1Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo.
1Juudas, Jeesuse Kristuse sulane, Jaakobuse vend - Jumalas Isas armastatud ja Jeesuses Kristuses hoitud kutsutuile:
2Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.
2Halastust teile ning rahu ja armastust saagu rohkesti!
3Ndugu wapenzi, wakati nimo katika jitihada ya kuwaandikieni juu ya ule wokovu tunaoshiriki sote, nimeona lazima ya kuwaandikieni na kuwahimizeni mwendelee kupigana kwa ajili ya imani ambayo Mungu amewajalia watu wake mara moja tu kwa wakati wote.
3Armsad, ma olen igati püüdnud teile kirjutada meie ühisest päästest, ja nüüd muutuski möödapääsmatuks kirjutada teile, et ergutada teid võitlema pühadele kord antud usu pärast.
4Maana watu wasiomcha Mungu wamepata kujiingiza kwa siri miongoni mwetu, watu ambao, kwa faida ya maisha yao mabaya, wanaupotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu na kumkana Yesu Kristo aliye peke yake kiongozi na Bwana wetu. Maandiko Matakatifu yalikwisha bashiri tangu awali hukumu inayowangojea watu hao.
4Sest teie hulka on end poetanud mõningad inimesed, kes juba muiste on ette kirja pandud selleks kohtuks: jumalakartmatud, kes meie Jumala armu kõlvatuseks pöörates salgavad ära ka ainsa Valitseja ja meie Issanda, Jeesuse Kristuse.
5Nataka kuwakumbusheni mambo fulani ambayo mmekwisha yajua: kumbukeni jinsi Bwana alivyowaokoa watu wa Israeli na kuwatoa katika nchi ya Misri, lakini baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
5Aga ma tahan meenutada teile, kes te seda kõike küll juba teate, et Issand, kui ta kord oli päästnud rahva Egiptusemaalt, teisel korral hukkas uskmatud,
6Na, malaika ambao hawakuridhika na cheo chao, wakayaacha makao yao ya asili, Mungu amewafunga gizani kwa minyororo ya milele wahukumiwe Siku ile kuu.
6ning et ta ingleidki, kes ei hoidnud kinni oma päritolust, vaid hülgasid oma eluaseme, säilitab pilkase pimeduse all jäädavais ahelais suure päeva kohtuni.
7Kumbukeni pia Sodoma na Gomora, na miji ya kandokando yake; wenyeji wake walifanya kama wale malaika; walifanya uzinzi na mambo yaliyo kinyume cha maumbile, wakapewa hukumu ya moto wa milele, iwe onyo kwa watu wote.
7Nii nagu ka Soodoma ja Gomorra ja nende ümberkaudsed linnad, kes samal kombel hoorasid nagu need inglid ning jooksid ebaloomulike himude järgi, seisavad juba hoiatuseks igavese tule karistuse kandjatena.
8Hivyo ndivyo pia walivyo watu hawa. ndoto zao huwaongoza katika kuichafua miili yao wenyewe, kuyadharau mamlaka ya Mungu na kuvitukana viumbe vitukufu vya huko juu.
8Otse nõndasamuti ju pilastavad ka need unenägijad ihu, lükkavad kõrvale Issanda valitsuse ja teotavad kirkuseingleid.
9Hata Mikaeli, malaika mkuu, hakufanya hivyo. Katika ule ubishi kati yake na Ibilisi waliobishana juu ya mwili wa Mose, Mikaeli hakuthubutu kumhukumu Ibilisi kwa matusi; ila alisema: "Bwana mwenyewe na akukaripie."
9Aga peaingel Miikael, kui ta riidles ja vaidles kuradiga Moosese keha pärast, ei julgenud lausuda teotavat otsust, vaid ütles: 'Issand sõidelgu sind!'
10Lakini watu hawa hutukana chochote wasichokielewa; mambo yaleyale wanayoyajua kwa silika kama vile wanyama wanayoyajua ndiyo yanayowaangamiza.
10Kuid need teotavad ju kõike, mida nad ei tunne. Millest nad aga loomu poolest nagu mõistuseta loomad aru saavad, selles nad hukutavad end.
11Ole wao! Watu hao wamefuata mwenendo uleule wa Kaini. Kwa ajili ya fedha, wamejiingiza katika mkosi uleule wa Baalamu. Wameasi kama Kora alivyoasi na wameangamizwa kama yeye alivyoangamizwa.
11Häda neile, sest nad on läinud Kaini teed ja andunud tasu eest Bileami eksitusele ning Korahi kombel vastuhakkamise läbi hukkunud!
12Kwa makelele yao yasiyo na adabu, watu hao ni kama madoa machafu katika mikutano yenu ya karamu ya Bwana. Hujipendelea wao wenyewe tu, na wako kama mawingu yanayopeperushwa huko na huko na upepo bila ya kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa majira yake, wamekufa kabisa.
12Nemad on need teie armastussöömaaegade mustuseplekid, kes kartmatult teiega koos pidutsedes iseennast nuumavad. Nad on tuulte aetavad veeta pilved, hilissügisesed viljatud puud, ülesjuuritult kahekordselt surnud,
13Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanaonekana dhahiri kama vile mapovu ya mawimbi. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, ambao Mungu amewawekea mahali pao milele katika giza kuu.
13oma häbi välja vahutavad metsikud merelained, ekslevad tähed, kelle jaoks on hoitud pilkane pimedus igavesti.
14Henoki, ambaye ni babu wa saba tangu Adamu, alibashiri hivi juu ya watu hawa: "Sikilizeni! Bwana atakuja pamoja na maelfu ya malaika wake watakatifu
14Aga nende kohta on ka Eenok, seitsmes Aadamast, ennustanud: 'Vaata, Issand tuleb mitmekümne tuhande pühaga
15kutoa hukumu juu ya binadamu wote, kuwahukumu wote kwa ajili ya matendo yao yote maovu waliyotenda na kwa ajili ya maneno yote mabaya ambayo watu waovu walimkashifu nayo."
15pidama kohut kõigi üle ja karistama iga hinge kõikide nende jumalakartmatute tegude eest, mis nad jumalakartmatult on teinud, ja kõikide kalkide sõnade eest, mida jumalakartmatud patused on tema vastu rääkinud.'
16Watu hawa wananung'unika daima na kuwalaumu watu wengine. Hufuata tamaa zao mbaya, hujigamba na kuwasifu watu wengine mno kusudi wafaulu katika mipango yao.
16Need on nurisevad saatusekirujad, oma himude järgi käijad, kelle suu räägib õõnsaid sõnu, ja nad lipitsevad inimeste ees kasu pärast.
17Lakini ninyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali ni mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo.
17Teie aga, armsad, meenutage meie Issanda Jeesuse Kristuse apostlite sõnu, mida nad juba enne on rääkinud.
18Waliwaambieni: "Siku za mwisho zitakapofika, watatokea watu watakaowadhihaki ninyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya."
18Sest nad ütlesid teile, et viimsel ajal tuleb oma jumalakartmatute himude järgi käivaid pilkajaid.
19Hao ndio watu wanaosababisha mafarakano, watu wanaotawaliwa na tamaa zao za kidunia, watu wasio na Roho wa Mungu.
19Need on lõhede tekitajad, maised, kellel ei ole Vaimu.
20Lakini ninyi, wapenzi wangu, endeleeni kujijenga kikamilifu katika imani yenu takatifu. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu,
20Teie aga, armsad, olles rajanud endid oma kõige pühamale usule ja palvetades Pühas Vaimus,
21na kubaki katika upendo wa Mungu, mkiwa mnamngojea Bwana wetu Yesu Kristo awapeni uzima wa milele kwa huruma yake.
21hoidke endid Jumala armastuses, oodates meie Issanda Jeesuse Kristuse halastust igaveseks eluks.
22Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka;
22Ja halastage nende peale, kes kahtlevad,
23waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni; na kwa wengine muwe na huruma pamoja na hofu, lakini chukieni hata mavazi yao ambayo yamechafuliwa na tamaa zao mbaya.
23päästke neid tulest välja kiskudes. Teiste peale halastage aga kartuses, vihates lihaliku loomuse poolt rüvetatud rüüdki.
24Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta ninyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake,
24Temale, kes suudab teid hoida komistamast ja panna laitmatuna oma kirkuse palge ette hõiskama,
25kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina.
25ainsale Jumalale, meie Päästjale, olgu Jeesuse Kristuse, meie Issanda läbi kirkus, üllus, võimus ja meelevald enne kõiki aegu ja nüüd ja kõigi aegadeni! Aamen.