Swahili: New Testament

Estonian

Revelation

17

1Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na bakuli akaja, akaniambia, "Njoo, mimi nitakuonyesha adhabu aliyopewa yule mzinzi mkuu, mji ule uliojengwa juu ya maji mengi.
1Üks seitsmest inglist, neist, kellel oli seitse kaussi, tuli ning rääkis minuga ja ütles: 'Tule, ma näitan sulle selle suure hoora karistamist, kes istub suurte vete ääres,
2Wafalme wa dunia wamefanya uzinzi pamoja naye; na wakazi wa dunia wamelewa divai ya uzinzi wake."
2kellega on hooranud ilmamaa kuningad ning kelle hooruse veinist on joobnud need, kes elavad ilmamaal!'
3Kisha, Roho akanikumba, akaniongoza mpaka jangwani. Huko nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama mwekundu. Mnyama huyo alikuwa ameandikwa kila mahali majina ya makufuru; alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
3Ja ta viis mu vaimus kõrbe.Ja ma nägin naist istuvat erepunase metsalise seljas, kes oli täis jumalateotuse nimesid ja kellel oli seitse pead ja kümme sarve.
4Mwanamke huyo alikuwa amevaa vazi la rangi ya zambarau na nyekundu; alikuwa amejipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu. Mkononi mwake alishika kikombe cha dhahabu ambacho kilikuwa kimejaa machukizo na mambo machafu yanayoonyesha uzinzi wake.
4Naine oli riietatud purpurpunasesse ja erepunasesse ning ehitud kulla ja kalliskivide ja pärlitega, ta käes oli kuldkarikas täis jäledusi ja oma hooruse saasta
5Alikuwa ameandikwa juu ya paji la uso wake jina la fumbo "Babuloni mkuu, mama wa wazinzi na wa mambo yote ya kuchukiza sana duniani."
5ning ta otsaette oli kirjutatud nimi, saladus: Suur Paabel, hoorade ja ilmamaa jäleduste ema!
6Nikamwona huyo mwanamke amelewa damu ya watu wa Mungu, na damu ya watu waliouawa kwa sababu ya kumtangaza Yesu. Nilipomwona nilishangaa mno.
6Ma nägin naise olevat joobnud pühade verest ja Jeesuse tunnistajate verest. Ma imestasin väga teda nähes.
7Lakini malaika akaniambia, "Kwa nini unashangaa? Mimi nitakuambia maana iliyofichika ya mwanamke huyu na mnyama huyo amchukuaye ambaye ana vichwa saba na pembe kumi.
7Ingel ütles mulle: 'Mispärast sa imestad? Mina ütlen sulle saladuse naise ja metsalise kohta, kes teda kannab ja kellel on seitse pead ja kümme sarve.
8Huyo mnyama uliyemwona alikuwa hai hapo awali, lakini sasa amekufa. Hata hivyo, karibu sana atapanda kutoka shimoni kuzimu, lakini ataangamizwa. Wanaoishi duniani watashangaa; naam, watu wote ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangu mwanzo wa ulimwengu, watashangaa kumwona huyo mnyama ambaye hapo awali, aliishi, kisha akafa na sasa anatokea tena!
8Metsaline, keda sa nägid, oli ning teda ei ole enam ning ta tuleb üles sügavikust ja läheb hukatusse. Ja need, kes elavad ilmamaal, kelle nimesid ei ole maailma rajamisest saadik kirjutatud eluraamatusse, imestavad, kui näevad metsalist, kes oli ja keda ei ole enam ning kes tuleb jälle.
9"Hapa panahitaji akili na hekima! Hivyo vichwa saba ni vilima saba, na huyo mwanamke anaketi juu yake. Vichwa hivyo pia ni wafalme saba.
9Siin olgu mõistust, millel on tarkust: need seitse pead on seitse mäge, mille peal istub naine. Ja on seitse kuningat:
10Kati ya hao wafalme saba, watano wamekwisha angamia, mmoja anatawala bado, na yule mwingine bado hajafika; na atakapofika atabaki kwa muda mfupi.
10viis on langenud, üks on praegu, teine ei ole veel tulnud, ning kui ta tuleb, siis ta peab jääma üürikeseks ajaks.
11Huyo mnyama ambaye alikuwa anaishi hapo awali lakini sasa haishi tena ni mfalme wa nane, naye pia ni miongoni mwa hao saba, na anakwenda zake kuharibiwa.
11Ja metsaline, kes oli ja keda enam ei ole, see on kaheksas, ja samas üks neist seitsmest, ja ta läheb hukatusse.
12"Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme ambao bado hawajaanza kutawala. Lakini watapewa mamlaka ya kutawala kwa muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.
12Kümme sarve, mida sa nägid, on kümme kuningat, kes ei ole veel saanud kuningavõimu, kuid nad saavad koos metsalisega meelevalla üheks tunniks, et valitseda kuningatena.
13Shabaha ya hawa kumi ni moja, na watampa yule mnyama nguvu na mamlaka yao yote.
13Nad on üht ja sama meelt, ning nad annavad oma väe ja meelevalla metsalise kätte.
14Watapigana na Mwanakondoo, lakini Mwanakondoo pamoja na wale aliowaita na kuwachagua, ambao ni waaminifu, atawashinda kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme."
14Nad hakkavad sõdima Tallega ja Tall võidab nad ära - sest tema on isandate Issand ja kuningate Kuningas - ja koos temaga võidavad need, kes on kutsutud ja valitud ja ustavad.'
15Malaika akaniambia pia, "Yale maji uliyoyaona pale alipokaa yule mzinzi, ni mataifa, watu wa kila rangi na lugha.
15Ja ta ütles mulle: 'Veed, mida sa nägid seal, kus hoor istub, on rahvad ja rahvahulgad ja paganad ja keeled.
16Pembe zile kumi ulizoziona na yule mnyama watamchukia huyo mzinzi. Watachukua kila kitu alicho nacho na kumwacha uchi; watakula nyama yake na kumteketeza kwa moto.
16Kümme sarve, mida sa nägid, ning metsaline, need hakkavad vihkama hoora ja teevad ta puupaljaks ja võtavad alasti ja söövad ta liha ja põletavad ta ära tulega.
17Maana Mungu ametia mioyoni mwao nia ya kutekeleza shabaha yake, yaani kwa kukubaliana wao kwa wao na kumpa huyo mnyama mamlaka yao ya kutawala, mpaka hapo neno la Mungu litakapotimia.
17Sest Jumal on nende südamesse andnud teha tema nõu järgi ning olla sama meelt ning anda oma kuningavõim metsalise kätte, kuni Jumala sõnad on läinud täide.
18"Na yule mwanamke uliyemwona ndio ule mji mkuu unaowatawala wafalme wa dunia."
18Ja naine, keda sa nägid, on suur linn, kellel on kuningavõim ilmamaa kuningate üle.'