1Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, "Nendeni mkamwage mabakuli hayo saba ya ghadhabu ya Mungu duniani."
1Ma kuulsin valju häält templist hüüdvat seitsmele inglile: 'Minge ja valage Jumala raevu seitse kaussi välja ilmamaa peale!'
2Basi, malaika wa kwanza akaenda akamwaga bakuli lake juu ya nchi. Mara madonda mabaya na ya kuumiza sana yakawapata wote waliokuwa na alama ya yule mnyama, na wale walioiabudu sanamu yake.
2Esimene läks ning valas oma kausi välja maa peale, ning kurje ja tigedaid paiseid lõi inimeste külge, kellel oli metsalise märk ja kes kummardasid tema kuju.
3Kisha malaika wa pili akamwaga bakuli lake baharini. Nayo bahari ikawa damu tupu kama damu ya mtu aliyekufa, na viumbe vyote hai baharini vikafa.
3Teine valas oma kausi välja merre, ning see sai otsekui surnu vereks ning iga elus hing meres suri.
4Malaika wa tatu akamwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, navyo vikageuka damu.
4Kolmas valas oma kausi välja jõgedesse ja veeallikaisse ning need muutusid vereks.
5Nikamsikia malaika msimamizi wa maji akisema, "Ewe mtakatifu, Uliyeko na uliyekuwako! Wewe ni mwenye haki katika hukumu hii uliyotoa.
5Ja ma kuulsin vete inglit hüüdvat: 'Õige oled sina, kes oled ja kes olid ja kes tuled, sina Püha, et sa nõnda oled kohut mõistnud,
6Maana waliimwaga damu ya watu wako na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; wamestahili hivyo!"
6sest nemad on valanud pühade ja prohvetite verd ning verd oled sina andnud neile juua. Nad on seda väärt.'
7Kisha nikasikia sauti madhabahuni ikisema, "Naam, Bwana Mungu Mwenye Uwezo! Hukumu zako ni za kweli na haki!"
7Ja ma kuulsin altarit ütlevat: 'Jah, Issand Jumal, Kõigeväeline, tõelised ja õiged on sinu kohtumõistmised!'
8Kisha malaika wa nne akamwaga bakuli lake juu ya jua. Jua likapewa nguvu ya kuwachoma watu kwa moto wake.
8Neljas valas oma kausi välja päikese peale, ning temale anti kõrvetada inimesi tulega.
9Basi, watu wakaunguzwa vibaya sana; wakamtukana Mungu aliye na uwezo juu ya mabaa hayo makubwa. Lakini hawakuziacha dhambi zao na kumtukuza Mungu.
9Ja suur kuumus kõrvetas inimesi ning inimesed teotasid Jumala nime, kellel on meelevald nende nuhtluste üle, ega parandanud meelt, et teda ülistada.
10Kisha malaika wa tano akamwaga bakuli lake juu ya makao makuu ya yule mnyama. Giza likauvamia utawala wake, watu wakauma ndimi zao kwa sababu za maumivu,
10Viies valas oma kausi välja metsalise trooni peale, ning tema kuningriik mattus pimedusse ning nad närisid oma keelt valu pärast
11wakamtukana Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na madonda yao. Lakini hawakuyaacha matendo yao mabaya.
11ning teotasid taeva Jumalat oma valude ja paisete pärast, ega parandanud meelt oma tegudest.
12Kisha malaika wa sita akamwaga bakuli lake juu ya mto mkubwa uitwao Eufrate. Maji yake yakakauka, na hivyo njia ilitengenezwa kwa ajili ya wafalme wa mashariki.
12Kuues valas oma kausi välja suure Eufrati jõe peale, ning selle vesi kuivas ära, et tee oleks valmis kuningatele päevatõusu poolt.
13Kisha nikaona pepo wabaya watatu walio kama vyura, wakitoka kinywani mwa yule joka, kinywani mwa yule mnyama, na kinywani mwa yule nabii wa uongo.
13Ja ma nägin, et lohe suust ja metsalise suust ja valeprohveti suust tuli välja kolm rüvedat vaimu otsekui konnad.
14Hawa ndio roho za pepo wafanyao miujiza. Ndio wanaokwenda kwa wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita kuu Siku ile ya Mungu Mwenye Uwezo.
14Need ongi need tunnustähti tegevad kurjad vaimud, kes tulevad kogu ilmamaa kuningate juurde neid koguma sõtta Kõigeväelise Jumala suureks päevaks.
15"Sikiliza! Mimi naja kama mwizi! Heri mtu akeshaye na kuvaa nguo zake ili asije akaenda uchi huko na huko mbele ya watu."
15Ennäe, ma tulen kui varas! Õnnis on see, kes valvab ning hoiab oma rõivaid, et ta ei käiks alasti ja et ei nähtaks tema häbi!
16Basi, roho hao wakawakusanya hao wafalme mahali paitwapo kwa Kiebrania Harmagedoni.
16Ja ta kogus nad kokku paika, mida heebrea keeles hüütakse Harmagedoon.
17Kisha malaika wa saba akamwaga bakuli lake hewani. Sauti kubwa ikasikika kutoka kwenye kiti cha enzi, Hekaluni, ikisema, "Mwisho umefika!"
17Seitsmes valas oma kausi välja õhku, ning vali hääl kostis templi seest troonilt: 'See on sündinud!'
18Kukatokea umeme, kelele, ngurumo na tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijapata kutokea tangu Mungu alipomuumba mtu.
18Ja sündis välke ja hääli ja kõuemürinaid ning suur maavärin, millist ei ole olnud sellest ajast, kui inimesed on elanud maa peal. See oli määratu suur maavärin.
19Mji ule mkuu ukapasuliwa sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikateketea. Babuloni, mji mkuu, haukusahauliwa na Mungu. Aliunywesha kikombe cha divai ya ghadhabu yake kuu.
19Ja suur linn jagunes kolmeks osaks ning paganate linnad varisesid kokku. Ja suurt Paabelit tuletati meelde Jumala ees, et Jumal annaks temale oma raevuviina karika.
20Visiwa vyote vikatoweka, nayo milima haikuonekena tena.
20Kõik saared põgenesid ning mägesid ei leidunud enam.
21Mvua ya mawe makubwa yenye uzito wa kama kilo hamsini kila moja, ikawanyeshea watu. Nao wakamtukana Mungu kwa sababu ya mapigo ya mvua hiyo ya mawe. Naam, pigo la mvua hiyo ya mawe lilikuwa kubwa mno.
21Ja suuri raheteri, talendiraskusi, sadas taevast alla inimeste peale, ning inimesed teotasid Jumalat rahenuhtluse pärast, sest see nuhtlus oli väga suur.