1"Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
1Efesose koguduse inglile kirjuta: Nõnda ütleb see, kes hoiab seitset tähte oma paremas käes, kes kõnnib seitsme kuldlambijala vahel:
2Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
2Ma tean su tegusid ja vaevanägemist ja kannatlikkust ning et sa ei või sallida kurjasid ning et sa oled läbi katsunud need, kes ütlevad end olevat apostlid, kuid ei ole seda, ning leidnud nad olevat valelikud.
3Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
3Sul on kannatlikkust ning sa oled talunud vaeva minu nime pärast ega ole ära väsinud.
4Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
4Kuid mul on sinu vastu, et sa oled oma esimese armastuse maha jätnud.
5Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
5Tuleta siis meelde, kust sa oled langenud, ja paranda meelt ning tee esimese armastuse tegusid! Muidu ma tulen su juurde ning lükkan su lambijala asemelt, kui sa ei paranda meelt.
6Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
6Seda sa teed siiski õigesti, et vihkad nikolaiitide tegusid, mida vihkan minagi.
7"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
7Kellel kõrv on, see kuulgu, mida Vaim ütleb kogudustele: Võitjale ma annan süüa elupuust, mis on Jumala paradiisis.
8"Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
8Ja Smürna koguduse inglile kirjuta: Nõnda ütleb Esimene ja Viimne, kes oli surnud ning on jälle elavaks saanud:
9Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
9Ma tean su viletsust ja vaesust - kuid sa oled rikas - ning nende teotamist, kes ütlevad end olevat juudid, kuid ei ole seda, vaid on saatana sünagoog.
10Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
10Ära karda seda, mida sul tuleb kannatada! Ennäe, kurat heidab mõned teie seast vangi, et teid läbi katsutaks, ning teil on viletsust kümme päeva. Ole ustav surmani, ja ma annan sulle elupärja!
11"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
11Kellel kõrv on, see kuulgu, mida Vaim ütleb kogudustele: Võitjale ei tee teine surm mingit kahju!
12"Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: "Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
12Ja Pergamoni koguduse inglile kirjuta: Nõnda ütleb see, kelle käes on vahe kaheterane mõõk:
13Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
13Ma tean, kus sa elad - seal, kus on saatana troon. Ja sa pead kinni minu nimest ega ole salanud minu usku ka neil päevil, mil Antipas, mu tunnistaja, minu ustav, tapeti teie juures, seal, kus elab saatan.
14Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
14Kuid mul on pisut sinu vastu: sinu juures on neid, kes peavad kinni Bileami õpetusest, kes õpetas Baalakit panema Iisraeli laste ette püünispaela: sööma ebajumalate ohvreid ning hoorama.
15Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
15Nõndasamuti on sinulgi nikolaiitide õpetusest kinnipidajaid.
16Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
16Paranda siis meelt, muidu ma tulen varsti su juurde ning sõdin nende vastu oma suu mõõgaga.
17"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
17Kellel kõrv on, see kuulgu, mida Vaim ütleb kogudustele: Võitjale ma annan süüa peidetud mannat ning annan talle valge kivikese ning kivikesele kirjutatud uue nime, mida ükski peale saaja ei tea.
18"Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: "Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
18Ja Tüatiira koguduse inglile kirjuta: Nõnda ütleb Jumala Poeg, kelle silmad on nagu tuleleek ning kelle jalad on vasemaagi sarnased:
19Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
19Ma tean sinu tegusid ja armastust ja usku ja teenimist ja su kannatlikkust ning et su viimaseid tegusid on rohkem kui esimesi.
20Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
20Kuid mul on sinu vastu, et sa lased naist Iisebeli, kes nimetab end prohvetiks ja õpetab, eksitada ka minu sulaseid hoorama ja sööma ebajumalate ohvreid.
21Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
21Ma olen talle andnud aega meeleparanduseks, ent tema ei taha parandada meelt oma hoorusest.
22Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
22Ennäe, ma viskan ta tõvevoodisse ning temaga abielu rikkujad suurde viletsusse, kui nad ei paranda meelt ega lõpeta oma tegusid,
23Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
23ja hävitan ta lapsed surmaga, ning kõik kogudused saavad aru, et mina olen see, kes uurib läbi meeled ja südamed, ning annan igaühele teist teie tegusid mööda.
24"Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
24Aga ma ütlen teile, muudele Tüatiiras, kellel ei ole seda õpetust, kes pole ära tundnud saatana sügavikke, nagu nemad ütlevad, - teie peale ma ei pane muud koormat.
25Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
25Pidage vaid kinni sellest, mis teil on, kuni ma tulen!
26"Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
26Kes võidab ja minu tegusid lõpuni hoiab, sellele ma annan meelevalla paganate üle
27Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
27ning ta hoiab neid kui karjane raudsauaga, nii nagu purustatakse saviastjaid,
28Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
28otsekui minagi olen saanud meelevalla oma Isalt, ning ma annan talle koidutähe.
29"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
29Kellel kõrv on, see kuulgu, mida Vaim ütleb kogudustele!