1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
1Tol ajal sai nelivürst Heroodes kuulda, mida Jeesusest räägiti.
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
2Ja ta ütles oma meestele: 'See on Ristija Johannes! Tema on üles äratatud surnuist ja seepärast toimivad imeväed tema kaudu.'
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
3Heroodes oli ju Johannese kinni võtnud, aheldanud ja pannud vanglasse Heroodiase, oma venna Filippuse naise pärast,
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
4sest Johannes oli talle öelnud: 'Sa ei tohi teda pidada!'
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
5Ja Heroodes oleks tahtnud Johannese tappa, kuid kartis rahvast, sest Johannest peeti prohvetiks.
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
6Aga kui tuli Heroodese sünnipäev, tantsis Heroodiase tütar nende keskel ja meeldis Heroodesele,
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
7nõnda et ta vandega tõotas talle anda, mida ta iganes soovib.
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
8Tema aga lausus oma ema õhutusel: 'Anna mulle vaagnal Ristija Johannese pea!'
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
9Kuningas kurvastas, kuid vande ja piduliste pärast käskis talle selle anda.
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
10Ja ta saatis vanglasse mehed Johannesel pead otsast lööma.
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
11Ja Johannese pea toodi vaagnal ja anti tüdrukule ning too viis selle oma emale.
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
12Ja Johannese jüngrid tulid, viisid ta surnukeha ära ja matsid maha ning tulid ja teatasid sellest Jeesusele.
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
13Kui Jeesus sai sellest kuulda, eemaldus ta sealt paadiga tühja paika, et olla omaette. Ja kui rahvahulgad sellest kuulsid, järgnesid nad talle jalgsi linnadest.
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
14Ja kui Jeesus astus paadist välja ja nägi suurt rahvahulka, läks ta meel haledaks ning ta tervendas nende haiged.
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
15Õhtu jõudes aga astusid Jeesuse jüngrid ta juurde ja ütlesid: 'Paik on üksildane ja aeg juba hiline, lase nüüd rahvahulgad ära minna, et nad läheksid küladesse endale süüa otsima!'
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
16Aga Jeesus ütles neile: 'Neil ei ole tarvis ära minna. Andke teie neile süüa!'
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
17Nemad aga ütlesid talle: 'Meil ei ole siin rohkem kui vaid viis leiba ja kaks kala.'
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
18Aga tema ütles: 'Tooge need mulle siia!'
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
19Ja Jeesus käskis rahvahulkadel istuda rohule, võttis need viis leiba ja kaks kala, vaatas üles taevasse, õnnistas ja murdis ning andis leivad jüngrite kätte, jüngrid aga andsid need rahvale.
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
20Ja kõik sõid ja said kõhud täis. Ja ülejäänud palakesi korjati kaksteist korvitäit.
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
21Aga sööjaid oli ligi viis tuhat meest, peale selle veel naised ja lapsed.
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
22Ja Jeesus käskis sedamaid oma jüngreid paati astuda ja sõita vastaskaldale tema eele, sellal kui ta laseb rahvahulkadel minna.
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
23Kui ta siis rahvahulgad oli minema lasknud, läks ta üles mäele üksinda palvetama. Ja õhtu jõudes oli ta seal üksinda.
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
24Aga paat oli juba hulga maad kaldast eemaldunud, heitlemas lainetega, sest tuul oli vastu.
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
25Ent neljandal öövahikorral tuli Jeesus nende juurde järve peal kõndides.
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
26Aga Jeesust järve peal kõndimas nähes ütlesid jüngrid kohkunult: 'See on tont!' ja hakkasid hirmu pärast kisendama.
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
27Aga Jeesus kõnetas neid sedamaid: 'Olge julged, see olen mina, ärge kartke!'
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
28Peetrus vastas: 'Issand, kui see oled sina, siis käsi mind tulla enda juurde vee peale!'
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
29Tema ütles: 'Tule!' Ja Peetrus astus paadist välja ning kõndis vee peal ja tuli Jeesuse juurde.
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
30Aga tuult nähes lõi ta kartma ja hüüdis uppuma hakates: 'Issand, päästa mind!'
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
31Jeesus sirutas kohe oma käe, haaras temast kinni ning ütles talle: 'Sa nõdrausuline, miks sa kahtlesid?'
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
32Ja kui nad astusid paati, rauges tuul.
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
33Paadisolijad aga kummardasid teda ja ütlesid: 'Tõesti, sina oled Jumala Poeg!'
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
34Ja kui nad olid sõitnud üle järve, siis nad tulid maale Genneesaretis.
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
35Ja kui selle koha mehed Jeesuse ära tundsid, läkitasid nad sõna kogu ümbruskonda ja tema juurde toodi kõik haiged
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.
36ja need palusid teda, et nad saaksid üksnes puudutada tema kuue palistust, ja kes iganes teda puudutas, sai terveks.