1Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisarea aitwaye Kornelio, Jemadari wa kikosi kimoja kiitwacho "Kikosi cha Italia."
1Huan, Kaisaria khua ah mi khat a min Kornelia a om a; Itali pawl a chih uh, huai pawla sepaih zaheutupa ahi a,
2Alikuwa mtu mwema; naye pamoja na jamaa yake yote walimcha Mungu; alikuwa anafanya mengi kusaidia maskini wa Kiyahudi na alikuwa anasali daima.
2Pathian limsakmi ahi a, a inkuanpihte tengteng toh Pathian laudan a siam uhi, mite kiangah thil tampi a pe jela, Pathian kiangah leng a thum gige hi.
3Yapata saa tisa mchana, aliona dhahiri katika maono malaika wa Mungu akiingia ndani na kumwambia, "Kornelio!"
3Hiai miin sun dak kuana khawng dingin manglam bangin chiantakin Pathian angel khat a kianga luta, Kornelia, chiin, a mu a.
4Kornelio alimkodolea macho huyo malaika kwa hofu, akamwambia, "Kuna nini Mheshimiwa?" Huyo malaika akamwambia, "Mungu amezipokea sala na sadaka zako kwa maskini.
4Huan, Korneliain amah a naen kilkela, a lau a, Toupa, bang ahia? a chi a. Huan, aman, a kiangah, Na thumnate leh na thilpiak thute theih gigena dingin Pathian maah a tungtouta.
5Sasa, watume watu Yopa wakamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
5Tunah Joppa khua ah mi sawl inla, mi khat Simon Peter a chih uh, va pi sak in;
6Yeye yumo nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi ambaye nyumba yake iko karibu na bahari."
6savun bawlpa Simon kiangah a tunga, a in tuipi geiah a om, a chi a.
7Huyo malaika aliyesema hayo alipokwisha kwenda zake, Kornelio aliwaita watumishi wawili wa nyumbani na mmoja wa askari zake ambaye alikuwa mcha Mungu,
7Huan, angel a houpihpa a pai takin, Korneliain a sikhate laka mi nih leh a nek bawl gigete laka Pathian limsak sepaih khat a sam a,
8akawaeleza yote yaliyotukia, akawatuma Yopa.
8huan, thu tengteng a kiang ua a hilh khitin Joppa khua ah a sawlta hi.
9Kesho yake, hao watu watatu wakiwa bado safarini, lakini karibu kufika Yopa, Petro alipanda juu ya paa la nyumba yapata saa sita mchana ili kusali.
9Huan, a jinga a pai lai un, kho kiang a tun kuan un, Peter tuh thum dingin, dak gukna khawngin, in tungah a kahtou a;
10Aliona njaa, akatamani kupata chakula. Chakula kilipokuwa kinatayarishwa, alipatwa na usingizi mzito akaona maono.
10Huan, a gil a hongkiala, annek a utta a; himahleh nekding a bawl lai un mengmu bangin a hongom a.
11Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka kubwa inateremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
11Huan, van kihongin, banghiam bawm, puan liantak bang, a ning lia khiha, lei a luai khiain a mu a.
12Ndani ya shuka hiyo kulikuwa na kila aina ya wanyama: wanyama wenye miguu minne, wanyama watambaao na ndege wa angani.
12Huai sungah leitunga khelinei chi chih leh, gamsa leh, ganhing bokvak, tungleng vasa chi chihte a om ua.
13Akasikia sauti ikimwambia: "Petro, amka uchinje, ule!"
13Huan, a kiangah awin, Peter, thou inla gou inla, ne in, a honchi a.
14Petro akajibu, "La, Bwana; mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu."
14Himahleh, Peterin, Toupa hi lou e; sianglou leh nin bangmah himhim ka ne ngeikei, a chi a.
15Ile sauti ikasikika tena ikimwambia: "Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa!"
15Huan awin, a nihveinain, Pathianin a hihsiangthousa nang sianglou chi ken, a chi a.
16Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.
16Huchi bang ngenin thumvei a hongoma; huan, bawm tuh vana khaitouhin a om nawnta hi.
17Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hilo maono alilokuwa ameliona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,
17Huan, Peterin mengmu banga a muh theisiamlou a, a buai lain, Kornelia mi sawlten Simon in a nakankheta ua.
18Wakaita kwa sauti: "Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?"
18Kongkhak bulah a nading ua, a sam ua, Simon, Peter a chih uh, huaia a tun leh tun louh a nadong uhi.
19Petro alikuwa bado anajaribu kuelewa lile maono, na hapo Roho akamwambia, "Sikiliza! kuna watu watatu hapa, wanakutafuta.
19Huan, Peterin mengmu banga a muh a ngaihtuah lain, Khain a kiangah, Ngai in, mi thumin a hongzong uh.
20Shuka upesi na wala usisite kwenda pamoja nao kwa maana ni mimi niliyewatuma."
20Huchiin, thou inla, kum inla, bangmah ginglel louin amau jui in; amau ka sawl ahi uh, a chi a.
21Basi, Petro akateremka chini, akawaambia hao watu, "Mimi ndiye mnayemtafuta. Kwa nini mmekuja?"
21Huchiin Peter tuh huai mite kiangah a hoh sukta a, a kiang uah, Ngai un na zon uh ka hi; bang ahia na hongna uh? chi a.
22Wao wakamjibu, "Jemadari Kornelio ambaye ni mtu mwema, mcha Mungu na mwenye kuheshimika mbele ya Wayahudi wote ametutuma. Aliambiwa na malaika mtakatifu akualike nyumbani kwake ili asikilize chochote ulicho nacho cha kusema."
22Huan, amau, Angel siangthou khatin, Kornelia sepaih zaheutupa, mi diktak, Pathian laudansiam, Juda nam tengteng laka mi hoih kiangah, na thugen a jakna din, a in ah nangmah sam dingin, a hih hi, a chi ua.
23Petro akawaalika ndani, akawapa mahali pa kulala usiku ule. Kesho yake, Petro alianza safari pamoja nao, na baadhi ya ndugu wa huko Yopa walifuatana naye.
23Huchiin mite tuh a sam luta, a giaksakta hi. Huan, a jingin Peter a thou a, a kiang uah a paia, Joppa khuaa mi unau kuate hiam leng a kiang uah a pai sam uhi.
24Siku ya pili yake, walifika Kaisarea na huko Kornelio alikuwa anawangojea pamoja na jamaa na marafiki aliokuwa amewaalika.
24Huan, a jing nawnin Kaisaria khua ah a lutta ua. Huan, Korneliain, a sanggamte leh a lawm deihpente samkhawmin, amau a na ngak nilouh a.
25Petro alipokuwa anaingia, Kornelio alitoka nje kumlaki, akapiga magoti mbele yake na kuinama chini kabisa.
25Huan, Peter a honglut dek laitakin Korneliain a nadawna, a khebula khupbohin, Pathian chibai buk bangin a buk a.
26Lakini Petro alimwinua, akamwambia, "Simama, kwa maana mimi ni binadamu tu."
26Himahleh, Peterin amah a kaithou a, ding in, kei leng mihing ka hi, a chi a.
27Petro aliendelea kuongea na Kornelio wakiwa wanaingia nyumbani ambamo aliwakuta watu wengi wamekusanyika.
27Huan, a kiangah thu gen kawmin a luta, mi tampi omkhawm a vamu hi.
28Petro akawaambia, "Ninyi wenyewe mnajua kwamba Myahudi yeyote amekatazwa na Sheria yake ya dini kushirikiana na watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amenijulisha nisimfikirie mtu yeyote kuwa najisi au mchafu.
28Huan, a kiang uah, Juda mi nam dang toh kithuah leh pai a sianlouh dan noun a thei ua; himahleh, kuamah sianglou leh nin ka chih ding ahi kei chih Pathianin a hontheisak ahi.
29Kwa sababu hiyo, mliponiita nimekuja bila kusita. Basi, nawaulizeni: kwa nini mmeniita?"
29Huaijiakin na hongsap takin sellouin ka hongpai ahi. Huchiin ka hondong ahi, bangdia honsam na hi ua le? a chi a.
30Kornelio akasema, "Siku tatu zilizopita saa kama hii, saa tisa alasiri, nilikuwa nikisali chumbani mwangu. Ghafla, mtu aliyekuwa amevaa mavazi yenye kun'gaa alisimama mbele yangu,
30Huan, Korneliain, Ni li ahita, tu hun bangtanin, ka in ah, dak kuana hun thumna ah ka thuma; huan, ngai in, puan vaktak silhin mi khat ka maah a hong dinga,
31akasema: Kornelio! Sala yako na sadaka zako kwa maskini vimekubaliwa na Mungu.
31Kornelia, na thumna jakin a omta, mi kianga na thilpiakte leng Pathianin a theigige hi.
32Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petroi; yuko nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi karibu na bahari.
32Huaijiakin, Joppa khua ah mi sawl inla, Simon, Peter a chih uh, na kiangah samin; amah tuh tuipi gei ah savun bawlpa Simon ina tungahi, a chi a.
33Kwa hiyo nilikutumia ujumbe bila kuchelewa, nawe umefanya vyema kuja. Sasa, sisi tuko mbele ya Mungu, kusikiliza chochote ambacho bwana amekuamuru kusema."
33Huaijiakin na kiangah mi ka honsawl pah ahi; na hong a hoih ahi. Huchiin Toupan thu a honpiak peuhmah thei dingin tun ah Pathian mitmuhin i vek un hiaiah i om hi, a chi a.
34Hapo Petro akaanza kusema: "Sasa nimetambua kwamba hakika Mungu hana ubaguzi.
34Huan, Peterin a gena, Pathianin mi deihsak tuam a neikei chih, diktakin ka thei hi;
35Mtu wa taifa lolote anayemcha Mungu na kutenda haki anapokelewa naye.
35ahihhangin, nam chih lakah kuapeuh amah kihtakdansiama, diktaka gamta peuhmah, a pahtak mi ahi naknak uhi.
36Huu ndio ule ujumbe Mungu alioupeleka kwa watu wa Israeli, akitangaza Habari Njema iletayo amani kwa njia ya Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa wote.
36Aman tuh khamuanna Tanchin Hoih Jesu Kris kama genin, Israel suante kiangah thu a khaka (Jesu tuh mi tengteng Toupa ahi a),
37Ninyi mnajua jambo lililotukia katika nchi yote ya Wayahudi kuanzia Galilaya baada ya ule ubatizo aliohubiri Yohane.
37Johanin a tangkou pihpih baptisma nungin, thu, Galili gam akipan a hongthang pana, Judia gam tengteng ah a thangsuaka, noumau leng na thei uhi;
38Mnajua Yesu wa Nazareti na jinsi Mungu alivyomteua kwa kummiminia Roho Mtakatifu na nguvu. Mungu alikuwa pamoja naye; yeye alikwenda huko na huko akitenda mema na kuwaponya wote waliokuwa wamevamiwa na Ibilisi.
38Nazaret Jesu tungtang thu, huchia Pathianin amah Kha Siangthou leh thilhihtheihna a a vuh dan, amah tuh mi tunga hih hoih leh diabol gawt tengteng hihdamin a vialvak vaka, Pathian a kianga a om jiakin.
39Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyotenda katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu. Walimuua kwa kumtundika msalabani;
39Judate gamah leh Jerusalem khua a a thilhih tengteng theihpih te ka hi uhi, amah lah sing dawnah khaiin a hihlumta ua.
40lakini Mungu alimfufua siku ya tatu, akamfanya aonekane
40Pathianin nithum niin a kaithou nawna, chiantakin a kitheisak hi,
41si kwa watu wote ila kwa wale Mungu aliokwisha wachagua wawe mashahidi wake, yaani sisi tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka kwake kutoka wafu.
41ahihhangin mi tengteng kiangah ahi keia, Pathianin theihpih dia a seh kholhte kiang kia ah ahi koute, misi lak akipan a thohnawn nunga a kianga nea dawnte kiangah.
42Alituamuru kuihubiri Habari Njema kwa watu wote na kushuhudia kwamba yeye ndiye aliyeteuliwa na Mungu awe Mwamuzi wa wazima na wafu.
42Amah tuh misi leh mihingte tunga Vaihawmpa dia Pathian seh ahi chih, mi kianga tangkoupih leh theisak dingin Pathianin thu a honpia hi.
43Manabii wote waliongea juu yake kwamba kila mtu atakayemwamini atasamehewa dhambi zake zote kwa jina lake."
43Kuapeuhmah amah gingta tuh a min jiakin khelhnate ngaihdamin a om ding uh chih hiai a tanchin tuh jawlnei tengtengin a natheihsaksak uh ahi, a chi a.
44Wakati Petro alipokuwa bado anasema maneno hayo, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wanasikiliza ujumbe huo.
44Huan, Peterin huai thu a gen laitakin thu zate tengteng tungah Kha Siangthou a hongtungta hi.
45Wale Wayahudi waumini waliokuja pamoja na Petro kutoka Yopa walishangaa kuona kuwa Mungu aliwamiminia zawadi ya Roho Mtakatifu watu wa mataifa mengine pia;
45Huan, Zeksumte laka a gingtate Peter honjui peuhmahin Kha Siangthou piak Jentelte tungah leng buak ahih jiakin lamdang a sa mahmah uhi.
46maana waliwasikia wakiongea kwa lugha mbalimbali wakimtukuza Mungu. Hapo Petro akasema,
46Pau theihlouha thu genin Pathian phatin a za ngal ua.
47"Watu hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi wenyewe tulivyompokea. Je, kuna yeyote atakayeweza kuwazuia wasibatizwe kwa maji?"
47Huan, Peterin a phuanga, hiai mite, eimah banga Kha Siangthou tang sam, baptis nadingin tuizat kuaman a kham thei dia hia? a chi a.Huchiin, Jesu Kris mina baptisma tan ding thu a pia a. Huan khitin ni bangzah hiam tam dingin a khou uh.
48Basi, akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Kisha wakamwomba akae nao kwa siku chache.
48Huchiin, Jesu Kris mina baptisma tan ding thu a pia a. Huan khitin ni bangzah hiam tam dingin a khou uh.