Swahili: New Testament

Estonian

Revelation

5

1Kisha katika mkono wa kulia wa huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, nikaona kitabu; nacho kilikuwa kimeandikwa ndani na nje na kufungwa na mihuri saba.
1Ja ma nägin troonil istuja paremas käes rullraamatut, täis kirjutatud seest ja väljast, kinni pandud seitsme pitseriga.
2Tena nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: "Nani anayestahili kuvunja hiyo mihuri na kukifungua kitabu hicho?"
2Ma nägin võimsat inglit, kes suure häälega kuulutas: 'Kes on väärt avama seda raamatut ja lahti tegema selle pitsereid?'
3Lakini hakupatikana mtu yeyote mbinguni, wala duniani, wala chini Kuzimu, aliyeweza kukifungua hicho kitabu au kukitazama ndani.
3Ning mitte ükski taevas ega maa peal ega maa all ei suutnud avada raamatut ega vaadata sinna sisse.
4Basi, mimi nikalia sana kwa sababu hakupatikana mtu aliyestahili kukifungua, au kukitazama ndani.
4Ma nutsin kibedasti, et kedagi ei leitud väärt olevat avama seda raamatut ning vaatama sinna sisse.
5Kisha mmoja wa wale wazee akaniambia, "Usilie! Tazama! Simba wa kabila la Yuda, mjukuu maarufu wa Daudi, ameshinda. Yeye anaweza kuivunja mihuri yake saba na kukifungua hicho kitabu."
5Siis üks vanemaist ütles mulle: 'Ära nuta! Ennäe, lõvi Juuda suguharust, Taaveti juur, tema on võitnud, tema võib avada raamatu ja selle seitse pitserit!'
6Kisha nikaona pale katikati ya kiti cha enzi Mwana kondoo amesimama, akizungukwa kila upande na vile viumbe hai vinne, na wale wazee. Huyo Mwanakondoo alionekana kana kwamba amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba ambayo ni roho saba za Mungu zilizokuwa zimepelekwa kila mahali duniani.
6Ja ma nägin trooni ja nelja olevuse ja vanemate keskel seismas Talle, kes oli otsekui tapetud ning kellel oli seitse sarve ja seitse silma - need on seitse Jumala vaimu, kes on läkitatud kogu ilmamaale.
7Mwanakondoo akaenda, akakitwaa hicho kitabu kutoka mkono wa kulia wa yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi.
7Ja ta tuli ning võttis raamatu troonil istuja paremast käest.
8Mara tu alipokwisha twaa hicho kitabu, vile viumbe hai vinne pamoja na wale wazee ishirini na wanne walianguka kifudifudi mbele ya Mwanakondoo. Kila mmoja, alikuwa na kinubi na bakuli za dhahabu zilizojaa ubani, ambao ni sala za watu wa Mungu.
8Kui ta oli võtnud raamatu, siis need olevused ja need kakskümmend neli vanemat heitsid maha Talle ette, igaühel oli käes kannel ja kuldkausid täis suitsutusrohte - need on pühade palved.
9Basi, wakaimba wimbo huu mpya: "Wewe unastahili kukitwaa hicho kitabu na kuivunja mihuri yake. Kwa sababu wewe umechinjwa, na kwa damu yako umemnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila, lugha, jamaa na taifa.
9Ning nad laulsid uut laulu: 'Sina oled väärt võtma raamatu ning avama selle pitserid, sest sina olid tapetud ning sina oled ostnud Jumalale oma verega inimesi kõigist suguharudest ja keeltest ja rahvastest ja paganahõimudest
10Wewe umewafanya wawe ufalme wa makuhani wamtumikie Mungu wetu nao watatawala duniani."
10ning oled nad teinud kuningriigiks ja preestreiks meie Jumalale ning nad hakkavad valitsema kuningatena üle ilmamaa.'
11Kisha nikatazama, nikasikia sauti ya malaika wengi sana, idadi isiyohesabika, maelfu na maelfu. Walikuwa wamekaa kuzunguka kiti cha enzi, vile viumbe hai vinne na wale wazee;
11Ja ma nägin ja kuulsin paljude inglite häält trooni ja olevuste ja vanemate ümber, ning nende arv oli kümme tuhat korda kümme tuhat ja tuhat korda tuhat.
12wakasema kwa sauti kuu: "Mwanakondoo aliyechinjwa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, utukufu na sifa."
12Nad hüüdsid valju häälega: 'Tall, kes on tapetud, on väärt võtma väge ja rikkust ja tarkust ja võimu ja au ja kirkust ja õnnistust!'
13Nikasikia viumbe vyote mbinguni, duniani, chini kuzimuni na baharini--viumbe vyote ulimwenguni--vikisema: "Kwake yeye aketiye katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo, iwe sifa na heshima na utukufu na enzi milele na milele."
13Ja kõike loodut taevas ja maa peal ja maa all ja meres ning kõike, mis on nendes, kuulsin ma hüüdvat: 'Sellele, kes istub troonil, ja Tallele - õnnistus ja au ja kirkus ja võimus olgu igavesest ajast igavesti!'
14Na vile viumbe vinne hai vikasema, "Amina!" Na wale wazee wakaanguka kifudifudi, wakaabudu.
14Ja need neli olevust ütlesid: 'Aamen.' Ning vanemad heitsid maha ja kummardasid.