Swahili: New Testament

Paite

Luke

13

1Wakati huo watu fulani walikuja, wakamweleza Yesu juu ya watu wa Galilaya ambao Pilato alikuwa amewaua wakati walipokuwa wanachinja wanyama wao wa tambiko.
1Huan, huchih lai takin, kuate hiam a na-om ua, huaiten, Galili gama Pilatin a sisan uh a Pathian biakna sa gohte laka a hel sakte tungtang Jesu a hilh ua.
2Naye Yesu akawaambia, "Mnadhani Wagalilaya hao walikuwa wahalifu zaidi kuliko Wagalilaya wengine, ati kwa sababu wameteseka hivyo?
2Huan, aman a kiang uah, Huai Galili gamete huchibang thil a thuak jiak un Galili gama tengteng sangin mi gilou tuan hi un na gingta ua hia?
3Nawaambieni hakika sivyo; lakini nanyi, hali kadhalika, msipotubu, mtaangamia kama wao.
3Hi lou e, ka honhilh ahi, nou leng na kisik kei uleh huchi bangmahin na mangthang vek dinguh.
4Au wale kumi na wanane walioangukiwa na mnara kule Siloamu wakafa; mnadhani wao walikuwa wakosefu zaidi kuliko wengine wote walioishi Yerusalemu?
4Huan, Siloam insangin mi sawm leh giat a delhlupte leng, Jerusalem khuaa omte tengteng sangin mi gilou tuan hi un na gingta ua hia?
5Nawaambieni sivyo; lakini nanyi msipotubu, mtaangamia kama wao."
5Hilou e, ka hon hilh ahi, nou leng na kisik kei uleh huchibang mahin na mangthang vek ding uh, a chi a, a dawnga.
6Kisha, Yesu akawaambia mfano huu: "Mtu mmoja alikuwa na mtini katika shamba lake. Mtu huyu akaenda akitaka kuchuma matunda yake, lakini akaukuta haujazaa hata tunda moja.
6Huan, hiai gentehna thu a gena; Kuahiamin a grep huanah theipi suan khat anei a: huan, a kungah a gah a hongzonga, khat leng amu kei a.
7Basi, akamwambia mfanyakazi wake: Angalia! Kwa miaka mitatu nimekuwa nikija kuchuma matunda ya mtini huu, nami nisiambulie kitu. Ukate! Kwa nini uitumie ardhi bure?
7Huchiin, grep gui kemmi kiangah, Ngai in, kum thum sung hiai thei kung ah a gah ka va zong jela, khatleng ka mu kei; phuk in; bangdia mun dala om nilouh ahia? a chi a.
8Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
8Huan, aman, a kiangah, Toupa, tukum bek om henla, a kimin ka tou dinga, ekin ka phungvuh tadih dia;
9Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata."
9huainunga a gah leh ahoih ding, a gah kei leh phuk mai in, achia.
10Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
10Huan khawl niin aman kikhopnain khat ah thu a hilh a.
11Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
11Huan, ngai in, kum sawm leh kum giat hatlouhna dawi mat numei khat a oma; huai mi tuh a kun kheukheu a, amah thuin a ding tang theikei hiala.
12Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, "Mama, umeponywa ugonjwa wako."
12Huan, Jesun amah a muh takin a sama, akiangah, Numei, na hatlouhnain a honkhahta, a chi a.
13Akamwekea mikono, na mara mwili wake ukawa wima tena, akawa anamtukuza Mungu.
13Huan, atungah a khut a koiha; huchiin, thakhatin a tangpah ngala, Pathian a phatta a.
14Lakini mkuu wa sunagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo akawaambia wale watu walikusanyika pale, "Mnazo siku sita za kufanya kazi. Basi, fikeni siku hizo mkaponywe magonjwa yenu; lakini msije siku ya Sabato."
14Huan, Jesun Khawlnia mi a hihdam jiakin kikhopna in heutu a heha, mipi a houpiha, a kiang uah, Mihing na sepna ding ni guk a om vo oi; huai sungin, kihihdam un, Khawlniin hi louin, a chi a.
15Hapo Bwana akamjibu, "Enyi wanafiki! Nani kati yenu hangemfungua ng'ombe au punda wake kutoka zizini ampeleke kunywa maji, hata kama siku hiyo ni ya Sabato?
15Toupan a kiangah, Nou lepchiahte aw, Khawlniin na bawng u hiam na sabengtung uhiam a an neknaa kipan phelin, tui dawndingin na pi khe chiat jel uh hi lou hia?
16Sasa, hapa yupo binti wa Abrahamu ambaye Shetani alimfanya kilema kwa muda wa miaka kumi na minane. Je, haikuwa vizuri kumfungulia vifungo vyake siku ya Sabato?"
16Hiai numei, Abraham tanu ahi ngala, ngai un, Setanin kum sawm leh kum giat a mana, Khawlniin leng hiai gak tuh phel sak louh dan ahia hia? a chi a, a donga.
17Alipokwisha sema hayo, wapinzani wake waliona aibu lakini watu wengine wote wakajaa furaha kwa sababu ya mambo yote aliyotenda.
17Huai thute a gen laiin a melmate tengteng a zum ua; mipi bel a thil thupi hih tengteng jiakin a kipak uh.
18Yesu akauliza: "Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaulinganisha na nini?
18Huchiin, aman, Pathian gam bang ahia? bang toh leng ka teh dia?
19NI kama mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake; ikaota hata ikawa mti. Ndege wa angani wakajenga viota vyao katika matawi yake."
19Ankam chi tangkhat min a laka, a huana a theh bang ahi, huai tuh a hongpou a, sing a honghi a, tungleng vasate khawng ahiangah a giak uh, a chi a.
20Tena akauliza: "Nitaulinganisha Ufalme wa Mungu na nini?
20Huan, Pathian gam bang toh ka the dia? a chi nawna.
21Ni kama chachu aliyoitwaa mama mmoja na kuichanganya pamoja na unga debe moja kisha unga wote ukaumuka wote."
21Silngou numeiin a laka, anbuang tehna thum laka a veka a thoh mateng a phumbang ahi, a chi a.
22Yesu alindelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri.
22Huan, aman thuhilh kawm jelin, Jerusalem kho lam naihin kholian leh kho neute a tawn jela.
23Mtu mmoja akamwuliza, "Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?"
23Huan, kuahiamin, a kiangah, Hotdamte tawm chik ahi ding u maw? a chi a.
24Yesu akawaambia, "Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.
24Huan, aman, a kiang uah, kong kochik ah lut tum teitei un; ka honhilh ahi, mi tampiin lut a tum ding ua, a lut thei ngal kei ding uh.
25"Wakati utakuja ambapo mwenye nyumba atainuka na kufunga mlango. Ninyi mtasimama nje na kuanza kupiga hodi mkisema: Bwana, tufungulie mlango. Lakini yeye atawajibu: Sijui mmetoka wapi.
25In neipa a thoha, kong a khak nungin, nou a puaa dingin, Toupa, kong honhonsak in, chiin kongkhak non kiuh chiang un, aman, Koi lam mi na hi ua, honthei lou ka hi, chiin, nou a hondawng dinga;
26Nanyi mtaanza kumwambia: Sisi ndio wale tuliokula na kunywa pamoja nawe; na wewe ulifundisha katika vijiji vyetu.
26huai hun chiangin, nou, Na muhin kane ua, ka dawn ve ua oi, ka kongzing uah leng thu na hilh jel vo oi, na chi ding uh.
27Lakini yeye atasema: Sijui ninyi mmetoka wapi; ondokeni mbele yangu, enyi nyote watenda maovu.
27Huan, aman, Ka honhilh ahi, Koi lam mi na hi ua, ka hon theikei; nou thil gilou hihtengtengte aw, ka kianga pat pai mang vek un, a honchi ding.
28Ndipo mtakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo, na manabii wote wapo katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mmetupwa nje!
28Abraham, Isaak, Jakob leh jawlnei tengteng Pathian gam, sunga om na muh ua, nou po lama delhkhiak na hih uh na kitheih chiangun, na kap ding ua, ha na gawi ding uh.
29Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini, watakuja na kukaa kwenye karamu katika Ufalme wa Mungu.
29Huan, suahlam leh tumlam, sim leh mal akipanin mite hongpai ding ua, Pathian gamah nein a dawn ding uh.
30Naam, wale walio wa mwisho watakuwa wa kwanza; na wale walio wa kwanza watakuwa wa mwisho."
30Huan, ngai un, nanungpente leng masapena om ding a om ua, masapente leng nanungpena om ding a om uh, a chi a.
31Wakati huohuo, Mafarisayo na watu wengine walimwendea Yesu wakamwambia, "Ondoka hapa uende mahali pengine, kwa maana Herode anataka kukuua."
31Huai laitakin Pharisai kuate hiam a hongpai ua, a kiangah, Pawt inla, hiaia kipan pai mang in: Herodin honhihlup ut mahmah ahi, a chi ua.
32Yesu akawajibu, "Nendeni mkamwambie huyo mbweha hivi: Leo na kesho ninafukuza pepo na kuponya wagonjwa, na siku ya tatu nitakamilisha kazi yangu.
32Huan, aman, a kiang uah, Huai sehal kiangah hiai thu vagen un: Ngai in, tuni toh, jingchiang toh dawite ka delhkhe dia, natnate leng ka hihdam dia a ni thum niin ka zou ding.
33Hata hivyo, kwa leo, kesho na kesho kutwa, ni lazima niendelee na safari yangu, kwa sababu si sawa nabii auawe nje ya Yerusalemu.
33Abangabang hitaleh, tuni toh, jingchiang toh, a ni thumni toh ka pai jel ding ahi; Jerusalem kho po lamah jawlnei sih theih hilou ahi.
34"Yerusalemu! We Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, Lakini wewe umekataa.
34Aw Jerusalem, Jerusalem: jawlneite that, na kianga honsawlte uh suanga na deng lum: akpiin a noute a kha nuaia a op khawmbangin na tate bangzah vei op khawm ka tum a? Himahleh na ut kei.En in, na in a vuaka taisanin a om. Huan, Ka honhilh ahi, Toupa mina hongpai a hampha, na chih ma siah non mu kei ding, a chi a.
35Haya, utaachiwa mwenyewe nyumba yako. Naam, hakika nawaambieni, hamtaniona mpaka wakati utakapofika mseme: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana."
35En in, na in a vuaka taisanin a om. Huan, Ka honhilh ahi, Toupa mina hongpai a hampha, na chih ma siah non mu kei ding, a chi a.