Swahili: New Testament

Estonian

Revelation

9

1Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu.
1Viies ingel puhus pasunat ning ma nägin tähe olevat kukkunud taevast ilmamaa peale. Sellele anti sügavuse kaevu võti
2Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu.
2ning ta avas sügavuse kaevu ja kaevust tõusis suitsu otsekui suurest ahjust, ning päike ja õhk pimenesid kaevu suitsust.
3Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.
3Suitsust tulid ilmamaa peale rohutirtsud, ja neile anti meelevald, nagu skorpionidel on meelevald ilmamaa peal.
4Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti yoyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.
4Neile öeldi, et nad ei tohi teha kurja ilmamaa rohule ega millelegi, mis haljendab, ega ühelegi puule, vaid ainult inimestele, kellel ei ole Jumala pitserit otsaesisel.
5Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano. Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
5Ja neile anti käsk, et nad neid ei tapaks, vaid et nad neid piinaksid viis kuud, ning nende piinamine on otsekui skorpioni piinamine, kui ta inimest salvab.
6Muda huo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata; watatamani kufa lakini kifo kitawakimbia.
6Neil päevil inimesed otsivad surma ega leia seda, nad igatsevad surra, aga surm põgeneb nende eest.
7Kwa kuonekana, nzige hao walikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita. Juu ya vichwa vyao walikuwa na taji zilizo kama za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
7Ja rohutirtsud olid välimuselt sõjaks seatud hobuste sarnased, neil olid pärjad peas otsekui kullast ning nende palged olid nagu inimeste palged
8Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
8ja juuksed nagu naiste juuksed ja nende hambad olid otsekui lõvidel.
9Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.
9Neil olid üll soomusrüüd otsekui raudrüüd ning nende tiibade kahin oli otsekui kaarikute mürin, kui palju hobuseid jookseb sõtta.
10Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano.
10Ja neil olid sabad ja astlad nagu skorpionidel, ning nende sabades oli meelevald teha inimestele kahju viis kuud.
11Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi.
11Nende kuningas oli sügavuse ingel, kelle nimi heebrea keeles on Abaddon, ja kreeka keeles Apollüon.
12Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanafuata.
12Esimene häda on möödas, ennäe, pärast seda tuleb veel kaks häda.
13Kisha malaika wa sita akapiga tarumbeta yake. Nami nikasikia sauti moja kutoka katika pembe nne za madhabahu ya dhahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
13Kuues ingel puhus pasunat ning ma kuulsin üht häält Jumala ees oleva kuldaltari neljast nurgast,
14Sauti hiyo ikamwambia huyo malaika wa sita mwenye tarumbeta, "Wafungulie malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Eufrate!"
14see hüüdis kuuendale inglile, kelle käes oli pasun: 'Lase lahti need neli inglit, kes on ahelais suure Eufrati jõe ääres!'
15Naye akawafungulia malaika hao wanne ambao walikuwa wametayarishwa kwa ajili ya saa hiyo ya siku ya mwezi huo, wa mwaka huohuo, kuua theluthi moja ya wanaadamu.
15Siis päästeti valla need neli inglit, kes on valmistunud selleks tunniks ja päevaks ja kuuks ja aastaks, et tappa kolmandik inimestest.
16Nilisikia idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili.
16Ja sõjaväe ratsanike arv oli kakskümmend tuhat korda kümme tuhat - ma kuulsin nende arvu -,
17Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika hiyo njozi: Walikuwa na ngao vifuani zilizokuwa moto mtupu, zenye rangi ya samawati na njano kama kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vya simba; na moto, moshi, na kiberiti vilikuwa vinatoka kinywani mwao.
17ning nõnda ma nägin oma nägemuses hobuseid ja nendel istujaid. Neil olid tulipunased ja sinised ja väävelkollased soomusrüüd ning hobuste pead olid nagu lõvide pead ning nende suust tuli välja tuld ja suitsu ja väävlit.
18Theluthi moja ya wanaadamu waliuawa kwa mabaa hayo matatu yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vyao;
18Nende kolme nuhtluse poolt tapeti kolmandik inimesi: tule ja suitsu ja väävli läbi, mis tuli nende suust.
19maana nguvu ya farasi hao ilikuwa vinywani mwao na katika mikia yao. Mikia yao ilikuwa na vichwa kama nyoka, na waliitumia hiyo kuwadhuru watu.
19Hobuste meelevald oli nende suus ja nende sabades, sest nende sabad olid madude sarnased, neil olid pead ning nendega nad tegid kahju.
20Wanaadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakugeuka na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; bali wakaendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.
20Aga inimesed, keda neis nuhtlustes ei tapetud, ei parandanud meelt oma kätetööst, et nad oleksid loobunud kummardamast kurje vaime ning kuld- ja hõbe- ja vask- ja kivi- ja puujumalaid, kes ei suuda näha ega kuulda ega kõndida.
21Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.
21Nad ei parandanud meelt oma mõrvadest ega oma nõidustest ega oma hoorustest ega oma vargustest.