Swahili: New Testament

Paite

John

20

1Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.
1Huan, ni sagih ni masapenin, jingin, khua a mial laiin, Mari Magdalini han ah a va hoha, suang tuh han akipan lak suanin a mu a.
2Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, "Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka."
2Huchiin a tai a, Simon Peter leh nungjui dang Jesun a itpa kiangah a hongpaia, a kiang uah, Hana kipan Toupa a pai mangpihta uh, a koihna uh ka theikei uh, a chi a.
3Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.
3Huchiin, Peter a pawta, nungjui dang toh, huan, han lam a juan ua.
4Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
4Huan, a tai tuak ua; nungjui dangin Peter a makhelh a, han a tung masa a.
5Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.
5Huan, a kun a, a en a, puan malngat hoih om tuh a mu a; himaleh a sungah a lut kei hi.
6Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,
6Huan, Simon Peterin leng a nungah a honjui a, han sungah a luta;
7na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.
7puan malngat hoih om leh, a lu-a kinulna puan om, puan malngat hoih laka om loua, jial saa mun tuama om a mu a.
8Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
8Huchiin nungjui dang, han tung masa leng a lut sama, a mu a, a gingtata hi.
9(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
9Misi laka kipan a thou nawn ding ahi chih laisiangthou a theigige nawn ngal kei ua.
10Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
10Huchiin, nungjuite amau in ah a pai nawnta uhi.
11Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,
11Himahleh, Mari tuh a pua ah han kiangah kap kawmin a dinga; huan kap kawmin a kuna, han sung a en a;
12akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.
12huan, angel nih puan ngou silhin, Jesu luang sialna munah, khat a lu lamah, khat a khe lamah tu a mu a.
13Hao malaika wakamwuliza, "Mama, kwa nini unalia?" Naye akawaambia, "Wamemwondoa Bwana wangu, na wala sijui walikomweka!"
13Huan, amau a kiangah, Numei, banga chia kap na hia? a chi ua. Aman a kiang uah, Ka Toupa a pai mang pih ua, a koihna uh ka theih louh jiakin, a chi a.
14Baada ya kusema hayo, aligeuka nyuma, akamwona Yesu amesimama hapo, lakini asitambue ya kuwa ni Yesu.
14Huan, huchia a gen takin a nung lam a nga a, Jesu ding tuh a mu a, himahleh Jesu ahi chih a theikei.
15Yesu akamwuliza, "Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?" Maria, akidhani kwamba huyo ni mtunza bustani, akamwambia, "Mheshimiwa, kama ni wewe umemwondoa, niambie ulikomweka, nami nitamchukua."
15Jesun a kiangah, Numei, Bang dia kap na hia? Kua ahia na zon? a chi a. Aman, huanpu hiam a sa a, a kiang ah, Pu, amah hiaia kipan na pai mang pih a hih leh, na koihna honhilh tanla, huchiin ka la ding, a chi a.
16Yesu akamwambia, "Maria!" Naye Maria akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, "Raboni" (yaani "Mwalimu").
16Jesun a kiangah, Mari, a chi a. Amah a kiheia, a kiangah Hebru pauin, Rabboni, a chi a; (huai tuh Sinsakpa, chihna ahi a).
17Yesu akamwambia, "Usinishike; sijakwenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu."
17Huan, Jesun a kiangah, Hon len ken, tu tan inleng Pa kiangah ka kah tou nai kei ahi; a hihhangin ka unaute kiangah vahoh inla, a kiang uah, Ka pa, na Pa uh, ka Pathian, na Pathian uh kiang ah ka kah tou dek, a chi hi, chiin, a chi a.
18Hivyo Maria Magdalene akaenda akawapa habari wale wanafunzi kuwa amemwona Bwana, na kwamba alikuwa amemwambia hivyo.
18Mari Magdalini a va hoha, nungjuite kiangah, Toupa ka muta, a chi a, a kianga thu a gendante leng a hilh a.
19Ilikuwa jioni ya siku hiyo ya Jumapili. Wanafunzi walikuwa wamekutana pamoja ndani ya nyumba, na milango ilikuwa imefungwa kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Basi, Yesu akaja, akasimama kati yao, akawaambia, "Amani kwenu!"
19Huan, huai ni, ni sagih ni masapenin, nitak lama hong hihin, Judate kihtak jiaka nungjuite omna kongkhakte a khak nung un, Jesu hongpaia, a lak uah a hongdinga, a kiang uah, Na tunguah khamuanna om hen, a chi a.
20Alipokwisha sema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi, hao wanafunzi wakafurahi mno kumwona Bwana.
20Huan, huai a gen khitin a khut leh a nak a kiang uah a laka. Huan, Toupa amuh tak un nungjuite a kipakta uh.
21Yesu akawaambia tena, "Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi."
21Huan, Jesun a kiang uah, Na tunguah khamuanna om hen, Pan kei honsawl bang mahin nou ka honsawl ahi, a chi nawna.
22Alipokwisha sema hayo, akawapulizia na kuwaambia, "Pokeeni Roho Mtakatifu.
22Huan, huai thu a gen khitin amau a hat khuma, a kiang uah, Kha Siangthou tang un,
23Mkiwasamehe watu dhambi zao, wamesamehewa; msipowaondolea, hawasamehewi."
23kua khelna leng na ngaihdam peuh uh ngaihdam ahi ding; kua khelhna leng na ngaihdam louh peuh uh, ngaihdam louh ahi ding, a chi a.
24Thoma mmoja wa wale kumi na wawili (aitwaye Pacha), hakuwa pamoja nao wakati Yesu alipokuja.
24Huan, Jesu a hong lain sawm leh nihte laka pangsam Thoma, Didum a chih uh, a kiang uah a om sam keia.
25Basi, wale wanafunzi wengine wakamwambia, "Tumemwona Bwana." Thoma akawaambia, "Nisipoona mikononi mwake alama za misumari, na kutia kidole changu katika kovu hizo, na kutia mkono wangu ubavuni mwake, sitasadiki."
25Huchiin, nungjui dangten, a kiang ah, Toupa ka muta uh, a chi ua. Himahleh aman a kiang uah, A khut sik khetna pawn khawng ka muha, ka khut a ka khoih a, a naka ka khut ka koih hial keileh, ka gingta kei ding, a chi a.
26Basi, baada ya siku nane hao wanafunzi walikuwa tena pamoja mle ndani, na Thoma alikuwa pamoja nao. Milango ilikuwa imefungwa, lakini Yesu akaja, akasimama kati yao, akasema, "Amani kwenu!"
26Huan, ni giat nungin, a nungjuite in sungah a om nawn ua, Thoma leng a kiang uah a om sama. Huan kongkhakte khak hinapiin, Jesu hongpaia a lak uah a hong dingta, a kiang uah, Na tunguah khamuanna om hen, a chi a.
27Kisha akamwambia Thoma, "Lete kidole chako hapa uitazame mikono yangu; lete mkono wako ukautie ubavuni mwangu. Usiwe na mashaka, ila amini!"
27Huan, Thoma kiangah, Na khutzungin honsawk inla, ka khutte en in; na khutin ban inla, ka nak khawngah sawk in; gingta louin om kenla, gingtain, a chi a.
28Thoma akamjibu, "Bwana wangu na Mungu wangu!"
28Thomain a kiangah, Ka Toupa leh ka Pathian na hi, a chi a, a dawnga.
29Yesu akamwambia, "Je, unaamini kwa kuwa umeniona? Heri yao wale ambao hawajaona, lakini wameamini."
29Jesun a kiangah, Nang jaw non muh jiakin na gingta ahi; mu loua gingta peuhmahte a hampha uhi, a chi a.
30Yesu alifanya mbele ya wanafunzi wake ishara nyingine nyingi ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki.
30Huan, Jesun nungjuite maah chiamtehna dang tampitak a hiha, huaite hiai laibu ah gelh ahi kei hi;himahleh hiaite Jesu, Kris, Pathian Tapa ahi chih na gintakna ding uleh, na gintak ua a mina hinna na neihna ding ua gelh ahi.
31Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mpate kuwa na uzima kwa nguvu ya jina lake.
31himahleh hiaite Jesu, Kris, Pathian Tapa ahi chih na gintakna ding uleh, na gintak ua a mina hinna na neihna ding ua gelh ahi.