1Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata.
1Kui siis Jeesus tuli mäelt alla, järgnesid talle suured rahvahulgad.
2Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, "Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!"
2Ja vaata, tema juurde astus pidalitõbine, kummardas teda ja ütles: 'Issand, kui sa tahad, siis sa võid mu puhtaks teha!'
3Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, "Nataka! Takasika." Mara huyo mtu akapona ukoma wake.
3Ja Jeesus sirutas käe välja, puudutas teda ja ütles: 'Ma tahan, saa puhtaks!' Ja ta sai otsekohe oma pidalitõvest puhtaks.
4Kisha Yesu akamwambia, "Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka iliyoamriwa na Mose kuwathibitishia kwamba umepona."
4Ja Jeesus ütles talle: 'Vaata, et sa sellest kellelegi ei räägi, vaid mine näita ennast preestrile ja ohverda and, mis Mooses on käskinud, neile tunnistuseks!'
5Yesu alipokuwa anaingia mjini Kafarnaumu, ofisa mmoja Mroma alimwendea, akamsihi
5Aga kui Jeesus tuli Kapernauma, astus tema juurde väeülem ja palus teda:
6akisema, "Mheshimiwa, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza na anaumwa sana."
6'Issand, minu teener lamab kodus halvatuna maas hirmsas piinas!'
7Yesu akamwambia, "Nitakuja kumponya."
7Jeesus ütles talle: 'Kas ma tulen ja teen ta terveks?'
8Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, sistahili uingie nyumbani mwangu. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona.
8Ent väeülem vastas: 'Ei, Issand, ma ei ole seda väärt, et sina mu katuse alla tuleksid. Ütle ainult üks sõna ja mu teener paraneb!
9Maana, hata mimi niliye mtu chini ya mamlaka ya wengine, ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda! naye huenda; na mwingine, Njoo! naye huja; na mtumishi wangu, Fanya kitu hiki! naye hufanya."
9Minagi olen ju inimene meelevalla all, aga minu käsu all on sõdureid ja kui ma ütlen ühele: 'Mine ära!', siis ta läheb, ja teisele: 'Tule siia!', siis ta tuleb, ja oma teenijale: 'Tee seda!', siis ta teeb.'
10Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia watu waliokuwa wanamfuata, "Kweli nawaambieni, sijapata kumwona mtu yeyote katika Israeli aliye na imani kama hii.
10Aga seda kuuldes Jeesus imestas ja ütles neile, kes temaga kaasas käisid: 'Tõesti, ma ütlen teile, nii suurt usku ei ole ma leidnud Iisraelis ühelgi!
11Basi, nawaambieni kwamba watu wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo katika Ufalme wa mbinguni.
11Ma ütlen aga teile, et paljud tulevad idast ja läänest ning istuvad lauda Aabrahami ja Iisaki ja Jaakobiga taevariigis,
12Lakini wale ambao wangalipaswa kuwa katika Ufalme huo watatupwa nje, gizani, ambako watalia na kusaga meno."
12Kuningriigi lapsed aga tõugatakse välja kaugele pimedusse, kus on ulgumine ja hammaste kiristamine.'
13Kisha Yesu akamwambia huyo ofisa Mroma, "Nenda nyumbani; na iwe kama ulivyoamini." Na mtumishi wake akapona saa ileile.
13Ja Jeesus ütles väeülemale: 'Mine! Nagu sa oled uskunud, nõnda sündigu sulle!' Ja tema teener paranes selsamal tunnil.
14Yesu alifika nyumbani kwa Petro, akamkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, ana homa kali.
14Ja Jeesus, tulnud Peetruse majja, nägi tema ämma lamavat palavikus.
15Basi, Yesu akamgusa huyo mama mkono, na homa ikamwacha; akasimama, akamtumikia.
15Ja Jeesus puudutas ta kätt, ning palavik lahkus temast. Ja ämm tõusis üles ning teenis teda.
16Ilipokuwa jioni, walimletea watu wengi waliokuwa wamepagawa na pepo; naye, kwa kusema neno tu, akawafukuza hao pepo. Aliwaponya pia watu wote waliokuwa wagonjwa.
16Aga õhtu jõudes toodi Jeesuse juurde palju kurjadest vaimudest vaevatuid, ja ta ajas neist vaimud välja sõnaga ning tervendas kõik haiged,
17Alifanya hivyo ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie: "Yeye mwenyewe ameondoa udhaifu wetu, ameyachukua magonjwa yetu."
17et läheks täide, mida on räägitud prohvet Jesaja kaudu: 'Ta on võtnud ära meie haigused ja kandnud meie tõved.'
18Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ng'ambo ya ziwa.
18Aga kui Jeesus nägi rahvahulka enese ümber, käskis ta minna vastaskaldale.
19Mwalimu mmoja wa Sheria akamwendea, akamwambia, "Mwalimu, mimi nitakufuata kokote uendako."
19Ja üks kirjatundja ütles tema juurde astudes: 'Õpetaja, ma tahan sulle järgneda, kuhu sa ka iganes läheksid!'
20Yesu akamjibu, "Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia."
20Ja Jeesus vastas talle: 'Rebastel on urud ja taeva lindudel pesad, aga Inimese Pojal ei ole, kuhu ta oma pea võiks panna.'
21Kisha mtu mwingine miongoni mwa wanafunzi wake akamwambia, "Bwana, niruhusu kwanza niende nikamzike baba yangu."
21Üks teine tema jüngritest ütles talle: 'Issand, luba mul enne minna matma oma isa!'
22Lakini Yesu akamwambia, "Nifuate! Waache wafu wazike wafu wao."
22Aga Jeesus vastas talle: 'Järgne mulle ja lase surnuil oma surnud matta!'
23Yesu alipanda mashua, na wanafunzi wake wakaenda pamoja naye.
23Jeesus astus nüüd paati ja ta jüngrid läksid temaga kaasa.
24Ghafla, dhoruba kali ikatokea ziwani, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua. Yesu alikuwa amelala usingizi.
24Ja vaata, järvel tõusis suur torm, nii et lained katsid paadi. Aga Jeesus magas.
25Wanafunzi wakamwendea, wakamwamsha wakisema, "Bwana, tuokoe, tunaangamia!"
25Ja jüngrid tulid ta juurde ja äratasid ta üles, öeldes: 'Issand, aita! Me hukkume!'
26Yesu akawaambia, "Enyi watu wenye imani haba; mbona mnaogopa?" Basi, akainuka, akazikemea pepo na mawimbi; kukawa shwari kabisa.
26Tema ütles neile: 'Miks te olete nõnda arad, te nõdrausulised?' Siis ta tõusis püsti, sõitles tuuli ja järve ning järv jäi täiesti vaikseks.
27Watu wakashangaa, wakasema, "Ni mtu wa namna gani huyu? Hata pepo na mawimbi vinamtii!"
27Inimesed aga imestasid, öeldes: 'Kes ta siis selline on, et isegi tuuled ja järv kuulavad tema sõna?'
28Yesu alifika katika nchi ya Wagerasi, ng'ambo ya ziwa, na huko watu wawili waliopagawa na pepo wakakutana naye wakitokea makaburini. Watu hawa walikuwa wenye kutisha mno, hata hakuna mtu aliyethubutu kupita katika njia hiyo.
28Ja kui Jeesus jõudis vastaskaldale gadaralaste maale, juhtus talle vastu kaks hauakambreist tulnud kurjast vaimust vaevatut, kes olid hirmsad ja väga ohtlikud, nii et keegi ei saanud käia seda teed.
29Nao wakaanza kupiga kelele, "Una shauri gani nasi, wewe Mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya wakati wake?"
29Ja vaata, need karjusid: 'Mis on meil sinuga asja, sa Jumala Poeg? Kas sa oled tulnud meid enneaegu piinama?'
30Karibu na mahali hapo kulikuwa na nguruwe wengi wakichungwa.
30Aga tükk maad neist eemal oli suur seakari söömas.
31Basi, hao pepo wakamsihi, "Ikiwa utatutoa, basi uturuhusu tuwaingie nguruwe wale."
31Kurjad vaimud palusid siis teda: 'Kui sa meid välja ajad, siis läkita meid seakarja sisse!'
32Yesu akawaambia, "Haya, nendeni." Hapo wakawatoka watu hao, wakawaingia nguruwe. Kundi lote la nguruwe likaporomoka kwenye ule mteremko mkali, likatumbukia ziwani; nguruwe wote wakafa maji.
32Ja ta ütles neile: 'Minge!' Siis need tulid välja ja läksid sigade sisse. Ja vaata, kogu kari sööstis järsakult järve ja uppus.
33Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakaenda mjini. Huko walitoa habari zote na mambo yaliyowapata wale watu waliokuwa wamepagawa.
33Karjased aga põgenesid ja läksid linna ja kuulutasid kõike ning kurjast vaimust vaevatute lugu.
34Basi, watu wote katika mji ule walitoka, wakamwendea Yesu; na walipomwona, wakamsihi aondoke katika nchi yao.
34Ja vaata, kogu linn tuli välja Jeesusele vastu. Ja teda nähes nad palusid, et ta lahkuks nende paikkonnast.