Swahili: New Testament

Paite

John

18

1Yesu alipokwisha sema hayo, alikwenda ng'ambo ya kijito Kedroni, pamoja na wanafunzi wake. Mahali hapo palikuwa na bustani, naye Yesu akaingia humo pamoja na wanafunzi wake.
1Jesun huai thute a gen khitin a nungjuite toh a pawt ua, Kidron luiguam a kan ua, huaiah huan a om a, hui ah a lut ua, amah leh a nungjuite toh.
2Yuda, aliyemsaliti Yesu, alipajua mahali hapo kwani mara nyingi Yesu alikutana na wanafunzi wake huko.
2Huan, a mansakpa Juda in leng huai mun a theita; Jesu a nungjuite toh huaiah a pawt jeljel ngal ua.
3Basi, Yuda alichukua kikosi cha askari na walinzi kutoka kwa makuhani wakuu na Mafarisayo, akaja nao bustanini wakiwa na taa, mienge na silaha.
3Huchiin Judain sepaih pawl toh, siampu liante leh Pharisaite kianga om heutute toh a pi a, khawnvakte, meiselte, galvante tawiin huaiah a hongpai ua.
4Yesu, hali akijua yote yatakayompata, akatokea, akawauliza, "Mnamtafuta nani?"
4Jesun a tunga thil tungding tengteng a thei gige a, a vapawta, a kiang uah, Kua ahia na zon uh? a chi a.
5Nao wakamjibu, "Yesu wa Nazareti!" Yesu akawaambia, "Mimi ndiye." Msaliti Yuda alikuwa amesimama hapo pamoja nao.
5Amau a kiangah, Nazaret Jesu a chi ua, a dawng ua. Jesun a kianguah Keimah ka hi, a chi a.
6Basi, Yesu alipowaambia: "Mimi ndiye", wakarudi nyuma, wakaanguka chini.
6Huan, a mansakpa Juda leng a lak uah a ding a. Huai Keimah ka hi, a chih takin, a nungtolh ua, leiah a puk duam ua.
7Yesu akawauliza tena, "Mnamtafuta nani?" Wakamjibu, "Yesu wa Nazareti!"
7Huan, aman a kianguah, Kua ahia na zon uh? a chi a, a dawng nawna. Huan, amau, Nazaret Jesu, a chi ua.
8Yesu akawaambia, "Nimekwisha waambieni kwamba mimi ndiye. Basi, kama mnanitafuta mimi, waacheni hawa waende zao."
8Huan, Jesun, Keimah ka hi chih kon hilhta a; nou kei honzong na hih uleh hiaite hoihtakin khah un, a chi a a dawng a.
9(Alisema hayo ili yapate kutimia yale aliyosema: "Wale ulionipa sikumpoteza hata mmoja.")
9Hiai tuh a thugen, Nang kei non piakte khat leng ka mangsaak kei, a chih, a tunna din ahi.
10Simoni Petro alikuwa na upanga; basi, akauchomoa, akamkata sikio la kulia mtumishi wa Kuhani Mkuu. Mtumishi huyo aliitwa Malko.
10Huan, Simon Peterin namsau a voma, a doka, siampu lianpen sikha a sata, a bil taklam a sat khiak saka. Sikha min tuh Malka ahi.
11Basi, Yesu akamwambia Petro, "Rudisha upanga wako alani. Je, nisinywe kikombe alichonipa Baba?"
11Huchiin, Jesun Peter kiangah, Huai namsau a pai ah siatin; Pain nou kei honpiak ka dawn kei dia hia? a chi a.
12Kile kikosi cha askari, mkuu wake na walinzi wa Wayahudi walimkamata Yesu, wakamfunga
12Huchiin, sepaih pawl toh, heutupen u toh, Judate heutute toh Jesu a man ua, a hen ua.
13na kumpeleka kwanza kwa Anasi; Anasi alikuwa baba mkwe wa Kayafa ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo.
13Ana kiangah a pi masa ua, Kaiapha sungpa a hih jiakin. Kaiapha, huai kuma siampu lianpen ahi a.
14Huyo Kayafa ndiye aliyekuwa amewashauri Wayahudi kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya taifa.
14Kaiapha, Mi tengteng sanga mikhat sih a hoih, chia, Judate hasuanpa ahi.
15Simoni Petro pamoja na mwanafunzi mwingine walimfuata Yesu. Huyo mwanafunzi mwingine alikuwa anajulikana kwa Kuhani Mkuu, hivyo aliingia pamoja na Yesu ndani ya ukumbi wa Kuhani Mkuu.
15Huan, Simon Peterin Jesu a juia, a nungjui dang khat toh. Huai nungjuipa tuh siampu lianpen mel theih ahia, siampu lianpen in huangsung intual ah, Jesu kiang ah a lut sam a;
16Lakini Petro alikuwa amesimama nje, karibu na mlango. Basi, huyo mwanafunzi mwingine aliyekuwa anajulikana kwa Kuhani Mkuu alitoka nje akasema na mjakazi, mngoja mlango, akamwingiza Petro ndani.
16himahleh Peter jaw po lamah kongkhak bulah a ding hi. Huchiin nungjui dang siampu lianpen meltheih, a va pawta, kongkhak ngaknu a houpiha, Peter a pi luta.
17Huyo msichana mngoja mlango akamwuliza Petro, "Je, nawe pia ni mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu?" Petro akamwambia, "Si mimi!"
17Huan, kongkhak ngaknu nungakin Peter kiangah, Nang leng hiai mi nungjuite laka pangsam na hi hia? a chi a.
18Watumishi na walinzi walikuwa wamewasha moto kwa sababu kulikuwa na baridi, wakawa wanaota moto. Naye Petro alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.
18Aman, Ka hi kei, a chi a. Huan, sikhate leh heutute huaiah a ding diamduam ua, a vot jiakin meiholin mei a toh ua, a lum a awi uhi; Peter leng a kiangua a pang a, ding kawmin mei lum a awi sam hi.
19Basi, Kuhani akamwuliza Yesu juu ya wanafunzi wake na mafundisho yake.
19Huan, siampu lianpenin Jesu a nungjuite tanchin leh a thuhilh dan a donga.
20Yesu akamjibu, "Nimesema na kila mtu daima hadharani. Kila mara nimefundisha katika masunagogi na Hekaluni, mahali wakutanikiapo Wayahudi wote; na wala sijasema chochote kwa siri.
20Jesun a dawnga, a kiangah, Khovel mi kiangah, vantang theihin, thu ka gen gige a; kikhopna in leh, Pathian biakin, Juda tengteng om khawmna ahte bang thu ka hilh jela, a simin bangmah ka gen kei hi.
21Kwa nini waniuliza mimi? Waulize wale waliosikia nini niliwaambia. Wao wanajua nilivyosema."
21Bang achia kei hondong? A kiang ua ka thu gendan ka thu zate dong in; ngaiin, huaiten ka thugen a thei uh a keihiam, a chi a.
22Alipokwisha sema hayo mlinzi mmoja aliyekuwa amesimama hapo akampiga kofi akisema, "Je, ndivyo unavyomjibu Kuhani Mkuu?"
22Huan a gen takin a kianga ding heutu khatin Jesu a benga, siampu lianpen hichi bangin na dawng maw? a chi a.
23Yesu akamjibu, "Kama nimesema vibaya, onyesha huo ubaya; lakini ikiwa nimesema vema, mbona wanipiga?"
23Jesun a kiangah, Thu gilou gen ka hih leh, a gitlouhna hontheisak in; himahleh, thu pha ka gen inleng bang achia honbeng? a chi a, a dawnga.
24Basi, Anasi akampeleka Yesu akiwa amefungwa, kwa Kuhani Mkuu Kayafa.
24Huan, Anain hensain siampu lianpen Kaiapha kiangah a saw hi.
25Petro alikuwa hapo akiota moto. Basi, wakamwuliza, "Je, nawe pia si mmoja wa wanafunzi wake?" Yeye akakana na kusema, "Si mimi!"
25Huan, Simon Peterin dingin meilum a awi a. Huan, Nang leng a nungjuite laka pang sam na hi hia? a chi ua. Aman, Ka hi kei, chiin, a kitheihmohbawla.
26Mmoja wa watumishi wa Kuhani Mkuu, jamaa wa yule aliyekatwa sikio na Petro, akamwuliza, "Je, mimi sikukuona wewe bustanini pamoja naye?"
26Huan, simapu lianpu sikha khat, Peter bil sat khiak sanggamin, A kiangah, huan ah ka honmu kei maw? a chi a.
27Petro akakana tena; mara jogoo akawika.
27Huchiin Peterin a kitheihmohbawl nawn a; huan, ak a khuang pah ngal hi.
28Basi, walimchukua Yesu kutoka kwa Kayafa, wakampeleka ikulu. Ilikuwa alfajiri, nao ili waweze kula Pasaka, hawakuingia ndani ya ikulu wasije wakatiwa najisi.
28Huan, Jesu Kaiapha in a kipanin kumpipa in ah a pi nawn ua; jingsang ahi a; huan, amau jaw kumpipa in ah a lut kei uh, a lut un jaw a buah ding ua, Paikan Ankuanglui a ne theikei kha ding uhi.
29Kwa hiyo, Pilato aliwaendea nje, akasema, "Mna mashtaka gani juu ya mtu huyu?"
29Huan, Pilat a kiang uah a va pawta, a kiang uah, Hiai mi tungah hekna bang ahia na neih uh? a chi a.
30Wakamjibu, "Kama huyu hangalikuwa mwovu hatungalimleta kwako."
30Amau a kiangah, Hiai mi migilou hi keileh na kiang ah kon pi kei ding uh, a chi ua, a dawng ua.
31Pilato akawaambia, "Haya, mchukueni ninyi wenyewe, mkamhukumu kufuatana na Sheria yenu." Wayahudi wakamjibu, "Sisi hatuna mamlaka ya kumwua mtu yeyote."
31Huan, Pilatin a kiang uah, Nou pi unla, na dan bang un a thu vaihawmsak un, a chi a. Judaten a kiangah, Kou thuin kuamah hihlup dan ahi kei, a chi ua.
32(Ilifanyika hivyo yapate kutimia maneno aliyosema Yesu kuonyesha atakufa kifo gani.)
32Hiai tuh a sih danding thu, Jesun a gen banga, a tuna dingin ahi.
33Pilato akaingia tena ndani ya ikulu, akamwita Yesu na kumwuliza: "Ati wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?"
33Huchiin, Pilat a in ah a lut nawna, Jesu a sama, a kiangah, Judate kumpipa na hi ahia? a chi a.
34Yesu akamjibu, "Je, hayo ni maneno yako au wengine wamekwambia habari zangu?"
34Jesun, Hiai nangmah lungsim puak khiaka na gen hia, midang in honhilh, ka tungtang thu? a chi a, a dawng a.
35Pilato akamjibu, "Je, ni Myahudi mimi? Taifa lako na makuhani wamekuleta kwangu. Umefanya nini?"
35Pilatin, Kei Juda mi ka hi ahia? Nangmah chite leh siampu lianten ka kiangah nang a honpi ua ahi; thil bang ahia na hih? a chi a, a dawng a.
36Yesu akamjibu, "Ufalme wangu si wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu watumishi wangu wangenipigania nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini sasa ufalme wangu si wa hapa."
36Jesun, Ka kumpihihna hiai khovela ahi kei; ka kumpihihna hiai khovela hi leh, ka sikhaten gal a dou ding uh, Judate kianga piaka ka om louhna dingin; himahleh, ka kumpihihna jaw hiai khovela kipan ahi kei hi, a chi a, a dawng a.
37Hapo Pilato akamwambia, "Basi, wewe ni Mfalme?" Yesu akajibu, "Wewe umesema kwamba mimi ni Mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili hiyo; na kwa ajili hiyo nimekuja ulimwenguni kuwaambia watu juu ya ukweli. Kila mtu wa ukweli hunisikiliza."
37Huan, Pilatin a kiangah, E, kumpipa na hi maw? a chi a. Jesun, Hi e, kumpipa ka hi. Thutak theihsak ka piansan leh khovela ka hongpai san ahi. Kuapeuh thutaka peuhmahin ka thu a sang uh, a chi a.
38Pilato akamwambia, "Ukweli ni kitu gani?" Pilato alipokwisha sema hayo, aliwaendea tena Wayahudi nje, akawaambia, "Mimi sioni hatia yoyote kwake.
38Pilatin, a kiangah, Thutak tuh bang ahia? a chi a. Huan, Huai thu a gen khit takin, Judate kiangah a vapawt nawna, a kiang uah, Bangmah a gitlouhna ka mu kei.
39Lakini, mnayo desturi kwamba mimi niwafungulie mfungwa mmoja wakati wa Pasaka. Basi, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?"
39Himahleh, Paikan Ankuangluina ah mi khat kon pawtsak ding dan na nei uh; huchiin, Judate kumpipa honpawt sak leng na ut uhia? a chi a.Huan, amau a kikou nawn ua, Hiai mi jaw hi kei henla, Barabba pen hi jaw heh a chi ua. Barabba tuh suamhat ahi.
40Hapo wakapiga kelele: "La! Si huyu ila Baraba!" Naye Baraba alikuwa mnyang'anyi.
40Huan, amau a kikou nawn ua, Hiai mi jaw hi kei henla, Barabba pen hi jaw heh a chi ua. Barabba tuh suamhat ahi.