Swahili: New Testament

Paite

Luke

15

1Siku moja, watoza ushuru na wahalifu wengi walikwenda kumsikiliza Yesu.
1Huan, siahkhonmite leh mi khialte tengtengin a thu za dingin a kiang a honjuan ua.
2Mafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunung'unika: "Mtazameni mtu huyu! Anawakaribisha wenye dhambi, na tena anakula nao."
2Huan, Pharisaite leh laigelhmiten, Hiai miin mi khialte a khawla, a kianguah an a ne chiin, a phun tuaktuak ua.
3Yesu akawajibu kwa mfano:
3Huchiin, aman a kianguah hiai gentehna a gen a:
4"Hivi, mtu akiwa na kondoo mia, akigundua kwamba mmoja wao amepotea, atafanya nini? Atawaacha wale tisini na tisa mbugani, na kwenda kumtafuta yule aliyepotea mpaka ampate.
4Nou lakah kuapeuhin belam ja nei unla, a lak ua khat mangsak le-uchin, gamdai ah sawmkua leh kuate nusiain, amang pen na muh nawn ma siah uh kua ahia zong lou ding?
5Akimpata, atambeba mabegani kwa furaha.
5Huan, na muh nawn un tuh kipaktakin na liangjang uah na pua ua.
6Anapofika nyumbani, atawaita rafiki zake akiwaambia, Furahini pamoja nami, kwa sababu nimempata yule kondoo wangu aliyepotea.
6Huan, in natun tak un, na lawmte uleh na vengte uh na sam khawm ua, a kiang uah, Hon kipahpih un, ka belam mang ka mu nawnta, na chi uh.
7Kadhalika nawaambieni, ndivyo kutakavyokuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya kutubu kwa mwenye dhambi mmoja, kuliko kwa ajili ya watu tisini na tisa wanaojiona kuwa wema, wasiohitaji kutubu.
7Ka honhilh ahi, huchi bangmahin, mi dik sawm kua leh kua kisik tuanding neiloute tungah sangin mi khial khat kisik tungah vana mi a kipak zo ding uh.
8"Au mwaonaje? Tuseme mwanamke fulani ana sarafu kumi za fedha, akipoteza moja, atafanya nini? Atawasha taa, aifagie nyumba na kuitafuta kwa uangalifu mpaka aipate.
8Huan, numei kuapeuhin makhai sawm neiin khat mang sak leh, khawnvak dein, in phiatin a muh nawn masiah kua ahia hoihtaka zong lou ding?
9Akiipata, atawaita rafiki na jirani zake akisema, Furahini pamoja nami, kwa sababu nimeipata ile sarafu yangu iliyopotea.
9Huan, a muh nawn intuh, a lawmte leh a vengte a sam khawma, Honkipahpih un, ka makhai mansak ka mu nawn ta, a chi a.
10Kadhalika nawaambieni, ndivyo watakavyofurahi malaika wa Mungu kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja anayetubu."
10Ka honhilh ahi, huchi bangmahin, Pathian angelte maah, mi khial khat kisik tungah, kipahna om nak.
11Yesu akaendelea kusema, "Kulikuwa na mtu mmoja mwenye wana wawili.
11Mi kua hiamin tapa nih a nei a;
12Yule mdogo, alimwambia baba yake: Baba, nipe urithi wangu. Naye akawagawia mali yake.
12huan, a naupang zopenin, a pa kiangah, Pa, gou ka tansik honpia in, a chi a. Huchiin, a sum tuh a kianguah a hawmta a.
13Baada ya siku chache, yule mdogo aliuza urithi wake, akasafiri na fedha aliyopata, akaenda nchi ya mbali ambako aliitumia ovyo.
13Huan, ni sawt lou nungin a tapa naupang zopenin a tansik tengteng a la khawm veka, gam gamlapi ah a zinta a, huai ah nuam tat luain a sum a mawk zat mangta a.
14Alipomaliza kutumia kila kitu, kukatokea njaa kali katika nchi ile, naye akaanza kuhangaika.
14Huan, a zat bei zoh vek takin, huai gamah kial thupitak a hongtunga; nek ding a hong kitasamta a.
15Akaomba kazi kwa mwananchi mtu mmoja wa huko naye akampeleka shambani mwake kulisha nguruwe.
15Huchiin, huai gam mi khat a vabela; huaiin vok an pe dingin a lou lamah a sawla.
16Alitamani kula maganda waliyokula wale nguruwe, ila hakuna mtu aliyempa kitu.
16Huan, bangkhat hawng vokin a nekte ua kihihvah a ut mahmaha; kuamahin lah bangmah a pe ngal kei ua.
17Alipoanza kupata akili akafikiri: Mbona kuna wafanyakazi wengi wa baba yangu wanaokula na kusaza, nami ninakufa njaa?
17Huan, amah leh amah hongkiphawk khiak takin, Ka pa kianga kilohte an nek zoh louha nei a tamtam utoh, kei lah hiai ah gilkiala si ding hi mai vengin;
18Nitarudi kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia.
18Ka thou dinga, ka pa kiangah ka pai dinga, a kiangah, Pa, vana tungah leh nangmah mitmuhin thil ka hihkhial; na tapaa seh tak ka hitakei hi;
19Sistahili hata kuitwa mwanao. Nifanye kama mmoja wa wafanyakazi wako.
19na kianga kiloh khat bangin hon bawl samin, ka chi ding, a chi a.
20Basi, akaanza safari ya kurudi kwa baba yake. Alipokuwa bado yu mbali, baba yake alimwona, na kwa moyo wa huruma alimkimbilia, akamkumbatia na kumbusu.
20Huchiin, a thou a, a pa kiangah a paita a. Huan, gamlapia a omlaiin, a pan a namu a, a lainat mahmaha, a taia, a vapoma a tawp tonton a.
21"Mwanawe akamwambia: Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia. Sistahili hata kuitwa mwanao.
21Huan, a kiangah a tapain, Pa, vana tungah leh nangmah mitmuhin thil ka hihkhial; na tapaa seh tak ka hita kei, a chi a.
22Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: Haraka! Leteni nguo nzuri mkamvike! Mvisheni pete na viatu!
22Himahleh, a pan, a sikhate kiangah, Puan hoihpen honla khepah unla, silh sak un; a khutah zungbuh a khepekah khedap bun sak un;
23Mchinjeni ndama mnono; tule kusherehekea!
23bawngnou thau tak honla unla; gou un, i ne ding ua, nopbawlin i om ding uh;
24Kwa sababu huyu mwanangu alikuwa amekufa, kumbe yu mzima alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana. Wakaanza kufanya sherehe.
24hiai ka tapa a sia, a honghing nawnta ahi; a manga, i mu nawnta uhi, a chi a. Huchiin kipaktakin a om panta ua.
25"Wakati huo kaka yake alikuwa bado shambani. Alipokuwa akirudi na kukaribia nyumbani akasikia vifijo na ngoma.
25Huan, a tapa upa jaw lou ah a oma; huan, in a hong tun kuanin bangpeuh tum ging leh lam husa a zata a.
26Akamwita mmoja wa watumishi, akamwuliza: Kuna nini?
26Huchiin, a sikha khat a sama, Tuabang ahia? chiin, a donga.
27Huyo mtumishi akamwambia: Ndugu yako amerudi nyumbani, na baba yako amemchinjia ndama mnono kwa kuwa amempata akiwa salama salimini.
27Huan, aman, a kiangah, Na nau a hongtunga, dam takin a muh nawn jiakin na pan bawng nou thau tak a gou, a chi a.
28Huyo kijana mkubwa akawaka hasira hata akakataa kuingia nyumbani. Baba yake akatoka nje na kumsihi aingie.
28Huan, a heha, a lut nuamta keia; huchiin, a pa hongpawt khia a, a khema.
29Lakini yeye akamjibu: Kumbuka! Miaka yote nimekutumikia, sijavunja amri yako hata mara moja. Umenipa nini? Hujanipa hata mwana mbuzi mmoja nikafanye sherehe pamoja na rafiki zangu!
29Himahleh, aman, a pa kiangah, Ngai in, kum hichi zah na na sem inga, na thua lah talek ngei lou inga; ka lawmte toh kipahna ka bawlna dingin kelnou leng non pe ngei ngal keia.
30Lakini mtoto wako huyu aliyekula mali yako pamoja na makahaba, mara tu alipokuja umemchinjia yule ndama mnono.
30Himahleh, hiai na tapa kijuakte kianga na sum ne mang vekpa a hongtun takin amah adingin bawngnou thau tak na nagoh sak viala, a chi a, a dawng a.
31Baba yake akamjibu: Mwanangu, wewe uko pamoja nami siku zote, na kila nilicho nacho ni chako.
31Huan, aman a kiangah, Ka tapa, ka kianga om gige hi china, ka neih tengteng leng nanga hi a.Kipak leh nuamtaka om ding ahi vo oi; hiai na nau a sia; a honghing nawna; a manga, i mu nawnta ahi ngala, a chi a, a chi a.
32Ilitubidi kufanya sherehe na kufurahi, kwa sababu huyu ndugu yako alikuwa amekufa, kumbe yu mzima; alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana."
32Kipak leh nuamtaka om ding ahi vo oi; hiai na nau a sia; a honghing nawna; a manga, i mu nawnta ahi ngala, a chi a, a chi a.