1Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu, na upinde wa mvua kichwani mwake. Uso wake ulikuwa kama jua, na miguu yake ilikuwa kama moto.
1Ma nägin teist võimsat inglit maha tulevat taevast, riietatud pilve, ning tema pea kohal oli vikerkaar ning ta palged olid nagu päike ning ta jalad nagu tulesambad
2Mikononi mwake alishika kitabu kidogo kimefunguliwa. Aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari, na wa kushoto juu ya nchi kavu,
2ning ta käes oli avatud väike rullraamat. Ta pani oma parema jala mere peale ja vasaku jala maa peale
3na kuita kwa sauti kubwa kama ya mngurumo wa simba. Alipopaaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo.
3ning kisendas suure häälega, otsekui lõvi möirgaks. Kui ta kisendas, rääkisid seitse pikset oma kõuemürinaga.
4Na hizo ngurumo saba ziliposema, mimi nikataka kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni: "Maneno ya ngurumo hizo saba ni siri; usiyaandike!"
4Ja kui need seitse pikset olid rääkinud, siis ma tahtsin hakata kirjutama. Ma kuulsin häält taevast hüüdvat: 'Pane pitseriga kinni, mis need seitse pikset on kõnelnud, ning ära kirjuta seda!'
5Kisha yule malaika niliyemwona akisimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni,
5Ingel, keda ma nägin seisvat mere peal ja maa peal, tõstis oma parema käe taeva poole
6akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, Mungu aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, bahari na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo. Akasema, "Wakati wa kusubiri zaidi umekwisha!
6ning vandus selle nimel, kes elab igavesest ajast igavesti, kes on loonud taeva ja mis seal on ning maa ja mis seal on ning mere ja mis seal on: Aega enam ei kulu,
7Lakini wakati ule malaika wa saba atakapotoa sauti yake, wakati atakapopiga tarumbeta yake, Mungu atakamilisha mpango wake wa siri kama alivyowatangazia watumishi wake manabii."
7vaid seitsmenda ingli hääle päevil, kui ta hakkab pasunat puhuma, siis on läinud täide Jumala saladus, nagu ta seda rõõmusõnumit on kuulutanud prohvetitele, oma sulastele.
8Kisha ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni pale awali ikasema nami tena: "Nenda ukakichukue kile kitabu kilichofunguliwa, kilicho mkononi mwa malaika asimamaye juu ya bahari na juu ya nchi kavu."
8Hääl, mida ma kuulsin taevast, rääkis minuga jälle ja ütles: 'Mine võta avatud raamat ingli käest, kes seisab mere peal ja maa peal!'
9Basi, nikamwendea huyo malaika, nikamwambia anipe hicho kitabu kidogo. Naye akaniambia, "Kichukue, ukile; kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali, lakini tumboni kitakuwa kichungu!"
9Ja ma läksin ingli juurde ja ütlesin, et ta annaks mulle raamatu. Tema ütles mulle: 'Võta ja söö see ära! See muutub su kõhus mõruks, kuid su suus on see magus nagu mesi.'
10Basi, nikakichukua kitabu hicho kidogo kutoka mkononi mwa huyo malaika, nikakila; nacho kilikuwa kitamu kinywani mwangu kama asali, lakini nilipokimeza kikawa kichungu tumboni mwangu.
10Ja ma võtsin ingli käest raamatu ning sõin selle ära, ning see oli mu suus magus nagu mesi, ja siis, kui ma olin selle söönud, hakkas mul kõhus mõru.
11Kisha nikaambiwa, "Inakubidi tena kutangaza ujumbe wa Mungu kuhusu watu wengi, mataifa, watu wa lugha nyingi na wafalme!"
11Ja mulle öeldi: 'Sa pead jälle ennustama rahvaste ja paganate ja keelte ja paljude kuningate kohta!'