1Basi, Pilato akaamuru Yesu achukuliwe, apigwe viboko.
1Huan, huchihlaiin Pilatin Jesu a pi a, a jep a.
2Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika na joho la rangi ya zambarau.
2Huan, sepaihten ling lukhu a phan ua, a khusak ua, puan san dup leng a silh sak uh;
3Wakawa wanakuja mbele yake na kusema: "Shikamoo, Mfalme wa Wayahudi!" Wakampiga makofi.
3huan, a kiangah a hongpai ua, Chibai; Judate Kumpipa: a chi ua, a beng uh.
4Pilato akatoka tena nje, akawaambia, "Tazameni, namleta nje kwenu, mpate kujua kwamba mimi sikuona hatia yoyote kwake."
4Huan, Pilat a pawt nawna, a kiang uah, En un, bangmah a gitlouhna ka mu kei chih na theihna ding un, na kiang uah ka honpi khia ahi, a chi a.
5Basi, Yesu akatoka nje amevaa taji ya miiba na joho la rangi ya zambarau. Pilato akawaambia, "Tazameni! Mtu mwenyewe ni huyo."
5Huan, Jesu linglukhu khuin leh puan sandup silh in a hong pawta. Huan, Pilatin a kiang uah, En un, Mihing! a chi a.
6Makuhani wakuu na walinzi walipomwona wakapaaza sauti: "Msulubishe! Msulubishe!" Pilato akawaambia, "Mchukueni basi, ninyi wenyewe mkamsulubishe, kwa maana mimi sikuona hatia yoyote kwake."
6Huan, siampu liante leh heututen amah a muh tak un a kikou ua, Kros ah kilhlum in, kros ah kilhlum in, a chi ua. Pilatin a kiang uah, Noumau paipih unla, kros ah kilhlum un; ken jaw bangmah a gitlouhna ka mu ngal kei a, a chi a.
7Wayahudi wakamjibu, "Sisi tunayo Sheria, na kufuatana na Sheria hiyo, ni lazima afe, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu."
7Judaten a kiangah, Ka dan uh khat a om, huai dan bang jelin Pathian Tapaa a kibawl jiakin a si ding ahi, a chi ua, a dawng ua.
8Pilato aliposikia maneno hayo akazidi kuogopa.
8Huan, Pilatin huai thu a jakin a lau nawn semsema;
9Basi, akaingia tena ndani ya ikulu, akamwuliza Yesu, "Umetoka wapi wewe?" Lakini Yesu hakumjibu neno.
9A in ah a lut nawna, Jesu kiangah, Koia kipan na hia? a chi a.
10Hivyo Pilato akamwambia, "Husemi nami? Je, hujui kwamba ninayo mamlaka ya kukufungua na mamlaka ya kukusulubisha?"
10Himahleh, Jesun a dawng kei. Huan, Pilatin a kiangah, Nang kei honhoupih lou ding maw? Honkhah thei ka hi, krosa honkilhlum thei ka hi chih na thei ka hia? a chi a.
11Yesu akamjibu, "Hungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama hungepewa na Mungu. Kwa sababu hiyo, yule aliyenikabidhi kwako ana dhambi kubwa zaidi."
11Jesun, Tunglam akipan piak hi kei lechin, ka tungah hih theih himhim na neikei ding; huaijiakin na kianga honpekhepan khelhna lianjaw a pua ahi, a chi a.
12Tangu hapo, Pilato akawa anatafuta njia ya kumwachilia, lakini Wayahudi wakapiga kelele: "Ukimwachilia huyu mtu, wewe si rafiki yake Kaisari; kila mtu anayejifanya kuwa Mfalme humpinga Kaisari!"
12Huai nungsiah Pilatin khah a tuma; himahleh Judate a kikou ua, Hiai mi na khah leh Kaisar lawm na hi kei ding; kuapeuh kumpipaa kibawl tuh Kaisar dou ahi, a chi ua.
13Basi, Pilato aliposikia maneno hayo akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo: "Sakafu ya Mawe" (kwa Kiebrania, Gabatha).
13Huan, Pilatin huai thu a jak takin, Jesu a pi khia a, a min Suanglep, Hebru paua Gabbatha a chih uh, huai munah thukhenna tutphah ah a tu a.
14Ilikuwa yapata saa sita mchana, siku ya maandalio ya Pasaka. Pilato akawaambia Wayahudi, "Tazameni, Mfalme wenu!"
14Huan, huai ni tuh Paikan Ankuangluina kiginni ahi a, dak gukna khawng ahi. Huan, aman Judate kiangah, En un, na Kumpipa uh, a chi a.
15Wao wakapaaza sauti: "Mwondoe! Mwondoe! Msulubishe!" Makuhani wakuu wakajibu, "Sisi hatuna Mfalme isipokuwa Kaisari!"
15Huan, amau a kikou ua, Hihmangthang in, hihmangthang in, kros ah kilhlum in, a chi ua. Pilatin a kiang uah, Na Kumpipa uh kros ah ka kilhlum ding maw? a chi a. Siampu lianten, Kaisar loungal kumpipa dang ka neikei uh, a chi ua, a dawng uh.
16Basi, hapo Pilato akamtia Yesu mikononi mwao ili asulubiwe. Basi, wakamchukua Yesu.
16Huchiin Pilatin krosa kilhlup dingin amah a kiang uah a peta hi.
17Naye akatoka akiwa amejichukulia msalaba wake kwenda mahali paitwapo "Fuvu la Kichwa", (kwa Kiebrania Golgotha).
17Huchiin Jesu a pita ua; huan, aman kros kipuakin Luguh Mun, a chih uh, Hebru paua Golgotha a chih uah, huai mun tan a paia;
18Hapo ndipo walipomsulubisha, na pamoja naye waliwasulubisha watu wengine wawili; mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto, naye Yesu katikati.
18huaiah kros ah a kilhlum ua, mi dang nih toh, a sik ah khat tuaktuakin, a lai ah Jesu.
19Pilato aliandika ilani akaiweka juu ya msalaba. Nayo ilikuwa imeandikwa hivi: "Yesu wa Nazareti, Mfalme wa Wayahudi."
19Huan, Pilatin lai a gelha, kros ah a suanga, NAZARET JESU JUDATE KUMPIPA, chia, gelh ahi.
20Wayahudi wengi waliisoma ilani hiyo, maana mahali hapo aliposulubiwa Yesu palikuwa karibu na mji. Tena ilani hiyo ilikuwa imeandikwa kwa Kiebrania, Kilatini, na Kigiriki.
20Huan, huai lai tuh Judate a khen tampiin a sim ua; Jesu kros a kilhlupna mun uh khopi kiang ahi a; Hebru pau bang. Rome pau bang, Grik pau banga gelh ahi ngala.
21Basi, makuhani wakuu wakamwambia Pilato, "Usiandike: Mfalme wa Wayahudi, ila Yeye alisema, Mimi ni Mfalme wa Wayahudi."
21Huchiin, Judate siampu lianten Pilat kiangah, Judate Kumpipa, chiin, gelh ken; Judate Kumpipa ka hi, a chi, chiin, gelh jawin, a chi ua.
22Pilato akajibu, "Niliyoandika, nimeandika!"
22Pilatin, Ka gelh khit tuh ka gelhkhit ahita, achia, a dawnga.
23Askari walipokwisha msulubisha Yesu, walizichukua nguo zake, wakazigawa mafungu manne, fungu moja kwa kila askari. Walichukua pia na kanzu yake; kanzu hiyo ilikuwa imefumwa kwa kipande kimoja tu, bila mshono.
23Huan, sepaihten Jesu krosa a kilhlup khit un a puansilh a la ua, phel liin a bawl ua, sepaihten phel khatin a tang chiat ua; a puannak leng a la uh. Puannak khui louh puannak ahi a a ngawng a kipan a puma gat vek ahi;
24Basi, hao askari wakashauriana: "Tusiipasue, ila tuipigie kura itakuwa ya nani." Jambo hilo lilifanyika ili yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: "Waligawana mavazi yangu, na nguo yangu wakaipigia kura." Basi, ndivyo walivyofanya hao askari.
24huaijiakin amau, I bot kek kei dia, kuaa pending a hihiam ai i san zo ding uh, a kichi ua. Laisiangthoua, Ka puansilhte a kihawm ua, ka puannak din ai a san uh, chih a tunn dingin. Huai thil tuh sepaihten a hih uhi.
25Karibu na msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada ya mama yake, Maria mke wa Kleopa, na Maria Magdalene.
25Huan, Jesu kros kiangah a nu leh a nu sanggam, Mari Kleopa ji leh Mari Magdalini a ding ua.
26Yesu alipomwona mama yake, na karibu naye amesimama yule mwanafunzi aliyempenda, akamwambia mama yake: "Mama! Tazama, huyo ndiye mwanao."
26Huan, Jesun a nu leh nungjui a itpa a kianga ding a mua, a nu kiangah, Numei, en in, na tapa; a chi a.
27Halafu akamwambia yule mwanafunzi: "Tazama, huyo ndiye mama yako." Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake.
27Huan, nungjuipa kiangah, En in, na nu; a chi a. Huan, huai nungsiah, huai nungjuiin amah in ah amah a pita hi.
28Yesu alijua kwamba yote yalikuwa yametimia; na, ili Maandiko Matakatifu yapate kutimia, akasema, "Naona kiu."
28Huai nungin, Jesu thil bangkim tunah hih zoh a hita chih a thei a, (laisiangthou a tuna dingin) Ka dang a tak, a chi a.
29Hapo palikuwa na bakuli limejaa siki. Basi, wakachovya sifongo katika hiyo siki, wakaitia juu ya ufito wa husopo, wakamwekea mdomoni.
29Huaiah bel khat uain thuka dim a tung ua, huchiin spanji khat uain thuka diah dimin, husop chiangah a tak ua, a muk ah a tun tou ua.
30Yesu alipokwisha pokea hiyo siki, akasema, "Yametimia!" Kisha akainama kichwa, akatoa roho.
30Huan, Jesun uain thuk a na dawn khitin, Zoh a hita, a chi a. Huan, a lu a kuna, a kha a khahta hi.
31Ilikuwa Ijumaa, siku ya Maandalio. Kwa hiyo, kusudi miili isikae msalabani siku ya Sabato, maana siku hiyo ya Sabato ilikuwa siku kubwa, Wayahudi walimwomba Pilato miguu ya hao waliosulubiwa ivunjwe na miili yao iondolewe.
31Huan, kiginni a hih jiakin, luangte khawlnia krosa a om nilouh louhna dingin, (huai Khawlni ni thupi ahi ngala), Judaten Pilat kiangah a khete uh hihtana a luang uh paipih dingin a ngen ua.
32Basi, askari walikwenda, wakaivunja miguu ya yule mtu wa kwanza na yule wa pili ambao walikuwa wamesulubiwa pamoja na Yesu.
32Huan, sepaih a hongpai ua, a kianga krosa a kilhlup uh mi tuah masak leh mi khat a khe uh a hihtan ua;
33Lakini walipomfikia Yesu waliona kwamba alikwisha kufa, na hivyo hawakumvunja miguu.
33himahleh, Jesu kiang a hongtun un, a na sita chih a thei ua, a khete a hihtan tuanta kei uh.
34Lakini askari mmoja alimtoboa ubavuni kwa mkuki, na mara ikatoka damu na maji.
34Himahleh, sepaihte laka mi khatin a nakah teiin a suna, huchiin sisan leh tui a pawt pah hi.
35(Naye aliyeona tukio hilo ametoa habari zake ili nanyi mpate kuamini. Na hayo aliyosema ni ukweli, tena yeye anajua kwamba anasema ukweli.)
35A mupan a theisakta, a thu theihsak a dik ahi; a gen dik chih a kithei-nou leng na gin takna ding un.
36Jambo hilo lilitendwa ili Maandiko Matakatifu yatimie: "Hapana hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa."
36Laisiangthou, A guh khat leng hihtan ahi kei ding, chih, tuna dingin huai thil a hongomta hi.
37Tena Maandiko mengine yanasema: "Watamtazama yule waliyemtoboa."
37Huan, laisiangthou dangin, Amah a sutpa uh a en ding uh, leng a chi hi.
38Baada ya hayo, Yosefu, mwenyeji wa Armathaya, alimwomba Pilato ruhusa ya kuuchukua mwili wa Yesu. (Yosefu alikuwa mfuasi wa Yesu, lakini kwa siri, maana aliwaogopa viongozi wa Wayahudi). Basi, Pilato akamruhusu. Hivyo Yosefu alikwenda, akauondoa mwili wa Yesu.
38Huan, huai thil hih khitin, Joseph, Arimathai mi, Jesu nungjui, Judate kihtak jiak a sim om in Jesu luang paipih dingin Pilat kiangah a ngena; huan, Pilatin a phala, Huchiin, a hongpaia, a luang a paipihta.
39Naye Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu usiku, akaja akiwa amechukua mchanganyiko wa manemane na ubani kiasi cha kilo thelathini.
39Huan, Nikodem, atunga jana a kianga hongin, murra leh aloe kihelsa buk sawmnga khawng tawiin a hong sama.
40Basi, waliutwaa mwili wa Yesu, wakaufunga sanda pamoja na manukato kufuatana na desturi ya Wayahudi katika kuzika.
40Huan, Jesu luang a la ua, Judate kivui dan bangin gimlimte toh puan malngat hoihin a tuam uh.
41Mahali hapo aliposulubiwa Yesu palikuwa na bustani, na katika bustani hiyo kulikuwa na kaburi jipya ambalo hakutiwa bado mtu yeyote ndani yake.
41Huan, krosa a kilh lupna mun uah huan khat a oma; huan ah kuamah sialna ngei nailouh han thak khat a om hi.Huan, Judate kiginni a hih jiakin, han a kiang chin uh a hih toh, huaiah Jesu a sialta uh.
42Basi, kwa sababu ya shughuli za Wayahudi za maandalio ya Sabato, na kwa vile kaburi hilo lilikuwa karibu, wakamweka Yesu humo.
42Huan, Judate kiginni a hih jiakin, han a kiang chin uh a hih toh, huaiah Jesu a sialta uh.