1Kisha ishara kubwa ikaonekana mbinguni. Palikuwa hapo mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi chini ya miguu yake, na taji ya nyota kumi na mbili juu ya kichwa chake!
1Suur tunnustäht sai nähtavaks taevas: naine, riietatud päikesesse, ning kuu tema jalge all, ning pärg kaheteistkümnest tähest tema peas.
2Alikuwa mja mzito, na akapaaza sauti kwa maumivu na uchungu wa kujifungua mtoto.
2Ja ta oli lapseootel ning kisendas tuhudes ja piinles sünnitusvaludes.
3Ishara nyingine ikatokea mbinguni: joka kubwa jekundu na lenye pembe kumi na vichwa saba; na kila kichwa kilikuwa na taji.
3Taevas sai nähtavaks teine tunnustäht, ennäe: suur tulipunane lohe, kellel oli seitse pead ja kümme sarve ning ta peadel seitse peaehet.
4Joka hilo liliburuta kwa mkia wake theluthi moja ya nyota za anga na kuzitupa duniani. Nalo lilisimama mbele ya huyo mama aliyekuwa karibu kujifungua mtoto, tayari kabisa kummeza mtoto, mara tu atakapozaliwa.
4Ta saba pühkis ära kolmandiku taevatähti ning viskas need maa peale. Ja lohe seisatas naise ees, kes oli sünnitamas, et niipea kui ta on sünnitanud, süüa ära ta laps.
5Kisha mama huyo akajifungua mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Lakini mtoto akanyakuliwa na kupelekwa kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi.
5Ja naine tõi ilmale poeglapse, kes karjasena hoiab raudsauaga kõiki paganaid. See laps haarati Jumala ja ta trooni juurde.
6Huyo mama akakimbilia jangwani, ambako Mungu alikuwa amemtayarishia mahali pa usalama ambapo angehifadhiwa kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini.
6Ja naine põgenes kõrbe, kus tal oli ase, mille Jumal oli valmistanud, et teda seal toidetaks tuhat kakssada kuuskümmend päeva.
7Kisha kukazuka vita mbinguni: Mikaeli na malaika wake walipigana na hilo joka, nalo likawashambulia pamoja na malaika wake.
7Ja taevas tõusis sõda: Miikael ja tema inglid hakkasid sõdima lohega, ning lohe sõdis ja tema inglid.
8Lakini joka hilo halikuweza kuwashinda, na hatimaye hapakuwa tena na nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika wake.
8Lohe ei saanud võimust, ja enam ei leidunud neile aset taevas.
9Basi, joka hilo kuu likatupwa nje. Joka hilo ndiye yule nyoka wa kale ambaye huitwa pia Ibilisi au Shetani. Ndiye anayeudanganya ulimwengu wote. Naam, alitupwa duniani, na malaika wake wote pamoja naye.
9Suur lohe heideti välja, see muistne madu, keda hüütakse Kuradiks ja Saatanaks, kes eksitab kogu ilmamaad - ta heideti maa peale ja tema inglid heideti koos temaga.
10Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikisema: "Sasa ukombozi utokao kwa Mungu umefika! Nguvu na Utawala wa Mungu wetu umedhihirika. Na Kristo wake ameonyesha mamlaka yake! Maana yule mdhalimu wa ndugu zetu, aliyesimama mbele ya Mungu akiwashtaki usiku na mchana, sasa ametupwa nje.
10Ja ma kuulsin suurt häält taevast hüüdvat: 'Nüüd on käes pääste ja vägi ning meie Jumala kuningriik ning tema Kristuse meelevald, sest välja on heidetud meie vendade süüdistaja, kes süüdistab neid Jumala ees päeval ja ööl.
11Ndugu zetu wameshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa nguvu ya ukweli walioutangaza; maana hawakuyathamini maisha yao kuwa kitu sana, wakawa tayari kufa.
11Nemad on ta ära võitnud Talle vere läbi ning oma tunnistuse sõna läbi ega ole oma elu armastanud surmani.
12Kwa sababu hiyo, furahini enyi mbingu na vyote vilivyomo ndani yenu. Lakini, ole wenu nchi na bahari, maana Ibilisi amewajieni akiwa na ghadhabu kuu, kwa sababu anajua kwamba siku zake zilizobakia ni chache."
12Seepärast rõõmustage, taevad, ning teie, kes neis viibite! Häda maale ja merele, sest kurat on tulnud alla teie juurde; ta on suures raevus, teades, et tal on aega üürikeseks.'
13Joka lilipotambua kwamba limetupwa chini duniani, likaanza kumwinda yule mama aliyekuwa amejifungua mtoto wa kiume.
13Kui lohe nägi, et ta oli heidetud maa peale, siis ta kiusas taga naist, kes oli toonud ilmale poeglapse.
14Lakini mama huyo akapewa mabawa mawili ya tai apate kuruka mbali sana na hilo joka, mpaka mahali, pake jangwani ambapo angehifadhiwa salama kwa muda wa miaka mitatu na nusu.
14Aga naisele anti kaks suure kotka tiiba, et ta lendaks kõrbesse paika, kus teda toidetakse üks aeg ja kaks aega ja pool aega, eemal mao palge eest.
15Basi, joka likatapika maji mengi kama mto, yakamfuata huyo mama nyuma ili yamchukue.
15Ja madu purskas oma suust naisele järele vett otsekui jõe, et teda jõevooluga ära uhtuda.
16Lakini nchi ikamsaidia huyo mama: ikajifunua kama mdomo na kuyameza maji hayo yaliyotoka kinywani mwa hilo joka.
16Maa aitas naist, avades oma suu ning neelates ära jõe, mille lohe purskas välja oma suust.
17Basi, joka hilo likamkasirikia huyo mama, likajiondokea, likaenda kupigana na wazawa wengine wa huyo mama, yaani wote wanaotii amri za Mungu na kuuzingatia ukweli wa Yesu.
17Ja lohe vihastas naise peale ja läks sõdima nendega, kes olid jäänud üle naise soost, kes hoiavad tallel Jumala käske ning kellel on Jeesuse tunnistus.
18Ja ta jäi seisma mere liivale.