1Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa makubwa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo makubwa saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
1Ma nägin taevas veel teist tunnustähte, suurt ja imelist: seitse inglit, kelle käes oli seitse viimset nuhtlust, sest nendes jõudis lõpule Jumala raev.
2Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
2Ja ma nägin otsekui tulega segatud klaasmerd ja neid, kes olid võitnud metsalise ning ta kuju ja ta nime arvu, seisvat klaasmere ääres, Jumala kandled käes.
3Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwanakondoo: "Bwana Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makuu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
3Nad laulsid Jumala sulase Moosese laulu ja Talle laulu: 'Suured ja imelised on sinu teod, Issand Jumal, Kõigeväeline! Õiged ja tõelised on sinu teed, sa paganate kuningas!
4Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yameonekana na wote."
4Kes ei peaks kartma sind, Issand, ning ülistama sinu nime? Sina üksi oled püha, kõik paganad tulevad ning kummardavad sinu ette, sest su õiged seadmised on saanud avalikuks.'
5Baada ya hayo nikaona Hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ionyeshayo kuwapo kwa Mungu.
5Pärast seda ma nägin: tunnistustelgi pühamu avanes taevas
6Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo Hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa, na kanda za dhahabu vifuani mwao.
6ning need seitse inglit, kelle käes oli seitse nuhtlust, tulid templist välja, üll puhas särav linane riie, kuldvöödega vöötatud rinde alt.
7Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele.
7Ja üks neljast olevusest andis seitsmele inglile seitse kuldkaussi, täis selle Jumala raevu, kes elab igavesest ajast igavesti,
8Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya wale malaika saba.
8ning tempel sai täis suitsu Jumala kirkusest ja tema väest ning ükski ei võinud minna templisse enne, kui olid lõpetatud seitsme ingli seitse nuhtlust.