1Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
1Huan, mi khat, Mari leh a sanggam Martha omna khua Bethani mi, Lazar, damlouin om a.
2Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
2Mari thau namtui Toupa nilha a sama a khe nulnu, huai sanggampa Lazar ahi, damlou tuh.
3Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: "Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!"
3Huan, a sanggamnuten Jesu kiang ah, Toupa, ngai dih, na it a china hi, chiin, mi a sawl ua.
4Yesu aliposikia hivyo akasema, "Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe."
4Huan, Jesun huai a jakin, Hiai natna sihna ding jen ahi kei, Pathian thupina ding ahi jaw. Pathian Tapa, hiai jiaka hihthupi a hih theihna dingin, a chi a.
5Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
5Huan, Jesun Martha te, a sanggamnu te, Lazar te a it hi.
6Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
6Huaijiakin a china chih a jakin, a omna ngeiah ni nih a tam lai hi.
7Kisha akawaambia wanafunzi wake, "Twendeni tena Yudea!"
7Huan, huaikhitin a nungjuite kiangah, Judia gamah I hoh nawn ding uh, achia.
8Wanafunzi wakamwambia, "Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?"
8Huan, nungjuiten a kiangah, Rabbi, tuma zekin Judaten suanga honden a tum ua; huchipi in leng huaiah na hoh nawn himhimdia hia? a chi ua.
9Yesu akajibu, "Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
9Huan, Jesun, Sunin dak kal sawm leh nih a om ka hia? Mi suna a vak leh, a hoi ngei keia, hiai khovel vak a muh jiakin.
10Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake."
10Ahihhangin, mi jana a vak leh, a hoi naka; amaha vak a om louh jiakin, a chi a, a dawnga.
11Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, "Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha."
11Huai thute a gen a; huan, huai khitin a kiang uah, I lawmpa Lazar a ihmuta; a ihmu phawng halh dingin ka hoh dek ahi, a chi a.
12Wanafunzi wake wakamwambia, "Bwana, ikiwa amelala, basi atapona."
12Huchiin, nungjuiten a kiangah, Toupa, a ihmut takleh a halh nawn nake, a chi ua.
13Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
13Jesun a sih thu a gen hi; himahleh, amau a khawl sunga aihmut thu a gen hiam a sa ua.
14Basi, Yesu akawaambia waziwazi, "Lazaro amekufa;
14Huchiin, Jesun chiantakin a kiang uah agen a, Lazar a si ahi.
15Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake."
15Huai ka om louh nou jiakin ka kipak hi, na gintak theihna ding un; himahleh a kiangah I hoh ding uh, a chi a.
16Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, "Twendeni nasi tukafe pamoja naye!"
16Huan, Thoma, Didum a chih un, a nungzuihpihte kiangah, A sihnaa I sih samna dingin i hoh ding uh, a chi a.
17Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
17Huchiin, Jesun a tunin, ni li hanah a na omta chih a thei a.
18Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
18Bethani khua tuh Jerusalem kho kianga om ahi a, ching sawm leh ching nga phiala gamla ahi;
19Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
19huchiin a sanggampa uh sih tunga khamuangsak dingin Judate tampi Martha leh Mari kiangah a hong ua.
20Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
20Huan, Marthain Jesu a hong dek chih a jakin a vadawn a; Mari bel in ah a tu lailai a.
21Martha akamwambia Yesu, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
21Huan, Marthain Jesu kiangah, Toupa, hiaia om hi lechin, ka sanggampa si lou ding hi a.
22Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa."
22Tun ah leng Pathian kianga na nget peuhmah Pathian in nang honpe ding chih ka thei, a chi a.
23Yesu akamwambia, "Kaka yako atafufuka."
23Jesun a kiangah, Na sanggampa a thounawn ding, a chi a.
24Martha akamjibu, "Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho."
24Marthain a kiangah, Ni tawp ni chiah, thohnawnna ah, a thou nawn ding chih ka thei, a chi a.
25Yesu akamwambia, "Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
25Huan, Jesun a kiangah, Kei thohnawnna leh hinna ka hi; kuapeuh hon gingta tuh si mahleh a hing gige ding;
26na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?"
26A hing peuhmaha, a hon gingta peuhmah khantawnin a si kei ding; huai thu na gingta hia? a chi a.
27Martha akamwambia, "Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni."
27Aman a kiangah, Gingta e, Toupa; Kris, Pathian Tapa, khovela hongpai dingpa na hi chih ka gingta hi, a chi a.
28Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, "Mwalimu yuko hapa, anakuita."
28Huan huai thu a gen khit takin a kuana, a sanggamnu Mari tuh a sim sapa, Sinsakpa hiaiah a om a, nang honsam hi, a chi a.
29Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
29Huan, aman huai a jak takin, a dingkhe paha, a kiangah a vahoh a.
30Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
30Jesun tuh khua ah a lut naikei a. Marthain a vadawn laia, a omna ngei ah a om lai hi.
31Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
31Huan, in sunga a khamuana ompih Judaten Mari dingkhe paha, a pawt a muh tak un, hanah kap dinga hoh dek hiin teh, chiin, a jui ua.
32Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!"
32Huan, Mari Jesu omna a vatunga, a muh takin a khebul ah a khupboha, a kiangah, Toupa, hiaia om hi lechin, ka sanggampa si louding hia, a chi a.
33Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
33Huan, Jesun Mari kap leh a honjui Judate kap a mu a, a lung a khoih mahmaha, khain amau hi;
34Kisha akawauliza, "Mlimweka wapi?" Wakamwambia, "Bwana, njoo uone."
34huan, aman amah kaw sial na hi ua? a chi a. Amau a kiangah, Toupa hongpai inla, en in, a chi ua.
35Yesu akalia machozi.
35Jesu a kapta.
36Basi, Wayahudi wakasema, "Tazameni jinsi alivyompenda!"
36Huan, Judaten, En di uh, Lazar it na tele; a chi ua.
37Lakini baadhi yao wakasema, "Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?"
37Himahleh khenkhatin, Hiai mi, mittopa mit hihvakpan, hiai mi leng a si lou sak theikeia eita? a chi ua.
38Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
38Huan, Jesu lungsung nakpi a khoiha om nawnin, han a tungta a. Huai han tuh kokhuk ahi a, suanga sit ahi.
39Yesu akasema, "Ondoeni hilo jiwe!" Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, "Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!"
39Jesun, Suang hem un, a chi a. A si sanggamnu Marthain a kiangah, Toupa, tun jaw a namta ding, a sihna ni li a hita ngala, a chi a.
40Yesu akamwambia, "Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?"
40Jesun a kiangah, Na gintak leh Pathian thupina na mu ding, kon chi ka hia? a chi a. Huchiin, suang a hem ua.
41Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, "Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
41Huan, Jesu a vandak a, Pa ka thu na ngaih khiak jiakin na tungah ka kipak hi.
42Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma."
42Ka thu na ngaikhe jel chih ka thei a; himahleh, mipi, ding diamduamte jiakin hiai ka chi ahi, nang non sawl chih a gintak theihna dingun, a chi a.
43Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: "Lazaro! Toka nje!"
43Huan, huchia a pau khitin aw ngaih takin, Lazar, hongpawt in, a chi a, a kikou a.
44Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, "Mfungueni, mkamwache aende zake."
44Huan, misi tuh a khut a khe, han puana tuam sain a hong pawtta a, a mai leng kinulna puana tuam ahi a. Jesun a kiang uah, Phel unla, pai sak un, a chi a.
45Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
45Huaijiakin Mari kianga hong; Jesu thil hih mu, Judate a khen tampiin Jesu a gingta uhi;
46Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
46himahleh, a khen Pharisaite kiangah a vahoh ua, a kianguah Jesu thilhihte a vahilh uh.
47kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, "Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
47Huchii siampuliante leh Pharisaiten vaihawmte a sam khawm ua, Bangchibangin i hih ding ua? Hiai miin thillamdang tampi a hih ngala.
48Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!"
48Hichi banga i khahzam injaw mi tengtengin amah a gingta ding ua; huan, Rome mite a hongpai ding ua, i mun leh i chite a honlak sak ding uh, a chi ua.
49Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, "Ninyi hamjui kitu!
49Huan, a lak ua mi khat Kaiaphain, huai kuma Siampu Lianpen ahi a, a kiang uah, Nou bangmah theikei uteh.
50Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?"
50i chi tengteng manthat louhna dingin mi tengteng sika mi khat sih, nou a din a hoih chih leng na ngaihtuah kei uh, a chi a.
51Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
51Huai thu tuh amah phuah tawmin a gen kei, huai kumin Siampu Lianpen ahi a, a chite uh sika Jesu a sih ding a genkhol ahi jaw hi.
52na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
52Huai chite sik kia ahi keia, Pathian ta khovela dalhte tengteng pawl khata a pi khawmna dingin leng ahi sam hi.
53Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
53Huchiin, huai ni akipan amah hihlum dingin a kihou jel uh.
54Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
54Huaijiakin Jesu Judate lakah a langin a vak nawnta keia, huaia kipanin gamdai jul lama kho khat Ephraim a chih uah a vahoh zota hi; huaiah nugjuite toh a om nilouh ta uhi.
55Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
55Huan, Judate Paikan Ankuangluina a naita a, mi tampi kisiangsak dingin, gam apat, Paikan Ankuanglui main, Jerusalem khua ah a hohtou ua.
56Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, "Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?"
56Huchiin, Jesu a zong ua, Pathian biakin ah ding kawmin a kihou ua, Bang ahia na gintak uh? Ankuangluina ah a hongkei ding maw? a kichi ua.Siampu liante leh Pharisaiten amah amat theihna ding un kuapeuhin a omna a theih uleh amaute theihsak ding thu a peta uhi.
57Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.
57Siampu liante leh Pharisaiten amah amat theihna ding un kuapeuhin a omna a theih uleh amaute theihsak ding thu a peta uhi.