1Baada ya hayo, nilimwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa na uwezo mkuu, na dunia ikamulikwa na mng'ao wake.
1Pärast seda nägin ma veel teist inglit, kellel oli suur meelevald, tulevat taevast alla, ning maailm läks valgeks tema hiilgusest.
2Basi, akapaaza sauti kwa nguvu akisema, "Umeanguka; Babuloni mkuu umeanguka! Sasa umekuwa makao ya mashetani na pepo wachafu; umekuwa makao ya ndege wachafu na wa kuchukiza mno.
2Ta hüüdis võimsa häälega: 'Langenud, langenud on suur Paabel ning on saanud kurjade vaimude eluasemeks ning kõigi rüvedate vaimude varjupaigaks ja kõigi rüvedate lindude varjupaigaks ning kõigi rüvedate loomade ja vihatute varjupaigaks!
3Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo."
3Sest tema hooruse raevuviinast on joonud kõik paganad ning temaga on hooranud maailma kuningad ning ilmamaa kaupmehed on rikastunud tema toretsemisest!'
4Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema, "Watu wangu, ondokeni kwake, ili msishirikiane naye katika dhambi zake, msije mkaipata adhabu yake.
4Ja ma kuulsin teist häält taevast hüüdvat: 'Tulge temast välja, mu rahvas, et te ei saaks tema pattude osaliseks ning et te ei kannaks midagi tema nuhtlustest!
5Kwa maana dhambi zake zimekuwa nyingi mno, zimelundikana mpaka mbinguni, na Mungu ameyakumbuka maovu yake.
5Sest tema patud on ulatunud taevani ning Jumalale on tulnud meelde tema ülekohtused teod.
6Mtendeeni kama alivyowatendea ninyi; mlipeni mara mbili kwa yale aliyoyatenda. Jazeni kikombe chake kwa kinywaji kikali mara mbili zaidi ya kile alichowapeni.
6Makske temale kätte, nõnda nagu tema on kätte maksnud, ning tasuge temale kahevõrra tema tegude järgi; karikasse, mille ta on valanud täis, valage talle kahevõrra,
7Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake, na kuishi kwake kwa anasa. Maana anajisemea moyoni: Ninaketi hapa; mimi ni malkia. Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!
7niipalju kui tema on iseennast ülistanud ja toretsenud, niisama palju andke temale piina ja leina! Tema ütleb oma südames: Ma istun kuningannana ega ole lesk ja ei saa iialgi näha leina.
8Kwa sababu hiyo mabaa yake yatampata kwa siku moja: ugonjwa, huzuni na njaa. Atachomwa moto, maana Bwana Mungu mwenye kumhukumu ni Mwenye Uwezo."
8Seepärast tulevad ühel päeval talle nuhtlused: surm ja lein ja nälg, ning ta põletatakse ära tulega, sest võimas on Issand Jumal, kes on mõistnud kohut tema üle.
9Wafalme wa Dunia waliofanya uzinzi naye na kuishi naye maisha ya anasa wataomboleza na kulia wakati watakapoona moshi wa mji huo unaoteketea.
9Tema pärast hakkavad nutma ja halisema ilmamaa kuningad, kes temaga on hooranud ja toretsenud, kui nad näevad tema põlemise suitsu,
10Wanasimama kwa mbali kwa sababu ya kuogopa mateso yake, na kusema, "Ole! Ole kwako Babuloni, mji maarufu na wenye nguvu! Kwa muda wa saa moja tu adhabu yako imekupata."
10seistes kartusest tema piina ees kaugel eemal ja hüüdes: 'Häda, häda, suur linn, Paabel, võimas linn, sest üheainsa tunniga on tulnud su kohtumõistmine!'
11Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumfanyia matanga, maana hakuna mtu anayenunua tena bidhaa zao;
11Ja ilmamaa kaupmehed nutavad ja leinavad tema pärast, sest keegi ei osta kunagi enam nende kaupa:
12hakuna tena wa kununua dhahabu yao, fedha, mawe ya thamani na lulu, kitani na nguo za rangi ya zambarau, hariri na nguo nyekundu; vyombo vya kila aina ya miti ya pekee, vyombo vya pembe za ndovu, vya miti ya thamani kubwa, vya shaba, chuma na marmari;
12ei kulda ega hõbedat, ei kalliskive ega pärleid, ei peenlinast ega purpurit, ei siidi ega erepunast riiet, ei mingisugust healõhnalist puud ega mingisugust elevandiluust eset, ei mingisugust väärispuust tehtud või vasest või rauast või marmorist eset,
13mdalasini, viungo, ubani, manemane, udi, divai, mafuta, unga na ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari ya kukokotwa, watumwa wao na hata maisha ya watu.
13ei kaneeli ega kardemoni, ei suitsutusrohte, mürri ega viirukit, ei veini ega õli, ei püülijahu ega nisu, ei veiseid ega lambaid, ei hobuseid ega tõldu, ei orje ega inimhingi.
14Wafanyabiashara wanamwambia: "Faida yote uliyotazamia imetoweka, na utajiri na fahari vimekuponyoka; hutaweza kuvipata tena!"
14Puuviljad, mida su hing himustas, on su käest kadunud ning kõik, mis särav ja läikiv, on su käest läinud kaotsi ning neid ei leita enam.
15Wafanya biashara waliotajirika kutokana na mji huo, watasimama mbali kwa sababu ya hofu ya mateso yake, watalalamika na kuomboleza,
15Nende asjadega kauplejad, kes on rikastunud selle linna varal, seisavad kartusest tema piina ees kaugel eemal, nuttes ja leinates:
16wakisema, "Ole! Ole kwa mji huu mkuu. Ulizoea kuvalia nguo za kitani, za rangi ya zambarau na nyekundu, na kujipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu!
16'Häda, häda, suur linn, riietatud peenlinasesse ja purpurisse ja erepunasesse ning ehitud kulla ja kalliskivide ja pärlitega, sest üheainsa tunniga on ära rüüstatud nii suur rikkus!'
17Kwa saa moja tu utajiri wako umetoweka!" Halafu manahodha wote na wasafiri wao, wanamaji na wote wanaofanya kazi baharini, walisimama kwa mbali,
17Kõik tüürimehed ja laevnikud ja kõik meremehed ja kõik, kes merel sõidavad, seisid kaugel eemal
18na walipouona moshi wa moto ule uliouteketeza, wakalia kwa sauti: "Hakujapata kuwako mji kama mji huu mkuu!"
18ja kisendasid, kui nad nägid ta põlemise suitsu: 'Kes on selle suure linna sarnane?'
19Wakajimwagia vumbi juu ya vichwa vyao wakilia kwa sauti na kuomboleza: "Ole! Ole kwako mji mkuu! Ni mji ambamo wote wenye meli zisafirizo baharini walitajirika kutokana na utajiri wake. Kwa muda wa saa moja tu umepoteza kila kitu!"
19Nad puistasid põrmu oma pea peale ning kisendasid nuttes ja leinates: 'Häda, häda, suur linn, kus on rikastunud kõik, kellel oli laevu merel - üheainsa tunniga on ta rüüstatud!'
20Furahi ee mbingu, kwa sababu ya uharibifu wake. Furahini watu wa Mungu, mitume na manabii! Kwa maana Mungu ameuhukumu kwa sababu ya mambo uliyowatenda ninyi!
20Rõõmusta tema pärast, taevas, ning pühad ja apostlid ja prohvetid, sest Jumal on teie kaebuse mõistnud tema kanda!'
21Kisha malaika mmoja mwenye nguvu sana akainua jiwe mfano wa jiwe kubwa la kusagia, akalitupa baharini akisema, "Ndivyo, Babuloni atakavyotupwa na kupotea kabisa.
21Ja üks võimas ingel tõstis kivi otsekui suure veskikivi ning viskas selle merre, hüüdes: 'Nõnda visatakse suur linn Paabel äkitselt ära ning teda ei leita enam!
22Sauti za vinubi za muziki, sauti za wapiga filimbi na tarumbeta hazitasikika tena ndani yako. Hakuna fundi wa namna yoyote ile atakayepatikana tena ndani yako; wala sauti ya jiwe la kusagia haitasikika tena ndani yako.
22Ja kandlemängijate ja pillimeeste ja vileajajate ja pasunapuhujate häält ei kuulda sinu sees enam ja ühtegi mis tahes käsitöömeistrit ei leita enam sinu seest ning veskikivide mürinat ei kuulda enam sinu sees,
23Mwanga wa taa hautaonekana tena ndani yako; sauti za bwana arusi na bibi arusi hazitasikika tena ndani yako. Wafanyabiashara wako walikuwa wakuu duniani, na kwa uchawi wako mataifa yote yalipotoshwa!"
23ja lambi valgust ei paista sinu sees enam ning peigmehe ja mõrsja häält ei kuulda enam sinu sees. Sest sinu kaupmehed olid ilmamaa ülikud ja sinu nõidusega on eksitatud kõik paganad,
24Mji huo uliadhibiwa kwani humo mlipatikana damu ya manabii, damu ya watu wa Mungu na damu ya watu wote waliouawa duniani.
24ning sinust on leitud prohvetite ja pühade verd ja kõikide verd, kes on tapetud ilmamaal.'