1"Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
1Taevariik on majaisanda sarnane, kes läks varahommikul välja palkama töötegijaid oma viinamäele.
2Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
2Kui ta oli töölistega päevapalga kokku leppinud ühele teenarile, läkitas ta nad oma viinamäele.
3Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
3Ja kui ta läks välja kolmandal tunnil, nägi ta turul teisi jõude seismas
4Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
4ja ta ütles neilegi: 'Minge ka teie viinamäele, ja ma annan teile, mis iganes õiglane!'
5Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
5Ja need läksid. Taas läks ta välja kuuendal ja üheksandal tunnil ning tegi nõndasamuti.
6Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
6Aga kui ta üheteistkümnendal tunnil välja läks, leidis ta teisi seisvat ja ütles neilegi: 'Mis te siin kogu päeva jõude seisate?'
7Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
7Nad ütlesid talle: 'Meid ei ole keegi palganud.' Ta ütles neile: 'Minge ka teie viinamäele!'
8"Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
8Aga kui õhtu tuli, ütles viinamäe isand oma valitsejale: 'Kutsu töölised ja anna neile palk viimasest kuni esimeseni!'
9Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
9Ja üheteistkümnendal tunnil palgatud tulid ning said igaüks ühe teenari.
10Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
10Kui siis esimesed tulid, oletasid nad, et nemad saavad rohkem, aga nemadki said igaüks ühe teenari.
11Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
11Aga kui nad selle olid saanud, siis nad nurisesid majaisanda üle:
12Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
12'Need viimased on töötanud ainult ühe tunni, ent sina oled teinud nad võrdseks meiega, kes me oleme kandnud päeva koormat ja lõõska!'
13"Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
13Isand aga vastas ühele nendest: 'Sõber, ma ei tee sulle ülekohut! Kas sa ei leppinud minuga kokku ühele teenarile?
14Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
14Võta oma palk ja mine oma teed, aga sellele viimasele tahan ma anda nagu sullegi!
15Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?"
15Kas ma ei tohi enese omaga teha, mida tahan? Või on sinu silm kade, et mina olen hea?'
16Yesu akamaliza kwa kusema, "Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho."
16Nõnda saavad viimased esimesteks ja esimesed jäävad viimasteks. [Sest paljud on kutsutud, aga vähesed on valitud.]'
17Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
17Kui Jeesus läks üles Jeruusalemma, võttis ta kaksteist jüngrit kõrvale ja ütles neile teel:
18"Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
18'Vaata, me läheme üles Jeruusalemma ja Inimese Poeg antakse ülempreestrite ja kirjatundjate kätte ning need mõistavad ta surma
19Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa."
19ja annavad ta paganate kätte teotada ja piitsutada ja risti lüüa; ning kolmandal päeval äratatakse ta üles.'
20Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
20Siis astus Sebedeuse poegade ema koos oma poegadega Jeesuse juurde, kummardas ja palus temalt midagi.
21Yesu akamwuliza, "Unataka nini?" Huyo mama akamwambia, "Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto."
21Jeesus küsis: 'Mida sa tahad?' Naine ütles talle: 'Ütle, et need mu kaks poega istuksid su Kuningriigis üks su paremal ja teine su pahemal käel!'
22Yesu akajibu, "Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?" Wakamjibu, "Tunaweza."
22Aga Jeesus kostis: 'Teie ei tea, mida te palute. Kas te võite juua karikast, mida minul tuleb juua?' Nad vastasid talle: 'Võime küll!'
23Yesu akawaambia, "Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu."
23Tema ütles neile: 'Küllap te joote minu karikast, kuid istuda mu paremal või pahemal käel - ei ole minul seda anda, vaid see antakse neile, kellele mu Isa selle on valmistanud.'
24Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
24Ja kui need kümme sellest kuulsid, läks nende meel pahaseks kahe venna peale.
25Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, "Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
25Aga Jeesus kutsus nad enese juurde ja ütles: 'Te teate, et rahvaste valitsejad peremehetsevad nende üle ja suured meelevallatsevad nende kallal.
26Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
26Nõnda ei tohi olla teie seas, vaid kes iganes teie seas tahab saada suureks, olgu teie teenija,
27na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
27ja kes iganes teie seas tahab olla esimene, olgu teie sulane,
28Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi."
28nii nagu Inimese Poeg ei ole tulnud, et lasta ennast teenida, vaid et ise teenida ja anda oma elu lunaks paljude eest!'
29Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
29Ja Jeerikost välja minnes läks Jeesusega kaasa suur rahvahulk.
30Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
30Ja vaata, kaks pimedat istus tee ääres. Kui nad kuulsid, et Jeesus möödub, kisendasid nad: 'Halasta meie peale, Issand, Taaveti Poeg!'
31Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
31Rahvahulk aga sõitles neid, et nad vaikiksid. Kuid nemad kisendasid veel rohkem: 'Halasta meie peale, Issand, Taaveti Poeg!'
32Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, "Mnataka niwafanyie nini?"
32Ja Jeesus seisatas, kutsus neid ja ütles: 'Mida te tahate, et ma teile teeksin?'
33Wakamjibu, "Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe."
33Nemad ütlesid talle: 'Issand, et meie silmad avaneksid!'
34Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.
34Jeesusel hakkas neist hale ja ta puudutas nende silmi. Ja kohe nägid nad jälle ning läksid temaga kaasa.