1Siku hiyohiyo, Yesu alitoka katika ile nyumba, akaenda na kuketi kando ya ziwa.
1Sel päeval läks Jeesus kodunt välja ja istus järve äärde.
2Makundi makubwa ya watu yalimzunguka hata Yesu akapanda mashua, akaketi. Hao watu walisimama kwenye ukingo wa ziwa,
2Ja tema juurde kogunes suur rahvahulk, nii et ta pidi astuma paati ning sinna istuma. Kõik rahvas seisis kaldal
3naye Yesu akawaambia mambo mengi kwa mifano. "Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
3ja tema rääkis neile palju asju tähendamissõnadega. Ta ütles:'Vaata, külvaja läks välja külvama.
4Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
4Ja külvamisel pudenes osa seemet tee äärde ning linnud tulid ja nokkisid selle.
5Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
5Aga osa kukkus kivisele maale, kus sel polnud palju mulda, ja see tärkas kohe, sest sel polnud sügavat mulda.
6Jua lilipochomoza, zilichomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
6Ent päikese tõustes see närtsis ja kuivas ära, sest sel polnud juurt.
7Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga.
7Osa seemet kukkus ohakate sekka ning ohakad sirgusid ja lämmatasid selle.
8Lakini nyingine zilianguka penye udongo mzuri, zikaota, zikazaa: nyingine punje mia moja, nyingine sitini na nyingine thelathini.
8Aga osa kukkus heasse mulda ning kandis vilja, mõni sada, mõni kuuskümmend, mõni kolmkümmend seemet.
9Mwenye masikio na asikie!"
9Kel kõrvad on, kuulgu!'
10Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwuliza, "Kwa nini unasema na watu kwa mifano?"
10Jüngrid astusid Jeesuse juurde ning küsisid temalt: 'Miks sa räägid neile tähendamissõnadega?'
11Yesu akawajibu, "Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za Ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakujaliwa.
11Ja Jeesus kostis: 'Teile on antud mõista taevariigi saladusi, neile aga ei ole,
12Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa; lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
12sest kellel on, sellele antakse, ja tal on rohkem kui küllalt, aga kellel ei ole, sellelt võetakse ära seegi, mis tal on.
13Ndiyo maana ninasema nao kwa mifano, kwa sababu wanatazama lakini hawaoni, wanasikiliza lakini hawasikii, wala hawaelewi.
13Ma räägin neile tähendamissõnadega sellepärast, et nad vaadates ei näe ja kuuldes ei kuule ega mõista.
14Kwao yametimia yale aliyosema nabii Isaya: Kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; Kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
14Ja nende kohta läheb täide Jesaja ennustus, mis ütleb: 'Kuuldes te kuulete ega mõista, vaadates vaatate ega näe.
15Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameyaziba masikio yao, wameyafumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao. wangesikia kwa masikio yao, wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya.
15Sest selle rahva süda on kalestunud ja nad kuulevad kõrvadega raskesti ja sulevad oma silmad, et nad silmadega ei näeks ja kõrvadega ei kuuleks, et nad südamega ei mõistaks ega pöörduks, et ma võiksin neid parandada.'
16"Lakini heri yenu ninyi, maana macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia.
16Õndsad on aga teie silmad, et need näevad, ja teie kõrvad, et need kuulevad.
17Kweli nawaambieni, manabii na watu wengi wema walitamani kuyaona yale mnayoyaona, wasiyaone, na kuyasikia yale mnayoyasikia, wasiyasikie.
17Sest tõesti, ma ütlen teile, palju prohveteid ja õigeid on ihaldanud näha, mida teie näete, ega ole näinud, ja kuulda, mida teie kuulete, ega ole kuulnud.
18"Basi, ninyi sikilizeni maana ya mfano huo wa mpanzi.
18Kuulge nüüd külvaja tähendamissõna tähendust.
19Yeyote asikiaye ujumbe wa ufalme bila kuuelewa, ni kama zile mbegu zilizoanguka njiani; yule Mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake.
19Igaühe juurde, kes sõna Kuningriigist kuuleb, ent ei mõista, tuleb kuri ning riisub külvatu ta südamest. See on tee äärde külvatu.
20Ile mbegu iliyopandwa penye mawe ni mfano wa mtu asikiaye ujumbe huo na mara akaupokea kwa furaha.
20Mis kivisele maale külvati, on see, kes sõna kuuleb ja selle kohe rõõmuga vastu võtab,
21Lakini haumwingii na kuwa na mizizi ndani yake; huendelea kuuzingatia ujumbe huo kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya ujumbe huo, anakata tamaa mara.
21aga tal enesel pole juurt, vaid ta on heitlik - kui teda sõna pärast hakatakse rõhuma või taga kiusama, laseb ta end kohe eksitada.
22Ile mbegu iliyoanguka kati ya miti ya miiba, ni mfano wa mtu asikiaye huo ujumbe, lakini wasiwasi wa ulimwengu huu na anasa za mali huusonga ujumbe huo, naye hazai matunda.
22Ohakate sekka külvatu on see, kes sõna küll kuuleb, ent selle ajastu muretsemised ja rikkuse petlik ahvatlus lämmatavad sõna ning see jääb viljatuks.
23Ile mbegu iliyopandwa katika udongo mzuri ni mfano wa mtu ausikiaye ujumbe huo na kuuelewa, naye huzaa matunda; mmoja mia, mwingine sitini na mwingine thelathini."
23Heasse mulda külvatu on aga see, kes sõna kuuleb ja mõistab ning siis ka vilja kannab: mõni saja-, mõni kuuekümne-, mõni aga kolmekümnekordselt.'
24Yesu akawaambia watu mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
24Jeesus kõneles neile veel teise tähendamissõna: 'Taevariik on inimese sarnane, kes külvas oma põllule head seemet.
25Lakini watu wakiwa wamelala, adui yake akaja akapanda magugu kati ya ngano, akaenda zake.
25Aga inimeste magades tuli ta vaenlane ja külvas raiheina nisu sekka ning läks minema.
26Basi, mimea ilipoota na kuanza kuchanua, magugu pia yakaanza kuonekana.
26Kui nüüd oras tärkas ja looma hakkas, tuli ka raihein nähtavale.
27Watumishi wa yule mwenye shamba wakamwendea, wakamwambia, Mheshimiwa, bila shaka ulipanda mbegu nzuri katika shamba lako. Sasa magugu yametoka wapi?
27Peremehe sulased astusid ta juurde ja ütlesid talle: 'Isand, eks sa külvanud head seemet oma põllule, kust nüüd tuleb sinna raihein?'
28Yeye akawajibu, Adui ndiye aliyefanya hivyo. Basi, watumishi wake wakamwuliza, Je, unataka twende tukayang'oe
28Tema lausus neile: 'See on vihamehe töö.' Siis küsisid sulased temalt: 'Kas sa tahad, et me läheme ning selle kokku korjame?'
29Naye akawajibu, La, msije labda mnapokusanya magugu, mkang'oa na ngano pia.
29Ei, vastas tema, sest muidu te kisuksite raiheina korjates üles ka nisu.
30Acheni vikue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji: kusanyeni kwanza magugu mkayafunge mafungumafungu ya kuchomwa. Lakini ngano ikusanyeni mkaiweke ghalani mwangu."
30Laske mõlemaid ühtmoodi kasvada lõikuseni ja lõikuse ajal ma ütlen lõikajaile: 'Koguge esmalt raihein ja siduge kimpu põletamiseks, nisu aga pange kokku mu aita!''
31Yesu akawaambia watu mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja, akaipanda katika shamba lake.
31Jeesus kõneles neile veel teise tähendamissõna: 'Taevariik on sinepiivakese sarnane, mille inimene võttis ja külvas oma põllule.
32Yenyewe ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini ikishaota huwa kubwa kuliko mimea yote. Hukua ikawa mti, na ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake."
32See on küll väiksem kõigist seemneist, ent kui taim kasvab, siis on see suurim aias ja saab puuks, nii et taeva linnud tulevad ja pesitsevad selle okstel.'
33Yesu akawaambia mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyotwaa mama mmoja, akaichanganya na unga pishi tatu, hata unga wote ukaumuka."
33Ta rääkis neile veel ühe tähendamissõna: 'Taevariik on haputaigna sarnane, mille naine võttis ja segas kolme vaka jahu sekka, kuni kõik läks hapnema.'
34Yesu aliwaambia watu hayo yote kwa mifano. Hakuwaambia chochote bila kutumia mifano,
34Seda kõike rääkis Jeesus rahvahulkadele tähendamissõnades ja ilma tähendamissõnata ei rääkinud ta neile midagi,
35ili jambo lililonenwa na nabii litimie: "Nitasema kwa mifano; nitawaambia mambo yaliyofichika tangu kuumbwa ulimwengu."
35et läheks täide, mis on üteldud prohveti kaudu: 'Ma avan oma suu tähendamissõnadeks, kuulutan, mis on olnud peidus maailma rajamisest peale.'
36Kisha Yesu aliwaaga wale watu, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, "Tufafanulie ule mfano wa magugu shambani."
36Siis laskis Jeesus rahvahulgad ära minna ja tuli koju. Ja ta jüngrid astusid ta juurde ning ütlesid: 'Seleta meile tähendamissõna raiheinast!'
37Yesu akawaambia, "Mpanzi wa zile mbegu nzuri ni Mwana wa Mtu.
37Ja tema kostis: 'Hea seemne külvaja on Inimese Poeg.
38Lile shamba ni ulimwengu. Zile mbegu nzuri ni watu wale ambao Ufalme ni wao. Lakini yale magugu ni wale watu wa yule Mwovu.
38Põld on maailm, hea seeme Kuningriigi pojad, raiheinad aga kurja pojad.
39Adui aliyepanda yale magugu ni Ibilisi. Mavuno ni mwisho wa nyakati na wavunaji ni malaika.
39Ent vihamees, kes neid külvab, on kurat. Lõikus on ajastu lõpp, lõikajad on inglid.
40Kama vile magugu yanavyokusanywa kuchomwa moto, ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati;
40Nii nagu nüüd raiheinad korjatakse ja tulega ära põletatakse, nõnda on ka selle ajastu lõpul.
41Mwana wa Mtu atawatuma malaika wake wawakusanye kutoka katika Ufalme wake wale wote wenye kusababisha dhambi, na wote wenye kutenda maovu,
41Inimese Poeg läkitab oma inglid ja need korjavad tema Kuningriigist kõik pahanduse- ja ülekohtutegijad
42na kuwatupa katika tanuru ya moto, na huko watalia na kusaga meno.
42ja viskavad nad tuleahju: seal on ulgumine ja hammaste kiristamine.
43Kisha, wale wema watang'ara kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Sikieni basi, kama mna masikio!
43Siis säravad õiged nagu päike oma Isa Kuningriigis. Kel kõrvad on, kuulgu!
44"Ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyofichika shambani. Mtu mmoja aliigundua, akaificha tena. Alifurahi sana hata akaenda kuuza yote aliyokuwa nayo, akalinunua shamba lile.
44Taevariik on põllusse peidetud aarde sarnane, mille inimene leidis ja peitis jälle. Ta läks rõõmuga ja müüs ära kõik, mis tal oli, ning ostis selle põllu.
45"Tena, Ufalme wa mbinguni umefanana na mfanyabiashara mmoja mwenye kutafuta lulu nzuri.
45Veel on taevariik kaupmehe sarnane, kes otsis ilusaid pärleid.
46Alipopata lulu moja ya thamani kubwa, alienda akauza yote aliyokuwa nayo, akainunua lulu ile.
46Kui ta siis leidis ühe eriti hinnalise pärli, läks ta ja müüs maha kõik, mis tal oli, ning ostis selle.
47"Tena, Ufalme wa mbinguni unafanana na wavu uliotupwa baharini, ukanasa samaki wa kila aina.
47Veel on taevariik nooda sarnane, mis heideti merre ja mis vedas kokku igasuguseid kalu.
48Ulipojaa, watu waliuvuta pwani, wakaketi, wakachagua samaki wazuri wakawaweka ndani ya vikapu vyao, na wabaya wakawatupa.
48Kui noot sai täis, veeti see rannale, istuti maha ja koguti head kalad korvidesse, halvad aga visati minema.
49Ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati: malaika watatokea, watawatenganisha watu wabaya na watu wema,
49Nõnda on ka selle ajastu lõpul: inglid tulevad ja eraldavad kurjad õigete keskelt
50na kuwatupa hao wabaya katika tanuru ya moto. Huko watalia na kusaga meno."
50ning viskavad nad tuleahju. Seal on ulgumine ja hammaste kiristamine.
51Yesu akawauliza, "Je, mmeelewa mambo haya yote?" Wakamjibu, "Naam."
51Kas te mõistate seda kõike?' Nad vastasid talle: 'Jah.'
52Naye akawaambia, "Hivyo basi, kila mwalimu wa Sheria aliye mwanafunzi wa Ufalme wa mbinguni anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale."
52Siis ta ütles neile: 'Sellepärast on iga kirjatundja, kes on õpetatud taevariigi jaoks, majaperemehe sarnane, kes oma varakambrist võtab välja uut ja vana.'
53Yesu alipomaliza kusema mifano hiyo alitoka mahali hapo,
53Ja sündis, et kui Jeesus oli need tähendamissõnad lõpetanud, lahkus ta sealt
54akaenda kijijini kwake. Huko akawa anawafundisha watu katika sunagogi hata wakashangaa, wakasema, "Huyu amepata wapi hekima hii na maajabu?
54ja tuli oma kodukohta ning õpetas nende sünagoogis, nii et nad hämmastusid ja ütlesid: 'Kust on pärit tema tarkus ja vägevad teod?
55Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
55Eks ta ole see puusepa poeg? Eks tema ema hüüta Maarjaks ja ta vendi Jaakobuseks ja Joosepiks ja Siimonaks ja Juudaks?
56Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?"
56Ja eks ta õed ole kõik meie juures? Kust siis talle see kõik on tulnud?'
57Basi, wakawa na mashaka naye. Lakini Yesu akawaambia, "Nabii hakosi kuheshimiwa, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani mwake!"
57Ja nad põlastasid teda. Aga Jeesus ütles neile: 'Kuskil ei austata prohvetit vähem kui ta oma kodukohas ja oma majas.'
58Kwa hiyo, hakutenda miujiza mingi pale kwa sababu ya kutoamini kwao.
58Ja ta ei teinud seal kuigi palju vägevaid tegusid nende uskmatuse pärast.