Swahili: New Testament

Estonian

Revelation

14

1Kisha nikaona mlima Sioni, na Mwanakondoo amesimama juu yake; pamoja naye walikuwa watu mia moja arobaini na nne elfu ambao juu ya paji za nyuso zao walikuwa wameandikwa jina la Mwanakondoo na jina la Baba yake.
1Ma nägin, ennäe: Tall seisis Siioni mäel ning koos temaga sada nelikümmend neli tuhat, kelle otsaesisele oli kirjutatud tema nimi ja tema Isa nimi.
2Basi, nikasikia sauti kutoka mbinguni, sauti iliyokuwa kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa. Sauti niliyosikia ilikuwa kama sauti ya wachezaji muziki wakipiga vinubi vyao.
2Ja ma kuulsin häält taevast otsekui suurte vete kohisemist ning nagu suure kõue mürisemist, ning hääl, mida ma kuulsin, oli otsekui kandlemängijate hääl, kes mängivad oma kandleid.
3Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu mia moja arobaini na nne elfu waliokombolewa duniani.
3Nad laulsid uut laulu trooni ees ning nende nelja olevuse ja vanemate ees, ning keegi muu ei suutnud õppida seda laulu kui vaid need sada nelikümmend neli tuhat, kes on ära ostetud ilmamaalt.
4Watu hao ndio wale waliojiweka safi kwa kutoonana kimwili na wanawake, nao ni mabikira. Wao humfuata Mwanakondoo kokote aendako. Wamekombolewa kutoka miongoni mwa binadamu wengine, wakawa wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwanakondoo.
4Need on need, kes ei ole endid rüvetanud naistega, nad on puhtad nagu neitsid. Need on need, kes järgivad Talle, kuhu ta iganes läheb. Need on inimeste seast ostetud esmaanniks Jumalale ja Tallele,
5Hawakupata kamwe kuwa waongo; hawana hatia yoyote.
5ning nende suust ei ole leitud valet, nad on laitmatud.
6Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote.
6Ma nägin teist inglit keset taevast lendavat; sellel oli igavene evangeelium, et kuulutada evangeeliumi neile, kes elavad ilmamaal - kõigile paganahõimudele ja suguharudele ja keeltele ja rahvastele.
7Akasema kwa sauti kubwa, "Mcheni Mungu na kumtukuza! Maana saa imefika ya kutoa hukumu yake. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu na nchi, bahari na chemchemi za maji."
7Ja ta hüüdis suure häälega: 'Kartke Jumalat ning ülistage teda, sest tema kohtumõistmise tund on tulnud, ning kummardage teda, kes on teinud taeva ja maa ja mere ja vete allikad!'
8Malaika wa pili alimfuata huyo wa kwanza akisema, "Ameanguka! Naam, Babuloni mkuu ameanguka! Babuloni ambaye aliwapa mataifa yote wainywe divai yake--divai kali ya uzinzi wake!"
8Veel teine ingel järgnes talle, hüüdes: 'Langenud, langenud on suur Paabel, kes oma hooruse raevuviinaga on jootnud kõiki paganaid!'
9Na malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, "Yeyote anayemwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,
9Veel kolmas ingel järgnes neile, hüüdes suure häälega: 'Kui keegi kummardab metsalist ja tema kuju ning võtab tema märgi oma otsaette või oma käe peale,
10yeye mwenyewe atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchanganywa na maji. Mtu huyo atateseka ndani ya moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele ya Mwanakondoo.
10siis ta saab juua Jumala raevu viina, mis lahjendamata on valatud tema vihakarikasse, ning teda piinatakse tules ja väävlis pühade inglite ees ja Talle ees.
11Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana."
11Ja nende piinasuits tõuseb üles igavesest ajast igavesti; ja neil, kes kummardavad metsalist ja tema kuju, ei ole hingamist päeval ega ööl, ei ühelgi, kes võtab endale ta nime märgi.
12Kutokana na hayo, ni lazima watu wa Mungu, yaani watu wanaotii amri ya Mungu na kumwamini Yesu, wawe na uvumilivu.
12Siin olgu kannatlikkust pühadel, kes hoiavad alal Jumala käske ja Jeesuse usku!'
13Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, "Andika! Heri watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa wameungana na Bwana." Naye Roho asema, "Naam! Watapumzika kutoka taabu zao; maana matunda ya jasho lao yatawafuata."
13Ma kuulsin häält taevast ütlevat: 'Kirjuta: Õndsad on surnud, kes nüüdsest peale surevad Issandas! Jah, Vaim ütleb, et nad võivad hingata oma vaevadest, sest nende teod lähevad nendega kaasa.'
14Kisha nikatazama, na kumbe palikuwapo wingu jeupe hapo. Na juu ya wingu hilo kulikuwa na kiumbe kama mtu. Alikuwa amevaa taji ya dhahabu kichwani, na kushika mundu mkononi mwake.
14Ma nägin, ennäe: valge pilv, ning see, kes istus pilvel, oli Inimese Poja sarnane, tal oli kuldpärg peas ning vahe sirp käes.
15Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni, na kwa sauti kubwa akamwambia yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu, "Tafadhali, tumia mundu wako ukavune mavuno, maana wakati wa mavuno umefika; mavuno ya dunia yameiva."
15Ja üks teine ingel väljus templist, hüüdes suure häälega sellele, kes istus pilvel: 'Hakka tööle oma sirbiga ning lõika, sest lõikustund on tulnud, sest ilmamaa lõikus on juba küps.'
16Basi, yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akautupa mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.
16Ja see, kes pilvel istus, pistis oma sirbi ilmamaa külge ning ilmamaa lõigati paljaks.
17Kisha malaika mwingine akatoka katika Hekalu mbinguni akiwa na mundu wenye makali.
17Üks teine ingel väljus templist taevas ning temalgi oli vahe sirp.
18Kisha malaika mwingine msimamizi wa moto, akatoka madhabahuni akamwambia kwa sauti kubwa yule malaika mwenye mundu wenye makali, "Nawe tia huo mundu wako mkali, ukakate vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva!"
18Ja üks teine ingel, kellel oli meelevald tule üle, tuli altarist, ning hõikas valju häälega sellele, kellel oli vahe sirp: 'Hakka tööle oma vaheda sirbiga ning lõika maha ilmamaa viinapuu kobarad, sest selle marjad on küpsed!'
19Basi, malaika huyo akautupa mundu wake duniani, akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya chombo kikubwa cha kukamulia zabibu, chombo cha ghadhabu ya Mungu.
19Ja ingel pistis oma sirbi ilmamaa külge ning lõikas paljaks ilmamaa viinamäe ning viskas marjad Jumala raevu suurde surutõrde.
20Zabibu zikakamuliwa ndani ya hilo shinikizo lililoko nje ya mji, na damu ikatoka katika shinikizo hilo mtiririko mrefu kiasi cha mita mia tatu na kina chake kiasi cha mita mia mbili.
20Ja surutõrt sõtkuti väljaspool linna ning tõrrest voolas välja verd hobuste valjastest saadik tuhat kuussada vagu maad.