1"Kwa malaika wa kanisa la Sarde andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye na roho saba za Mungu na nyota saba. Nayajua mambo yako yote; najua unajulikana kuwa na uhai kumbe umekufa!
1Ja Sardese koguduse inglile kirjuta: Nõnda ütleb see, kellel on seitse Jumala vaimu ja seitse tähte: Ma tean su tegusid, et sul on nimi, et sa elad. Ometi oled sa surnud.
2Amka! Imarisha chochote chema kilichokubakia kabla nacho hakijatoweka kabisa. Maana, mpaka sasa, sijayaona matendo yako kuwa ni makamilifu mbele ya Mungu wangu.
2Ole valvas ja hoia, mis on veel jäänud; seegi on juba suremas, sest ma ei ole leidnud su tegusid olevat täiuslikud oma Jumala silmis.
3Kumbuka, basi, yale uliyofundishwa na jinsi ulivyoyasikia, uyatii na ubadili nia yako mbaya. Usipokesha nitakujia ghafla kama mwizi, na wala hutaijua saa nitakapokujia.
3Tuleta siis meelde, kuidas sa sõna oled vastu võtnud ja kuulnud, ning hoia seda tallel ja paranda meelt! Kui sa nüüd ei valva, siis ma tulen kui varas ja sa ei saa arugi, mis tunnil ma tulen su peale.
4Lakini wako wachache huko Sarde ambao hawakuyachafua mavazi yao. Hao wanastahili kutembea pamoja nami wakiwa wamevaa mavazi meupe.
4Kuid Sardeses on sul mõned, kes ei ole määrinud oma rõivaid, ning need saavad kõndida koos minuga valgeis rõivais, sest nad on seda väärt.
5"Wale wanaoshinda, watavikwa mavazi meupe kama hao. Nami sitayafuta majina yao kutoka katika kitabu cha uzima; tena nitawakiri kwamba ni wangu mbele ya Baba yangu na mbele ya malaika wake.
5Kes võidab, see riietatakse samamoodi valgete rõivastega. Mina ei kustuta tema nime eluraamatust ning ma tunnistan tema nime oma Isa ees ja Isa inglite ees.
6"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
6Kellel kõrv on, see kuulgu, mida Vaim ütleb kogudustele!
7"Kwa malaika wa kanisa la Filadelfia andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, ambaye anao ule ufunguo wa Daudi, na ambaye hufungua na hakuna mtu awezaye kufungua.
7Ja Filadelfia koguduse inglile kirjuta: Nõnda ütleb Püha, Tõeline, kelle käes on Taaveti võti, kes avab, ja ükski ei lukusta, ning lukustab, ja ükski ei ava:
8Nayajua mambo yako yote! Sasa, nimefungua mbele yako mlango ambao hakuna mtu awezaye kuufunga; najua kwamba ingawa huna nguvu sana, hata hivyo, umezishika amri zangu, umelitii neno langu wala hukulikana jina langu.
8Ma tean su tegusid! Ennäe, ma avasin su ees ukse, mida ükski ei suuda lukustada. Sul on vähe jõudu, kuid sa oled hoidnud tallel mu sõna ega ole salanud mu nime.
9Sikiliza! Nitawapeleka kwako watu wa kundi lake Shetani, watu ambao hujisema kuwa ni Wayahudi, kumbe ni wadanganyifu. Naam, nitawapeleka kwako na kuwafanya wapige magoti mbele yako wapate kujua kwamba kweli nakupenda wewe.
9Ennäe, ma annan saatana sünagoogist mõned, kes nimetavad endid juutideks, kuid ei ole seda, vaid valetavad. Ennäe, ma teen, et nad tulevad ja kummardavad sinu jalge ette ning saavad aru, et mina olen sind armastanud.
10Kwa kuwa wewe umezingatia agizo langu la kuwa na uvumilivu, nami pia nitakutegemeza salama wakati ule wa dhiki inayoujia ulimwengu mzima kuwajaribu wote wanaoishi duniani.
10Et sa oled hoidnud minu ootamise sõna, siis hoian ka mina sind läbikatsumistunni eest, mis on tulemas kogu ilmamaa peale, et katsuda läbi ilmamaal elavaid.
11Naja kwako upesi! Linda, basi, ulicho nacho sasa, ili usije ukanyang'anywa na mtu yeyote taji yako ya ushindi.
11Ma tulen varsti. Pea kinni, mis sul on, et ükski sinu pärga ei võtaks!
12"Wale wanaoshinda nitawafanya wawe minara katika Hekalu la Mungu wangu, na hawatatoka humo kamwe. Pia nitaandika juu yao jina la Mungu wangu na jina la mji wa Mungu wangu, yaani Yerusalemu mpya, mji ambao utashuka kutoka juu mbinguni kwa Mungu wangu. Tena nitaandika juu yao jina langu jipya.
12Kes võidab, selle teen ma sambaks oma Jumala templis ja enam iialgi ei lähe ta sealt välja, ning ma kirjutan tema peale oma Jumala nime ja oma Jumala linna, uue Jeruusalemma nime, mis tuleb maha taevast minu Jumala juurest, ning oma uue nime.
13"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
13Kellel kõrv on, see kuulgu, mida Vaim ütleb kogudustele!
14"Kwa malaika wa kanisa la Laodikea andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aitwaye Amina. Yeye ni shahidi mwaminifu na wa kweli, ambaye ni chanzo cha viumbe vyote alivyoumba Mungu.
14Ja Laodikeia koguduse inglile kirjuta: Nõnda ütleb Aamen, ustav ja tõeline Tunnistaja, Jumala loomise Algus:
15Nayajua mambo yako yote! Najua kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali ungekuwa kimojawapo: baridi au moto.
15Ma tean su tegusid, et sa ei ole külm ega kuum. Oh oleksid sa ometi külm või kuum!
16Basi, kwa kuwa hali yako ni vuguvugu, si baridi wala si moto, nitakutapika!
16Aga nüüd, et sa oled leige ja mitte külm ega kuum, sülitan ma su välja oma suust.
17Wewe unajisema, Mimi ni tajiri; ninajitosheleza, sina haja ya kitu chochote. Kumbe, hujui kwamba wewe ni mnyonge, unahitaji kuhurumiwa, maskini, kipofu tena uko uchi!
17Et sina ütled: Ma olen rikas ja mul on rikkust küllalt ning mul ei ole puudu millestki - ning sa ei teagi, et sa oled vilets ja armetu ja vaene ja pime ja alasti -,
18Nakushauri ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto upate kuwa tajiri kweli. Tena afadhali ununue pia vazi jeupe, uvae na kufunika aibu ya uchi wako. Nunua pia mafuta ukapake machoni pako upate kuona.
18siis ma annan sulle nõu osta minu käest tules proovitud kulda, et sa saaksid rikkaks, ning valgeid rõivaid, et end nendega riietada ja et ei saaks avalikuks sinu alastioleku häbi, ning silmasalvi võida silmi, et sa näeksid.
19Mimi ndiye mwenye kumwonya na kumrudi yeyote ninayempenda. Kwa hiyo kaza moyo, achana na dhambi zako.
19Keda iganes mina armastan, neid kõiki ma noomin ja karistan. Ole siis innukas ja paranda meelt!
20Sikiliza! Mimi nasimama mlangoni na kubisha hodi. Mtu akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia nyumbani kwake na kula chakula pamoja naye, naye atakula pamoja nami.
20Ennäe, ma seisan ukse taga ja koputan. Kui keegi kuuleb mu häält ja avab ukse, siis ma tulen tema juurde sisse ning söön õhtust temaga ja tema minuga.
21"Wale wanaoshinda nitawaketisha pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi mwenyewe nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
21Kes võidab, sellel ma lasen istuda koos minuga mu troonile, nagu minagi olen võitnud ning istunud oma Isaga tema troonile.
22"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!"
22Kellel kõrv on, see kuulgu, mida Vaim ütleb kogudustele!