Swahili: New Testament

Estonian

Revelation

8

1Na Mwanakondoo alipouvunja mhuri wa saba, kukawa kimya mbinguni kwa muda wa nusu saa.
1Kui Tall avas seitsmenda pitseri, sündis taevas vaikus ligi pooleks tunniks.
2Kisha nikawaona wale malaika saba wanaosimama mbele ya Mungu wamepewa tarumbeta saba.
2Ja ma nägin neid seitset inglit, kes seisid Jumala palge ees, ning neile anti seitse pasunat.
3Malaika mwingine akafika, akiwa anachukua chetezo cha dhahabu, akasimama mbele ya madhabahu ya kufukizia ubani. Naye akapewa ubani mwingi autoe sadaka pamoja na sala za watu wote wa Mungu, juu ya madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kiti cha enzi.
3Ning üks teine ingel tuli ja seisis altari ette, kuldne suitsutusastja käes, ja talle anti palju suitsutusrohte, et ta paneks neid koos kõikide pühade palvetega kuldaltarile, mis on trooni ees.
4Moshi wa ubani ukapanda juu, pamoja na sala za watu wa Mungu, kutoka mikononi mwake huyo malaika aliyekuwa mbele ya Mungu.
4Ja suitsutusrohtude suits tõusis koos pühade palvetega ingli käest Jumala ette.
5Kisha malaika akakichukua hicho chetezo, akakijaza moto wa madhabahuni akakitupa duniani. Kukawa na ngurumo, sauti, umeme na tetemeko la ardhi.
5Ja ingel võttis suitsutusastja ning täitis selle tulega altarilt ja viskas ilmamaa peale, ning sündis pikselööke ja kõuemürinaid ja välke ja maavärinat.
6Kisha wale malaika saba wenye tarumbeta saba wakajiweka tayari kupiga mbiu ya mgambo.
6Ja need seitse inglit, kelle käes oli seitse pasunat, seadsid end pasunat puhuma.
7Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake. Mchanganyiko wa mvua ya mawe na moto, pamoja na damu, ukamwagwa juu ya nchi. Theluthi moja ya nchi ikaungua, theluthi moja ya miti ikaungua, na majani yote mabichi yakaungua.
7Esimene puhus pasunat ning sündis rahet ja tuld segamini verega ja see visati ilmamaa peale ning kolmandik ilmamaad põles ära ja kolmandik puudest põles ära ning kõik haljas rohi põles ära.
8Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake. Na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto ukatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikawa damu,
8Teine ingel puhus pasunat ning otsekui suur tules põlev mägi visati merre ning kolmandik merd muutus vereks,
9theluthi moja ya viumbe vya baharini vikafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
9ja kolmandik mereloomi, kel hing sees, suri ära, ja kolmandik laevu läks põhja.
10Kisha malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa ikiwaka kama bonge la moto, ikaanguka kutoka mbinguni, na kutua juu ya theluthi moja ya mito na chemchemi za maji.
10Kolmas ingel puhus pasunat ning taevast kukkus maha suur täht, mis põles otsekui tõrvik ning kukkus kolmandiku jõgede ja veeallikate peale.
11(Nyota hiyo inaitwa "Uchungu.") Basi, theluthi moja ya maji yakawa machungu; watu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.
11Tähe nimi oli Koirohi. Kolmandik vetest muutus koirohuks ning palju inimesi suri vee kätte, sest see oli läinud mõruks.
12Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta yake. Ndipo theluthi moja ya jua, ya mwezi na ya nyota ikapata pigo; hata mwangaza ukapoteza theluthi moja ya mng'ao wake. Theluthi moja ya mchana ikakosa mwanga, hali kadhalika na theluthi moja ya usiku.
12Neljas ingel puhus pasunat ning kustutati kolmandik päikest ja kolmandik kuud ja kolmandik tähti, nii et kolmandik neist pimeneks ja kolmandik päeva ei paistaks ja ööd nõndasamuti.
13Kisha nikatazama, nikasikia tai akiruka juu kabisa angani anasema kwa sauti kubwa, "Ole, ole, ole kwa wanaoishi duniani wakati malaika watatu waliobaki watakapopiga tarumbeta zao!"
13Ja ma nägin ja kuulsin üht kotkast keset taevast lendamas ning suure häälega hüüdmas: 'Häda, häda, häda neile, kes elavad ilmamaa peal, nende kolme ingli pasunahääle pärast, kes alles hakkavad pasunat puhuma!'