1Siku sita kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu alifika Bethania alikoishi Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka wafu.
1Huan, Paikan Ankuangluina ding ni guk a om nalai a, Jesun misi laka kipana a kaihthoh Lazar omna Bethani khua a hongtung a.
2Huko walimwandalia chakula cha jioni, naye Martha akawa anawatumikia. Lazaro alikuwa mmoja wa wale waliokuwa mezani pamoja na Yesu.
2Huan, huaiah amaha din nitakan a bawl ua, Marthain nek a bawl hi, Lazar bel a ankuang umpih khat ahi a.
3Basi, Maria alichukua chupa ya marashi ya nardo safi ya thamani kubwa, akampaka Yesu miguu na kuipangusa kwa nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marashi.
3Huan, Mariin buk kimkhat spiknardi that namtui manpha tak a hontawia, Jesu khete a nuih a, a samin a khete a nula, huchiin huai thau gimin in tuh a dimta hi.
4Basi, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
4Himahleh, Iskariot, Juda, a nungjui khat, a mansak dingpan,
5"Kwa nini marashi hayo hayakuuzwa kwa fedha dinari mia tatu, wakapewa maskini?"
5Hiai thau namtui bangdia makhai zathuma juaka mi gentheite kianga pe zolou uh ahia? a chi a.
6Alisema hivyo, si kwa kuwa alijali chochote juu ya maskini, bali kwa sababu alikuwa mweka hazina, na kwa kuwa alikuwa mwizi, mara kwa mara aliiba kutoka katika hiyo hazina.
6Mi gentheite a khotuah jiaka huai theu gen ahi kei; guta ahi a, dangka ip a kem a, a sunga koih a lak jel jiak ahi jaw.
7Lakini Yesu akasema, "Msimsumbue huyu mama! Mwacheni ayaweke kwa ajili ya siku ya mazishi yangu.
7Huan, Jesun, Hih hen aw. Ka kivui ni-a dinga a sit a zang ahi, sen hen aw.
8Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini hamtakuwa nami siku zote."
8Mi gentheite na kiang ua om gige ahi ua, kei bel na kiang ua om gige ding ka hi kei, a chi a.
9Wayahudi wengi walisikia kwamba Yesu alikuwa Bethania. Basi, wakafika huko si tu kwa ajili ya kumwona Yesu, ila pia wapate kumwona Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka wafu.
9Huan, Jesu huaiah a om chih Juda mipi vantangin a na theita ua; huan, a hong ua, Jesu jiak kia hi louin, misi laka kipan a kaihthoh, Lazar mah leng a muh nop jiak uh ahi.
10Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,
10Huan, siampu liante Lazar leng hihlum dingin a kikou ua;
11Maana kwa sababu ya Lazaro Wayahudi wengi waliwaasi viongozi wao, wakamwamini Yesu.
11amah jiaka Judate tampiin a langkai san ua, Jesun a gintak jiakun.
12Kesho yake, kundi kubwa la watu waliokuja kwenye sikukuu walisikia kuwa Yesu alikuwa njiani kuja Yerusalemu.
12A jingin, ankuangluinaa hong mipi tampiin, Jesu Jerusalem khua ah a hong ding chih a jak un,
13Basi, wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki; wakapaaza sauti wakisema: "Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana. Abarikiwe mfalme wa Israeli."
13tum nahte a tawi ua, a dawn dingin a vapawt ua, Hosanna, Toupa mina Israelte Kumpipa hongpai a hampha e, chiin, a kikou ua.
14Yesu akampata mwana punda mmoja akapanda juu yake kama yasemavyo Maandiko:
14Huan, Jesun sabengtung nou a mu a, a tungah a tuang a.
15"Usiogope mji wa Sioni! Tazama, Mfalme wako anakuja, Amepanda mwana punda."
15Lau ken, Zion tanu; en in, na Kumpipa, sabengtung nou tunga tuangin, a hongding, chih gelh bangin.
16Wakati huo wanafunzi wake hawakuelewa mambo hayo, lakini Yesu alipokwisha tukuzwa, ndipo walipokumbuka kwamba hayo yalikuwa yameandikwa juu yake, na kwamba watu walikuwa wamemtendea hivyo.
16Huai thute a tungin a nungjuiten a theisiam keu ua; himahleh, Jesu pahtawia a om nungin, a tanchin ah huai thu gelh ahi chih leh, a tungah huai thilte a na hih ngei uh chih a theita ua.
17Kundi la watu wale waliokuwa pamoja naye wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, akamfufua kutoka wafu, walisema yaliyotukia.
17Huan, Lazar hana kipana a sapkhiakpa, misi laka kipan a kaihthoh laia a kianga mipi omten, a thu a theihpih uhi.
18Kwa hiyo umati huo wa watu ulimlaki, maana wote walisikia kwamba Yesu alikuwa amefanya ishara hiyo.
18Huaijiakin ahi, mipiten leng amah a vadawn uh, huai thillamdang a hih chih a thei ngal ua.
19Basi, Mafarisayo wakaambiana, "Mnaona? Hatuwezi kufanya chochote! Tazameni, ulimwengu wote unamfuata."
19Huchiin, Pharisaiten, Thei un, bangmah na hih theih louh uh, en un, khovelin amah a juita hi, a kichi ua.
20Kulikuwa na Wagiriki kadhaa miongoni mwa watu waliokuwa wamefika Yerusalemu kuabudu wakati wa sikukuu hiyo.
20Huan, ankuangluinaa Pathian be dinga hohtoute lakah Grik kuate hiam a om ua;
21Hao walimwendea Filipo, mwenyeji wa Bethsaida katika Galilaya, wakasema, "Mheshimiwa, tunataka kumwona Yesu."
21huan huaite Galili gama Bethsaida khuaa mi Philip kiangah a hong ua, a kiangah, Pu, Jesu mu nuam ung, a chi ua, a thum un.
22Filipo akaenda akamwambia Andrea, nao wawili wakaenda kumwambia Yesu.
22Philipin Andru a honghilha; huan, Andru leh Philipin Jesu a honghilh uh.
23Yesu akawaambia, "Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mtu imefika!
23Huan, Jesun a dawnga, a kiang uah, Mihing Tapa pahtawia a omna ding hun a tungta.
24Kweli nawaambieni, punje ya ngano hubaki punje tu isipokuwa ikianguka katika udongo na kufa. Kama ikifa, basi huzaa matunda mengi.
24Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, Buh tang leia a kiak a, a sih kei leh, amah kiain a om tawntung hi; a sihin bel, tampiin a gah nak hi.
25Anayependa maisha yake, atayapoteza; anayeyachukia maisha yake katika ulimwengu huu, atayaweka kwa ajili ya uzima wa milele.
25Kuapeuh a hinna itin a magsak a; kuapeuh hiai khovela a hinna ngaineuin khantawna hinna ah a vom gige ahi.
26Anayetaka kunitumikia ni lazima anifuate, hivyo kwamba popote pale nilipo mimi ndipo na mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu yeyote anayenitumikia Baba yangu atampa heshima.
26Kuapeuhin ka na a sep leh honjui hen; ka omna ah ka nasempa leng a om ding hi; kuapeuhin ka na a sep leh Pain amah a pahtawi ding hi.
27"Sasa roho yangu imefadhaika, na niseme nini? Je, niseme: Baba, usiruhusu saa hii inifikie? Lakini ndiyo maana nimekuja--ili nipite katika saa hii.
27Tun ah ka kha a mangbang hi; bang ka gen dia? Pa, hiai hun lakah honhondam in, ka chi dia hia? Chi lou e. Hiai dinga tu tana na om hiing a.
28Baba, ulitukuze jina lako." Hapo sauti ikasema kutoka mbinguni, "Nimelitukuza, na nitalitukuza tena."
28Pa na min pahtawi in, a chi a. Huchiin vana kipanin aw hongsuaka, Ka pahtawita, ka pahtawi lai ding achia a.
29Umati wa watu waliokuwa wamesimama hapo walisikia sauti hiyo, na baadhi yao walisema, "Malaika ameongea naye!"
29Huan, mipi a kianga dingten huai a ja ua, Vanpi ging ahi, a chi ua; midangten, Angelin amah a houpih ahi, a chi ua.
30Lakini Yesu akawaambia, "Sauti hiyo haikutokea kwa ajili yangu mimi, ila kwa ajili yenu.
30Jesun a dawnga, Huai aw keia dia hongsuak ahi kei, noumaua ding ahi jaw.
31Sasa ndio wakati wa ulimwengu huu kuhukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu huu atapinduliwa.
31Tu tuh hiai khovel vaihawmsakna hun ahi; tuin hiai khovel lal paih khiak ahi ding.
32Nami nitakapoinuliwa juu ya nchi nitamvuta kila mmoja kwangu."
32Huan, leia kipana khai kanga ka om leh, mi tengteng kei mah kiangah ka hip ding, a chi a.
33(Kwa kusema hivyo alionyesha atakufa kifo gani).
33Huai thu tuh a sih dingdan theihsakna dia a gen ahi.
34Basi, umati huo ukamjibu, "Sisi tunaambiwa na Sheria yetu kwamba Kristo atadumu milele. Wawezaje basi, kusema ati Mwana wa Mtu anapaswa kuinuliwa? Huyo Mwana wa Mtu ni nani?"
34Huan, mipin a kiangah, Kris khantawnin a om ding chih dan bu ah ka thei uh, Nang, Mihing Tapa khaikanga om ding ahi, bangchi chiha chi na hia? Huai Mihing Tapa tuh kua ahia? a chi ua, adawng ua.
35Yesu akawaambia, "Mwanga bado uko nanyi kwa muda mfupi. Tembeeni mngali mnao huo mwanga ili giza lisiwapate; maana atembeaye gizani hajui aendako.
35Huan, Jesun a kianguah, Vak na lak uah sawt lou a omtadih hi. Vak na neih lai un vak ah khosa un, huchilouin jaw mialin honlap ding hi. Kuapeuh miala khosain a paina a theikei.
36Basi, wakati mnao huo mwanga uaminini ili mpate kuwa watu wa mwanga." Baada ya kusema maneno hayo, Yesu alikwenda zake na kujificha mbali nao.
36Vak na neih lai un vak gingta un, vak tate na honghih theihna dingun, a chi a. Huai thute Jesun a gena; huan, apaia, amuh louh dingun a buta.
37Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini.
37A ma uah huchi tela tam thillamdang hih mahleh, amah a gingta tuan kei ua:
38Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia: "Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu? Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?"
38Toupa, ka thu gen uh kuan ahia gingta? Toupa khut leng kua kiangah ahia latsaka a om? chih jawlnei Isai thugen a tun na dingin.
39Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya tena alisema:
39Hiai jiakin ahi a gintak theih louh uh, Isaiin.
40"Mungu ameyapofusha macho yao, amezipumbaza akili zao; wasione kwa macho yao, wasielewe kwa akili zao; wala wasinigeukie, asema Bwana, ili nipate kuwaponya."
40Aman a mit uh a hihtaw a, a lung tang uh a hihkhauh a; huchilou injaw a mit un a mu khading ua, a lungtang un a thei kha ding uh, huan, hongkihei nawn khading ua, ken amau ka hihdam khading hi, chih, a gen nawn jiakin.
41Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliuona utukufu wa Yesu, akasema habari zake.
41Isaiin a thupina a muh leh a tanchin thu agen jiakin huai thu a gen hi.
42Hata hivyo, wengi wa viongozi wa Wayahudi walimwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakumkiri hadharani kwa kuogopa kwamba watatengwa na sunagogi.
42Himahleh, heutute laka nangawn tampiin Jesu a gingta ua; a hihhangin Pharisaite jiakin a kipulak nuam kei uh, huchilou injaw kikhopna in ah a nong kha ding uh:
43Walipendelea kusifiwa na watu kuliko kusifiwa na Mungu
43Pathian pahtawina sangin mihing pahtawina a deih zo ngal ua.
44Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, "Mtu aliyeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma.
44Huan, Jesu a kikou a, Kuapeuh hon gingta tuh kei gingta ahi kei, honsawlpa gingta ahi jaw.
45Anayeniona mimi anamwona pia yule aliyenituma.
45Kuapeuh kei hon mu tuh honsawlpa mu ahi.
46Mimi ni mwanga, nami nimekuja ulimwenguni ili wote wanaoniamini wasibaki gizani.
46Vak dia khovela hong ka hi a, kuapeuh kei hon gingta tuh miala a om louhna ding in.
47Anayeyasikia maneno yangu lakini hayashiki mimi sitamhukumu; maana sikuja kuhukumu ulimwengu bali kuuokoa.
47Kuapeuh ka thu gen jain, gingta kei mahleh, ken siam louh ka tangsak kei: khovel siam louh tangsak dinga hong ka hi kei a, khovel humbit dinga hong ka hi zo ngala.
48Asiyeyashika maneno yangu anaye wa kumhukumu: neno lile nililosema ni hakimu wake siku ya mwisho.
48Kuapeuh kei hondeih lou a, ka thu gente pom louin, siamlouh tangsak khat a nei ahi, ka thu gen, huai thu mahmahin, ni tawpni chiah amah siamlouh a tang sak ding hi.
49Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini.
49Keimah phuahtawmin ka gen ngal keia; Pa honsawlpan ka gen ding leh ka hih ding thu a honpe jaw ahi.Amah thupiak khantawna hinna ahi chih ka thei; huaijiakin thu ka gen, Pa honhilh bang jelin ka gen ahi, a chi a.
50Nami najua kuwa amri yake huleta uzima wa milele. Basi, mimi nasema tu yale Baba aliyoniagiza niyaseme."
50Amah thupiak khantawna hinna ahi chih ka thei; huaijiakin thu ka gen, Pa honhilh bang jelin ka gen ahi, a chi a.