Swahili: New Testament

Estonian

3 John

1

1Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
1Vanem - armsale Gaiusele, keda ma armastan tões.
2Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
2Armas, soovin sulle, et sul läheks igati hästi ja sa oleksid terve, nõnda nagu läheb hästi su hingel.
3Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
3Ma ju rõõmustasin väga, kui vennad tulid ja andsid tunnistust sinu elamisest tões, nii nagu sa käidki tões.
4Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
4Mul pole millestki suuremat rõõmu, kui kuulda oma lapsi käivat tões.
5Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
5Armas, sa oled ustav olnud selles, mida sa oled iganes teinud vendadele, koguni neile, kes on sulle võõrad.
6Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
6Nad on tunnistanud sinu armastusest siinse koguduse ees. Sa teed hästi, kui sa läkitad nad edasi väärikal viisil Jumala ees.
7Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
7Nad on teele läinud tema nime pärast ega võta midagi vastu paganatelt.
8Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
8Seepärast me oleme kohustatud nendesuguseid vastu võtma, et saaksime tõe kaastöölisteks.
9Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
9Ma kirjutasin mõne sõna kogudusele, aga Diotrefes, kes püüab olla nende seas esimene, ei võta meid vastu.
10Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
10Seepärast, kui ma tulen, siis ma tuletan talle meelde teod, mida ta teeb, laimates meid kurjade sõnadega ja rahule jäämata sellega, et ta ise ei võta vastu vendi, takistab veel neidki, kes tahavad seda teha, ning heidab nad kogudusest välja.
11Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
11Armas, ära võta eeskujuks paha, vaid head! Kes teeb head, on Jumalast, kes teeb paha, ei ole Jumalat näinud.
12Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
12Demeetriosele on antud tunnistus kõigilt ja tõelt eneselt; ning meiegi tunnistame, ja sina tead, et meie tunnistus on tõsi.
13Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
13Mul oleks sulle palju kirjutada, kuid ma ei taha sulle kirjutada tindi ja sulega.
14Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. (G1-15) Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.
14Aga ma loodan sind peatselt näha ja siis räägime silmast silma.
15Rahu sulle! Sind tervitavad sõbrad. Tervita sõpru nimepidi!