1Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu, mkoani Yudea, wakati Herode alipokuwa mfalme. Punde tu baada ya kuzaliwa kwake, wataalamu wa nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu,
1Kui nüüd Jeesus oli sündinud kuningas Heroodese ajal Juudamaal Petlemma linnas, siis vaata, hommikumaalt saabusid tähetargad Jeruusalemma
2wakauliza, "Yuko wapi mtoto, Mfalme wa Wayahudi, aliyezaliwa? Tumeiona nyota yake ilipotokea mashariki, tukaja kumwabudu."
2ja küsisid: 'Kus on see juutide vastsündinud kuningas? Me nägime tema tähte tõusmas ja oleme tulnud teda kummardama.'
3Mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, yeye pamoja na wakazi wote wa Yerusalemu.
3Seda kuuldes kohkus kuningas Heroodes ja kogu Jeruusalemm koos temaga.
4Basi akawaita pamoja makuhani wakuu wote na walimu wa Sheria, akawauliza, "Kristo atazaliwa wapi?"
4Ja ta kutsus kokku kõik rahva ülempreestrid ja kirjatundjad ning päris nende käest, kus Messias pidi sündima.
5Nao wakamjibu, "Mjini Bethlehemu, mkoani Yudea. Ndivyo nabii alivyoandika:
5Need ütlesid talle: 'Petlemmas Juudamaal, sest nõnda on kirjutatud prohveti käe läbi:
6Ewe Bethlehemu katika nchi ya Yuda, kwa vyovyote wewe si mdogo kabisa kati ya viongozi wa Yuda; maana kwako atatokea kiongozi atakayewaongoza watu wangu, Israeli."
6Ja sina, Petlemm Juudamaal, ei ole Juuda vürstkondadest hoopiski kõige pisem, sest sinust lähtub Valitseja, kes hoiab mu Iisraeli rahvast kui karjane.'
7Hapo, Herode aliwaita faraghani hao wataalamu wa nyota, akawauliza wakati hasa ile nyota ilipowatokea.
7Seepeale laskis Heroodes tähetargad salaja enda juurde kutsuda, päris nendelt täpset aega, millal täht oli paistma hakanud,
8Kisha akawatuma Bethlehemu akisema, "Nendeni mkachunguze kwa makini habari za mtoto huyo. Mkisha mpata nileteeni habari ili nami niende nikamwabudu."
8ja saatis nad Petlemma, öeldes: 'Minge ja uurige täpselt välja, kes see laps on! Ja kui te olete ta leidnud, teatage mulle, et ka mina saaksin minna teda kummardama.'
9Baada ya kumsikiliza mfalme, hao wataalamu wa nyota wakaenda. Kumbe ile nyota waliyokuwa wameiona upande wa mashariki iliwatangulia hata ikaenda kusimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto.
9Tähetargad kuulasid kuninga jutu ära ning asusid teele. Ja vaata, täht, mille tõusmist nad olid näinud, käis nende eel, kuni jäi seisma selle paiga kohale, kus oli laps.
10Walipoiona hiyo nyota, walifurahi mno.
10Tähte nähes rõõmustasid nad üliväga.
11Basi, wakaingia nyumbani, wakamwona yule mtoto pamoja na Maria mama yake; wakapiga magoti, wakamsujudia. Kisha wakafungua hazina zao, wakampa zawadi: dhahabu, ubani na manemane.
11Ja majja sisse astudes nägid nad last koos Maarja, tema emaga, ja kummardasid teda tema ette maha heites, avasid oma aarded ning andsid talle kinke: kulda, viirukit ja mürri.
12Mungu aliwaonya katika ndoto wasimrudie Herode; hivyo wakarudi makwao kwa njia nyingine.
12Ja kui neid unenäos hoiatati, et nad ei läheks enam Heroodese juurest läbi, läksid nad teist teed tagasi oma maale.
13Baada ya wale wageni kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto, akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapokwambia, maana Herode anakusudia kumwua huyu mtoto."
13Kui nüüd tähetargad olid lahkunud, vaata, siis ilmus Issanda ingel Joosepile unenäos ja ütles: 'Tõuse, võta kaasa laps ja tema ema ning põgene Egiptusesse ja jää sinna, kuni ma sind käsin, sest Heroodes tahab lapse üles otsida ja hukata!'
14Hivyo, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akaondoka usiku, akaenda Misri.
14Siis Joosep tõusis, võttis lapse ja tema ema ning põgenes öösel Egiptusesse.
15Akakaa huko mpaka Herode alipokufa. Jambo hilo lilifanyika ili neno alilosema Bwana kwa njia ya nabii litimie: "Nilimwita Mwanangu kutoka Misri."
15Ja ta oli seal Heroodese surmani, et läheks täide, mis Issand on rääkinud prohveti suu kaudu: 'Ma olen kutsunud oma Poja Egiptusest.'
16Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota walikuwa wamemhadaa, alikasirika sana. Akaamuru watoto wote wa kiume mjini Bethlehemu na kandokando yake wenye umri wa miaka miwili na chini yake wauawe. Alifanya hivyo kufuatana na muda aliopata kujua kutoka kwa wale wataalamu wa nyota.
16Kui nüüd Heroodes nägi, et tähetargad on teda petnud, raevutses ta väga ning laskis tappa Petlemmas ja selle piirkonnas kõik poeglapsed, kaheaastased ja nooremad, arvestades seda aega, mille ta oli tähetarkadelt täpselt välja uurinud.
17Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Yeremia:
17Siis läks täide, mida on räägitud prohvet Jeremija kaudu:
18"Sauti imesikika mjini Rama, kilio na maombolezo mengi. Raheli anawalilia watoto wake, wala hataki kutulizwa, maana wote wamefariki."
18'Raamas kuuldakse häält, nutmist ja kaebamist on palju. Raahel nutab oma lapsi ega lase ennast lohutada, sest neid ei ole enam.'
19Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri,
19Kui nüüd Heroodes oli surnud, vaata, siis ilmus Issanda ingel Egiptuses viibivale Joosepile unenäos
20akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa."
20ja ütles: 'Tõuse üles, võta laps ja tema ema ning mine Iisraelimaale, sest need, kes püüdsid last tappa, on surnud!'
21Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli.
21Siis ta tõusis, võttis lapse ja tema ema ning tuli Iisraelimaale.
22Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya,
22Kuulnud aga, et Arhelaos on kuningaks Juudamaal oma isa Heroodese järel, kartis Joosep sinna minna. Teda hoiatati unenäos, et neil tuleb varjuda Galileas,
23akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: "Ataitwa Mnazare."
23ning ta tuli ja asus elama külla, mida kutsutakse Naatsaretiks, et läheks täide, mida on räägitud prohvetite kaudu, et teda hüütakse Naatsaretlaseks.