kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, bila kwanza kumfunga huyo mtu mwenye nguvu? Hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
29Või kuidas saab keegi minna vägimehe majja ja röövida tema asju, kui ta esmalt ei köida vägimeest kinni? Alles siis saab ta tema maja röövida.
30"Yeyote asiyejiunga nami, anapingana nami; na yeyote asiyekusanya pamoja nami, hutawanya.
30Kes ei ole minuga, see on minu vastu, ja kes ei kogu minuga, see pillab laiali.
31Kwa sababu hiyo, nawaambieni, watu watasamehewa dhambi na kufuru zao zote, lakini hawatasamehewa dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu.
31Seepärast ma ütlen teile: Inimestele antakse andeks iga patt ja teotamine, aga Vaimu teotamist ei anta andeks.
32Tena, asemaye neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa, lakini yule asemaye neno la kumpinga Roho Mtakatifu, hatasamehewa, wala katika ulimwengu huu, wala katika ulimwengu ujao.
32Ja kui keegi ütleb midagi Inimese Poja vastu, võib ta saada andeks, aga kui keegi ütleb midagi Püha Vaimu vastu, ei andestata talle ei sellel ega tulevasel ajastul.
33"Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake yatakuwa mema; ufanyeni kuwa mbaya na matunda yake yatakuwa mabaya. Mti hujulikana kwa matunda yake.
33Kui puu on hea, siis on ta viligi hea, või kui puu on halb, siis on ta viligi halb; sest puud tuntakse tema viljast.
34Enyi kizazi cha nyoka! Mnawezaje kusema mambo mema hali ninyi ni waovu? Maana mtu husema kutokana na yale yaliyojaa moyoni.
34Teie rästikute sugu, kuidas te võiksitegi rääkida head, kui te olete kurjad? Sest suu räägib sellest, millest süda on tulvil.
35Mtu mwema hutoa mambo mema katika hazina yake njema; na mtu mbaya hutoa mambo mabaya katika hazina yake mbaya.
35Hea inimene võtab heast varamust head ja kuri inimene võtab kurjast varamust kurja.
36"Basi, nawaambieni, Siku ya hukumu watu watapaswa kujibu juu ya kila neno lisilofaa wanalosema.
36Aga ma ütlen teile, et inimesed peavad kohtupäeval aru andma igast tühjast sõnast, mis nad on rääkinud,
37Maana kwa maneno yako, utakubaliwa kuwa mwadilifu, na kwa maneno yako, utahukumiwa kuwa na hatia."
37sest su sõnadest mõistetakse sind õigeks ja su sõnadest mõistetakse sind süüdi.'
38Kisha baadhi ya walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamwambia Yesu, "Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako."
38Siis mõned kirjatundjad ja variserid vastasid talle: 'Õpetaja, me tahame sinult näha tunnustähte!'
39Naye akawajibu, "Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara; hamtapewa ishara nyingine, ila tu ile ishara ya nabii Yona.
39Aga tema ütles neile: 'See kuri ja abielurikkuja sugupõlv nõuab tunnustähte, ent talle ei anta muud kui prohvet Joona tunnustäht,
40Jinsi Yona alivyokaa siku tatu kutwa kucha tumboni mwa nyangumi, ndivyo naye Mwana wa Mtu atakavyokaa ndani ya ardhi siku tatu kutwa kucha.
40sest nii nagu Joona oli merekoletise kõhus kolm päeva ja kolm ööd, nõnda peab ka Inimese Poeg olema maapõues kolm päeva ja kolm ööd.
41Watu wa Ninewi watatokea siku ya hukumu, nao watakihukumu kizazi hiki kwamba kina hatia. Maana Waninewi walitubu kwa sababu ya mahubiri ya Yona, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Yona!
41Niineve mehed tõusevad kohtupäeval üles koos selle sugupõlvega ja mõistavad selle sugupõlve süüdi, sest nemad parandasid meelt Joona jutluse peale, ja vaata, siin on rohkem kui Joona!
42Malkia wa kusini atatokea wakati kizazi hiki kitakapohukumiwa, naye atakihukumu kwamba kina hatia. Maana yeye alisafiri kutoka mbali akaja kusikiliza maneno ya hekima ya Solomoni, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Solomoni.
42Lõunamaa kuninganna tõuseb kohtupäeval üles koos selle sugupõlvega ja mõistab ta süüdi, sest tema tuli ilmamaa otsast kuulama Saalomoni tarkust, ja vaata, siin on rohkem kui Saalomon!
43"Pepo mchafu akifukuzwa kwa mtu, huzururazurura jangwani akitafuta mahali pa kupumzika asipate.
43Kui rüve vaim on inimesest välja läinud, käib ta põuaseid paiku pidi hingamist otsides ega leia seda.
44Hapo hujisemea: Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka. Lakini anaporudi na kuikuta tupu, imefagiwa na kupambwa,
44Siis ta ütleb: 'Ma pöördun tagasi oma majja, kust ma välja tulin.' Ja tulles leiab ta selle tühja olevat ning puhtaks pühitud ja ehitud.
45huenda kuwachukua pepo wengine saba, wabaya kuliko yeye; na wote huja wakamwingia huyo mtu. Na hali ya mtu huyo sasa huwa mbaya kuliko hapo mwanzo. Ndivyo itakavyokuwa kwa watu hawa waovu."
45Siis ta läheb ja võtab enesega kaasa teist seitse vaimu, kes on kurjemad temast endast, ja nad tulevad ning asuvad sinna elama, ja selle inimese viimne lugu läheb pahemaks kui esimene. Nõnda sünnib ka sellele kurjale sugupõlvele!'
46Yesu alikuwa bado anasema na umati wa watu wakati mama yake na ndugu zake walipofika na kusimama nje, wakitaka kusema naye.
46Kui Jeesus alles rääkis rahvahulkadele, vaata, siis seisid tema ema ja vennad väljas, otsides võimalust temaga rääkida.
47Basi, mtu mmoja akamwambia, "Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kusema nawe."
47[Aga keegi ütles talle: 'Vaata, su ema ja su vennad seisavad väljas ja tahavad sinuga rääkida!']
48Lakini Yesu akamjibu mtu huyo, "Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni kina nani?"
48Tema aga kostis teate toojale: 'Kes on mu ema ja kes on mu vennad?'
49Kisha akaunyosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema, "Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu!
49Ja sirutades käed jüngrite poole ütles ta: 'Ennäe, mu ema ja mu vennad!
50Maana yeyote anayefanya anavyotaka Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu."
50Sest kes iganes teeb mu Isa tahtmist, kes on taevas, see on mu vend ja õde ja ema.'