1Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
1Jeesuse Kristuse ilmutus, mille Jumal temale on andnud, et ta näitaks oma sulastele, mis peatselt peab sündima. Ta näitas seda, läkitades oma ingli oma sulase Johannese juurde,
2naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
2kes on tunnistanud Jumala sõna ning Jeesuse Kristuse tunnistust, kõike, mida ta on näinud.
3Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
3Õnnis on see, kes loeb, ning need, kes kuulavad neid ennustuse sõnu ja hoiavad tallel, mis sellesse on kirjutatud, sest aeg on lähedal.
4Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
4Johannes - seitsmele Aasia kogudusele: Armu teile ja rahu temalt, kes on ja kes oli ja kes tuleb, ning seitsmelt vaimult, kes on tema trooni ees,
5na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
5ning Jeesuselt Kristuselt, kes on ustav tunnistaja, esikpoeg surnuist ja maa kuningate valitseja. Temale, kes meid armastab ning on meid lunastanud meie pattudest oma verega
6akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina.
6ning kes meid on teinud kuningriigiks, preestreiks Jumalale ja oma Isale - temale olgu kirkus ja võimus igavesest ajast igavesti! Aamen.
7Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
7Ennäe, ta tuleb pilvedega ja iga silm saab teda näha, ka need, kes tema on läbi torganud, ning kõik maa suguharud halisevad tema pärast. Jah, aamen.
8"Mimi ni Alfa na Omega," asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
8'Mina olen A ja O,' ütleb Issand Jumal, 'kes on ja kes oli ja kes tuleb, Kõigeväeline.'
9Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
9Mina, Johannes, teie vend ja kaasosaline viletsuses ja kuningriigis ja kannatlikkuses Jeesuses, olin saarel, mida hüütakse Patmoseks, Jumala sõna ja Jeesuse tunnistamise pärast.
10Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
10Ma olin vaimus Issanda päeval ning kuulsin enese taga valju häält, otsekui pasunast,
11Nayo ilisema, "Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea."
11mis ütles: 'Mida sa näed, kirjuta raamatusse ning saada neile seitsmele kogudusele: Efesosse ja Smürnasse ja Pergamoni ja Tüatiirasse ja Sardesesse ja Filadelfiasse ja Laodikeiasse.'
12Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
12Ma pöördusin ümber vaatama seda häält, kes rääkis minuga. Ja kui ma olin pöördunud, siis ma nägin seitset kuldlambijalga
13na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
13ning lambijalgade keskel kedagi, kes oli Inimese Poja sarnane ja kellel oli üll pikk kuub, vöötatud rinde alt kuldvööga.
14Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
14Aga tema pea ja juuksed olid valged nagu valge vill, nagu lumi, ning tema silmad nagu tuleleek,
15miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
15ning tema jalad olid vasemaagi sarnased, kui see on hõõguvas ahjus, ning tema hääl oli otsekui suurte vete kohin.
16Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
16Tal oli paremas käes seitse taevatähte ning tema suust välkus vahe kaheterane mõõk ning tema palged olid otsekui päike, kui see paistab oma väes.
17Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, "Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
17Kui ma teda nägin, langesin ma tema jalge ette nagu surnu. Ning tema pani oma parema käe mu peale ja ütles: 'Ära karda! Mina olen Esimene ja Viimne
18Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu.
18ja Elav. Ma olin surnud, ning ennäe, ma elan igavesest ajast igavesti ning minu käes on surma ja surmavalla võtmed.
19Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
19Kirjuta siis, mida sa oled näinud ja mis on ning mis sünnib pärast seda!
20Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.
20Nende seitsme taevatähe saladus, mida sa näed mu paremas käes, ja nende seitsme kuldlambijala saladus on see: seitse tähte on seitsme koguduse inglid ja seitse lambijalga on seitse kogudust.