Swahili: New Testament

Paite

Luke

14

1Siku moja ya Sabato, Yesu alikwenda kula chakula nyumbani kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo; watu waliokuwapo hapo wakawa wanamchunguza.
1Huan, hichi ahi a, Khawlniin Pharisai vaihawmmi khat ina an ne dinga hoh in, a en khia ua.
2Mbele yake Yesu palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa na ugonjwa wa kuvimba mwili.
2Huan, ngai in, a ma ah damlou chibawk mi kua hiam a oma.
3Yesu akawauliza walimu wa Sheria na Mafarisayo, "Je, ni halali au la kumponya mtu siku ya sabato?"
3Huchiin, Jesun dan theimi leh Pharisaite a houpiha, a kiang uah, Khawlniin hihdam asiang hia, siang lou? a chi a.
4Lakini wao wakakaa kimya. Yesu akamshika huyo mgonjwa, akamponya, akamwacha aende zake.
4Amau bel a dai dide ua, huan, aman damlou tuh a len a, a hihdama, a paisakta a.
5Halafu akawaambia, "Ni nani kati yenu ambaye mtoto wake au ng'ombe wake akitumbukia shimoni, hangemtoa hata kama ni siku ya Sabato?"
5Huan, a kianguah, Na lak uah na sabengtung u hiam, bawng hiam tuitohkhiakkhuk ah nake taleh, Khawlniin leng kua ahia kai khepah lou ding? a chi a.
6Nao hawakuweza kumjibu swali hilo.
6Huai thu tuh a dawng theikei uh.
7Yesu aliona jinsi wale walioalikwa walivyokuwa wanajichagulia nafasi za heshima, akawaambia mfano:
7Huan, a mi sapte un tutnamun hoihpen a tel jel dan uh a mu a, a kiang uah gentehna thu a genta a:
8"Kama mtu akikualika arusini, usiketi mahali pa heshima isije ikawa amealikwa mwingine mheshimiwa kuliko wewe;
8Kitenna an ne dinga kuapeuhin a honsap chiangin tutnamun hoihpen ah tu kei un; huchilou injaw, na sang ua mi phajaw a na sam kha dia, huchiin, a honsampan,
9na mwenyeji wenu ninyi wawili atakuja na kukwambia: Mwachie huyu nafasi. Hapo utaaibika mbele ya wote na kulazimika kwenda kuchukua nafasi ya mwisho.
9Hiai mi tutna ding awn in, a hon chi dia; huan nang zumpiin tutnamun niam pen ah natu nawn phing ding ahi.
10Bali ukialikwa kwenye karamu, keti mahali pa mwisho, ili mwenyeji wako atakapokuja akwambie: Rafiki, njoo hapa mbele, mahali pazuri zaidi. Hapo utakuwa umeheshimika mbele ya wote wanaoketi pamoja nawe.
10A honsap chiangin tutnamun niam pen ah na vatu zo ding a; huchiin a honsampa a hong chiangin, na kiangah, Lawm, tutnamum hoih deuh ah tu in, a honchi theiding. Huchiin na anumpihte mitmuhin pahtawiin na om ding.
11Kwa maana yeyote anayejikweza atashushwa, na anayejishusha, atakwezwa."
11Kingaipha peuh a neu ding ua: kingaineu tuh pahtawiin a om ding uh, a kiang uah a chi a.
12Halafu akamwambia na yule aliyemwalika, "Kama ukiwaandalia watu karamu mchana au jioni, usiwaalike rafiki zako au jamaa zako au jirani zako walio matajiri, wasije nao wakakualika nawe ukawa umelipwa kile ulichowatendea.
12Huan, a sampa kiangah leng, Sunin hiam, janin hiam ankuang na lui chiangin, na lawmte, na unaute, na sanggamte, na inveng mihaute na sam kei ding; huchilou injaw a honsam thuk ding ua, a honthuk chitchiat kha ding uh.
13Badala yake, unapofanya karamu, waalike maskini, vilema viwete na vipofu,
13Ankuang na lui chiangin, tagahte, piangsualte, khebaite, mittawte, na sam zo ding;
14nawe utakuwa umepata baraka, kwa kuwa hao hawana cha kukulipa. Maana Mungu atakupa tuzo lako wakati watu wema watakapofufuka."
14huchiin, huai bangten thukna ding a neih louh jiak un, na hampha ding; mi dikte thoh nawn chiangin thuk nawn na hih ding jiakin, a chi a.
15Mmoja wa wale waliokuwa wameketi pamoja na Yesu akasema, "Ana heri mtu yule atakayekula chakula katika Ufalme wa Mungu."
15Huan, a anumpih kuahiamin huai thu tuh a ja a, a kiangah, Pathian gama an ne ding tuh a hampha, a chi a.
16Yesu akamjibu, "Mtu mmoja alifanya karamu kubwa, akaalika watu wengi.
16Huan, aman, a kiangah, Mi kuahiamin janin ankuang thupi luina a bawla, mi tampi a sama;
17Wakati wa karamu ulipofika alimtuma mtumishi wake awaambie walioalikwa, Njoni, kila kitu ni tayari.
17huan, anek hunin, ami sapte kiangah, Hong ua, tuin bangkim manta, chi dingin a sikha a sawla.
18Lakini wote, kwa namna moja, wakaanza kuomba radhi. Wa kwanza akamwambia mtumishi: Nimenunua shamba, kwa hiyo sina budi kwenda kuliangalia; nakuomba uniwie radhi.
18Huan, a vek un thu khat satin paulam a nei chiat ua. A masapenin, a kiangah, Lou ka leita a, a en dia ka hoh kipha moh hi; honhehpih inla, hon na ngai siam heh, a chi a.
19Mwingine akasema: Nimenunua ng'ombe jozi tano wa kulima; sasa nimo njiani kwenda kuwajaribu; nakuomba uniwie radhi.
19Huan, midangin, Bawng tuak nga ka leita a, a siat a phat chiandingin ka kuan dinga, honhehpih inla hon na ngai siam heh, a chi a.
20Na mwingine akasema: Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.
20Huan, mi dangin, ji ka neita a, huaijiakin ka hoh theikei, a chi a.
21Mtumishi huyo akarudi na kumwarifu bwana wake jambo hilo. Yule mwenye nyumba alikasirika, akamwambia mtumishi wake: Nenda upesi kwenye barabara na vichochoro vya mji, uwalete hapa ndani maskini, viwete, vipofu na waliolemaa.
21Huan, sikhain, a pu kiangah, huai thute tuh a vahilh ta a. Huan, inneipa tuh a heh a, a sikha kiangah, Pawt inla, kongzing khawngah, kawmkal khawngah pai mengmeng inla, tagahte, piangsualte, mittawte, khebaite hiai laiah honpilut in, a chi a.
22Baadaye, mtumishi huyo akasema: Bwana mambo yamefanyika kama ulivyoamuru, lakini bado iko nafasi.
22Huan, a sikhain, Pu, non thupiak bangin ka hihkhina, himahleh mun awng lailaive aw, a chi a.
23Yule bwana akamwambia mtumishi: Nenda katika barabara na vichochoro vya mji uwashurutishe watu kuingia ili nyumba yangu ijae.
23Huan, a puin, sikha kiangah, Pawt inla, lamlian khawng ah, dai khawng ah pai inla, ka in dimna dingin mi hon sawl lut teitei in.
24Kwa maana, nawaambieni, hakuna hata mmoja wa wale walioalikwa atakayeonja karamu yangu."
24Ka honhilh ahi, Mi ka sapte khatin leng ka ankuang lui achiam kei hial ding, a chi a, a chi a.
25Hapo, makundi mengi yakawa yanaandamana pamoja na Yesu. Basi, akawageukia akawaambia,
25Huan, mipi thupi takte a kiangah a hoh sam ua; huchiin amah a kiheia, a kianguah,
26"Mtu yeyote akija kwangu, asipowachukia baba na mama yake, mke wake, watoto, ndugu na dada zake, naam, hata na nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
26Kuapeuh ka kianga hongin, a pa, a nu, a ji, a tate, a unau a sanggamnu, leh amah hinna nangawn toh a huat keileh ka nungjui ahi theikei ding.
27Mtu asipochukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
27Kuapeuh a kros pua honjui lou tuh ka nungjui ahi theikei ding.
28Kwa maana, ni nani miongoni mwenu ambaye akitaka kujenga mnara hataketi kwanza akadirie gharama zake ili ajue kama ana kiasi cha kutosha cha kumalizia?
28Nou laka kuapeuhin in sang lam tum le uchin, amasain tuin, lam zohna khop sum na neih uleh neih louh thei dingin, aman ding dan kuaa hia sut lou ding.
29La sivyo, baada ya kuweka msingi na kushindwa kumaliza, watu watamcheka
29Huchilou injaw, suang phum khin phota, a lam zoh theih kei leh, a en peuhin,
30wakisema: Mtu huyu alianza kujenga, lakini hakumalizia.
30Hiai min a gel na a, a lam zou thei ngal keia chiin, a nuihsan kha ding uh.
31"Au, ni mfalme gani ambaye, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, hataketi kwanza chini na kufikiri kama ataweza, kwa askari wake elfu ishirini?
31Huan, kumpipa kuain ahia kumpipa dang dou dinga a kuan dingin, a masaa tu a, mi sing nih toh amah dou ding a hong tuh, mi sing khat toh a tuah ngam ding leh ding louh, mi dong lou ding?
32Kama anaona hataweza, atawatuma wajumbe kutaka masharti ya amani wakati mfalme huyo mwingine angali mbali.
32Huchi a hihkei vanglakleh, kumpipa dang tuh gamla pia a om laiin, kituahna lam thuchiam ngen dingin palai a sawl ding.
33Vivyo hivyo, basi, hakuna hata mmoja wenu atakayekuwa mwanafunzi wangu kama asipoachilia kila kitu alicho nacho.
33Huchi bangmahin, nou lakah kuapeuh a neih tengteng paisan lou tuh ka nungjui ahi theikei ding.
34"Chumvi ni nzuri; lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini?
34Chi a hoiha, himahleh, chi leng a pen khitin, bangin a hih-al nawn ding ua?Leia dingin a hoih kei; ekvum dingin leng a hoih sam kei; min a pai khia uh. Kuapeuh jakna dinga bil neiin ja hen, a chi a.
35Haifai kitu wala kwa udongo wala kwa mbolea. Watu huitupilia mbali. Sikieni basi, kama mna masikio!"
35Leia dingin a hoih kei; ekvum dingin leng a hoih sam kei; min a pai khia uh. Kuapeuh jakna dinga bil neiin ja hen, a chi a.