1Baada ya hayo nikawaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za dunia wakishika pepo nne za dunia ili upepo usivume hata kidogo: wala katika nchi, wala baharini, wala kwenye miti.
1Pärast seda ma nägin nelja inglit seisvat ilmamaa neljal nurgal kinni pidamas ilmamaa nelja tuult, et tuul ei puhuks ilmamaa peale ega mere peale ega ühegi puu peale.
2Kisha nikamwona malaika mwingine akipanda juu kutoka mashariki akiwa na mhuri wa Mungu aliye hai. Akapaaza sauti na kuwaambia hao malaika wanne waliokabidhiwa jukumu la kuiharibu nchi na bahari,
2Ja ma nägin teist inglit tulevat üles päevatõusu poolt, temal oli elava Jumala pitsat ning ta hüüdis suure häälega neile neljale inglile, kellel oli lastud teha kahju ilmamaale ja merele:
3"Msiharibu nchi, wala bahari, wala miti, mpaka tutakapokwisha wapiga mhuri watumishi wa Mungu wetu katika paji la uso."
3'Ärge tehke kahju ilmamaale ega merele ega puudele, enne kui me oleme pannud pitseri oma Jumala sulaste otsaesisele!'
4Kisha nikasikia idadi ya hao waliopigwa mhuri: Watu mia moja arobaini na nne elfu wa makabila yote ya watu wa Israeli.
4Ma kuulsin pitseriga märgitute arvu: sada nelikümmend neli tuhat pitseriga märgitut kõigist Iisraeli laste suguharudest:
5Kabila la Yuda walikuwa watu kumi na mbili elfu; kabila la Reubeni, kumi na mbili elfu, kabila la Gadi, kumi na mbili elfu;
5Juuda suguharust kaksteist tuhat, Ruubeni suguharust kaksteist tuhat, Gaadi suguharust kaksteist tuhat,
6Kabila la Asheri, kumi na mbili elfu; kabila la Naftali, kumi na mbili elfu; kabila la Manase, kumi na mbili elfu;
6Aaseri suguharust kaksteist tuhat, Naftali suguharust kaksteist tuhat, Manasse suguharust kaksteist tuhat,
7kabila la Simeoni, kumi na mbili elfu, kabila la Lawi, kumi na mbili elfu, kabila la Isakari, kumi na mbili elfu;
7Siimeoni suguharust kaksteist tuhat, Leevi suguharust kaksteist tuhat, Issaskari suguharust kaksteist tuhat,
8kabila la Zabuloni, kumi na mbili elfu; kabila la Yosefu, kumi na mbili elfu, na kabila la Benyamini, kumi na mbili elfu.
8Sebuloni suguharust kaksteist tuhat, Joosepi suguharust kaksteist tuhat, Benjamini suguharust kaksteist tuhat pitseriga märgitut.
9Kisha nikatazama, nikaona umati mkubwa wa watu wasiohesabika: watu wa kila taifa, ukoo, jamaa na lugha. Nao walikuwa wamesimama mbele ya kiti cha enzi na mbele ya Mwanakondoo, wakiwa wamevaa mavazi meupe na kushika matawi ya mitende mikononi mwao.
9Pärast seda ma nägin, ennäe: suur rahvahulk, keda ükski ei suutnud loendada, kõigist paganahõimudest ja suguharudest ja rahvastest ja keeltest seisis trooni ees ning Talle ees, valged rüüd üll ja palmioksad käes.
10Wakapaaza sauti: "Ukombozi wetu watoka kwa Mungu wetu aketiye juu ya kiti cha enzi, na kutoka kwa Mwanakondoo!"
10Nad hüüdsid suure häälega: 'Pääste on meie Jumalal, kes istub Troonil, ja Tallel!'
11Malaika wote wakasimama kukizunguka kiti cha enzi, wazee na vile viumbe hai vinne. Wakaanguka kifudifudi mbele ya kiti cha enzi, wakamwabudu Mungu,
11Kõik inglid seisid trooni ja vanemate ja nelja olevuse ümber ning heitsid trooni ette silmili maha ja kummardasid Jumalat,
12wakisema, "Amina! Sifa, utukufu, hekima, shukrani, heshima, uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu, milele na milele! Amina!"
12hüüdes: 'Aamen! Õnnistus ja kirkus ja tarkus ja tänu ja au ja vägi ja võim olgu meie Jumalale igavesest ajast igavesti! Aamen.'
13Mmoja wa hao wazee akaniuliza, "Hawa waliovaa mavazi meupe ni watu gani? Na wametoka wapi?"
13Ja üks vanematest kõneles ja ütles mulle: 'Need seal valgetes rüüdes - kes nad on ja kust nad tulid?'
14Nami nikamjibu, "Mheshimiwa, wewe wajua!" Naye akaniambia, "Hawa ni wale waliopita salama katika ule udhalimu mkuu. Waliyaosha mavazi yao katika damu ya Mwanakondoo, yakawa meupe kabisa.
14Ma vastasin talle: 'Mu isand, sina tead.' Ning tema ütles mulle: 'Need on need, kes tulevad suurest viletsusest ning on pesnud oma rüüd ja teinud need valgeks Talle veres.
15Ndiyo maana wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Humtumikia Mungu mchana na usiku katika Hekalu lake; naye aketiye juu ya kiti cha enzi atatandaza hema lake juu yao kuwalinda.
15Sellepärast nad on Jumala trooni ees ning on teenimas teda ööd ja päevad tema templis. See, kes istub troonil, laotab oma telgi nende üle.
16Hawataona tena njaa wala kiu; jua wala joto kali halitawachoma tena,
16Neile ei tule iial enam nälga ega iial enam janu, ka ei lange nende peale päikest ega mingit lõõska,
17kwa sababu Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi atakuwa mchungaji wao, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji ya uzima. Naye Mungu atayafuta machozi yote machoni mwao."
17sest Tall, kes on trooni keskel, hoiab neid kui karjane ja juhatab nad eluvee allikaile; ning Jumal pühib ära iga pisara nende silmist.'