1Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
1Ja Jeesus astus paati ja tuli teisele poole järve oma kodulinna.
2Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako."
2Ja vaata, tema juurde kanti üks halvatu, kes oli kanderaamil. Ja nende usku nähes ütles Jeesus halvatule: 'Ole julge, poeg, sinu patud on sulle andeks antud!'
3Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, "Mtu huyu anamkufuru Mungu!"
3Ja vaata, mõned kirjatundjad mõtlesid endamisi: 'See teotab Jumalat!'
4Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, "Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
4Jeesus, teades nende mõtteid, ütles neile: 'Mispärast te mõtlete kurja oma südames?
5Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
5Sest kumb on kergem, kas öelda: 'Sinu patud on andeks antud!' või öelda: 'Tõuse püsti ja kõnni!'?
6Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako."
6Aga et te teaksite, et Inimese Pojal on meelevald patte andeks anda maa peal,' - siis ta ütles halvatule - 'tõuse püsti, võta oma kanderaam ja mine koju!'
7Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
7Ja too tõusis ning läks koju.
8Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
8Seda nähes hakkasid rahvahulgad kartma ja ülistasid Jumalat, kes annab inimestele sellise meelevalla.
9Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, "Nifuate." Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
9Ja sealt edasi minnes nägi Jeesus meest, Matteus nimi, tollihoone juures istuvat, ja ütles talle: 'Järgne mulle!' Ja Matteus tõusis ning järgnes talle.
10Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
10Ja kui Jeesus istus lauas tema kodus, vaata, palju tölnereid ja muid patuseid tuli ning istus koos Jeesuse ja ta jüngritega.
11Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, "Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
11Ja seda nähes ütlesid variserid tema jüngritele: 'Miks teie õpetaja sööb koos tölnerite ja patustega?'
12Yesu aliwasikia, akasema, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
12Aga seda kuuldes vastas Jeesus: 'Ei vaja arsti terved, vaid haiged.
13Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi."
13Aga minge ning õppige, mis see on: Ma ei taha ohvrit, vaid halastust! Jah, ma ei ole tulnud kutsuma õigeid, vaid patuseid!'
14Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, "Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?"
14Siis tulid ta juurde Johannese jüngrid ja küsisid: 'Miks meie ja variserid paastume, sinu jüngrid aga ei paastu?'
15Yesu akawajibu, "Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
15Ja Jeesus ütles neile: 'Ega peiupoisid või leinata sel ajal, kui peigmees on nende juures!? Ent päevad tulevad, mil peigmees neilt ära võetakse, küll nad siis paastuvad!
16"Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
16Aga keegi ei paika vanutamata riidetükiga vana kuube, sest paik rebeneks küljest ja käristaks augu veel suuremaks.
17Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama."
17Ei kallata ka värsket veini vanadesse nahklähkritesse, muidu lähkrid rebeneksid ja vein voolaks maha ning lähkrid muutuksid kõlbmatuks, vaid värske vein kallatakse uutesse lähkritesse, ja siis säilivad mõlemad.'
18Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, "Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi."
18Kui Jeesus seda neile rääkis, vaata, siis tuli üks ülem, kummardas teda ja ütles: 'Mu tütar suri äsja, kuid tule, pane oma käsi ta peale, siis ta ärkab ellu!'
19Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
19Ja Jeesus tõusis, läks temaga kaasa ja samuti ta jüngrid.
20Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
20Ja vaata, üks naine, kes oli olnud veritõves kaksteist aastat, tuli ta selja taha ja puudutas ta kuue palistust,
21Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
21sest naine mõtles endamisi: 'Kui ma ainult saaksin puudutada tema kuube, siis ma pääseksin!'
22Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, "Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya." Mama huyo akapona saa ileile.
22Aga Jeesus pöördus ja sõnas teda nähes: 'Tütar, ole julge, sinu usk on su päästnud!' Ja naine sai terveks selsamal hetkel.
23Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
23Kui Jeesus ülema majja jõudis ning nägi vilepuhujaid ja käratsevat rahvahulka,
24akasema, "Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu." Nao wakamcheka.
24siis ta ütles: 'Hoiduge eemale, tüdruk ei ole surnud, vaid magab!' Aga nad naersid tema üle.
25Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
25Ent kui rahvahulk oli välja aetud, läks Jeesus sisse, võttis tal käest kinni ja tüdruk ärkas üles.
26Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
26Ja kuuldus sellest levis üle kogu selle maa.
27Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, "Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
27Kui Jeesus sealt edasi läks, järgnesid talle kaks pimedat, kisendades: 'Taaveti Poeg, halasta meie peale!'
28Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, "Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?" Nao wakamjibu, "Naam, Mheshimiwa."
28Kui ta siis koju tuli, astusid pimedad ta juurde. Ja Jeesus küsis neilt: 'Kas te usute, et mina võin seda teha?' Nemad ütlesid talle: 'Jah, Issand!'
29Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, "Na iwe kwenu kama mnavyoamini."
29Siis ta puudutas nende silmi ja ütles: 'Teile sündigu teie usku mööda!'
30Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: "Msimwambie mtu yeyote jambo hili."
30Ja nende silmad avanesid. Ja Jeesus hoiatas neid: 'Vaadake, et keegi sellest teada ei saaks!'
31Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
31Aga nemad läksid välja ja levitasid juttu tema kohta kogu sellel maal.
32Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
32Kui need olid lahkunud, vaata, siis toodi tema juurde tumm mees, kes oli kurjast vaimust vaevatud.
33Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, "Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!"
33Ja kui kuri vaim oli välja aetud, hakkas tumm rääkima. Rahvahulgad panid seda imeks ja ütlesid: 'Sellist asja ei ole Iisraelis iialgi nähtud!'
34Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, "Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya."
34Variserid aga ütlesid: 'Ta ajab kurje vaime välja kurjade vaimude ülema abil.'
35Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
35Ja Jeesus rändas läbi kõik linnad ja külad, õpetades nende sünagoogides ja jutlustades evangeeliumi Kuningriigist ja parandades kõik haigused ja kõik nõtrused.
36Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
36Aga rahvahulka nähes hakkas tal neist hale, sest nad olid väsitatud ja vaevatud otsekui lambad, kellel ei ole karjast.
37Hapo akawaambia wanafunzi wake, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
37Siis ta ütles oma jüngritele: 'Lõikust on palju, töötegijaid aga vähe.
38Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake."
38Paluge siis lõikuse Issandat, et ta saadaks töötegijaid välja oma lõikusele!'