Swahili: New Testament

Paite

Mark

10

1Yesu alitoka hapo akaenda mkoani Yudea na hata ng'ambo ya mto Yordani. Umati wa watu ukamwendea tena, naye akawafundisha tena kama ilivyokuwa desturi yake.
1Huan, a dinga, huaia kipanin Judia gamah leh Jordan gal ah a paita a; huan, mipite tuh a kiangah a hongkikhawm ua; huchiin, a hih ngeingei danin amau thu a hih nawn a.
2Basi, Mafarisayo wakamwendea, na kwa kumjaribu wakamwuliza, "Je, ni halali mtu kumpa talaka mkewe?"
2Huan, Pharisai khenkhat a kiangah a hong ua, amah zeetna dingin, Min ji a mak a siang hia? chiin, a dong ua.
3Yesu akawajibu, "Mose aliwapa maagizo gani?"
3Huan, aman, a kiang uah, Mosiin bang chiin thu a honpia a? chiin, a dawng a.
4Nao wakasema, "Mose aliagiza mume kumpatia mkewe hati ya talaka na kumwacha."
4Huan, amau, Mosiin kimakna lai gelha mak a phal jel hi, a chi ua.
5Yesu akawaambia, "Mose aliwaandikia amri hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
5Himahleh, Jesun a kiang uah, Na lungtang khauh jiakun aka huai thupiak nou dia a hon gelh sak.
6Lakini tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu aliumba mwanamume na mwanamke.
6Himahleh leitung pian tunga kipanin, Pathianin amau tuh numei leh pasal-in a siam ahi.
7Hivyo mwanamume atawaacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe,
7Huai thu jiakin pasalin a nu leh a pa a paisan dinga, a ji a len chinten ding;
8nao wawili watakuwa mwili mmoja. Kwa hiyo, wao si wawili tena bali mwili mmoja.
8huchiin, a nih un sa khat a honghi ta ding ua; huan nih ahi nawn ta kei ua, sa khat a honghi zota ding uh.
9Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe."
9Huaijiakin Pathianin a gawmsa mihingin khen kei heh, achia.
10Walipoingia tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake walimwuliza juu ya jambo hilo.
10Huan, in ah a nungjuiten huai thu tuh amah a dong nawn ua.
11Naye akawaambia, "Anayemwacha mkewe na kuoa mwingine, anazini dhidi ya mkewe.
11Huan, aman, a kiang uah, Kuapeuh a ji ma a, mi dang nei in a ji tuh ang a kawm san ahi;
12Na mwanamke anayemwacha mumewe na kuolewa na mwingine anazini."
12Aman leng a pasal a khena, mi dang a neih leh, angkawm ahi sam hi, a chi a.
13Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
13Huan, a khoih dingin a kiangah naupang neute a honpi ua; huan, nungjuiten a na tai ua.
14Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa.
14Himahleh, Jesun huai a muhin a lunghikei mahmaha, nungjuite kiangah, Naupang neute ka kiangah honpaisak unla, kham kei un; Pathian gam huchibang mitea ahi ngala.
15Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia katika Ufalme huo."
15Chihtaktakin ka honhilh ahi, Kuapeuh Pathian gam naupang neuten a kipahpih banga kipahpih lou tuh a sungah a lutkei hial ding uh, a chi a.
16Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.
16Huan, amau a pom a, a tunguah a khut a koiha vual a jawlsakta a.
17Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja alimjia mbio, akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, "Mwalimu mwema, nifanyeje ili niupate uzima wa milele?"
17Huan, pai dinga a pawt laiin mi khat amah lamah a hongtaia, a ma ah a khukdin a, a kiangah, Sinsakpa hoih, khantawna hinna ka tan theihna dingin bangchin ka hih ding? chiin, a dong a.
18Yesu akamjibu, "Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
18Huan, Jesun a kiangah, Bangdia hoih honchi? mi khat kia loungal kuamah hoih a om kei uh, huai tuh Pathian ahi.
19Unazijua amri: Usizini; Usiue; Usiibe; Usitoe ushahidi wa uongo; Usidanganye; Waheshimu baba na mama yako."
19Thupiakte khawng na thei vo oi - Tual that ken, Angkawm ken, Gu ken, Hek ken, Khem ken, Na nu leh na pa pahtawiin, chih khawng, a chi a.
20Naye akamjibu, "Mwalimu, hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu."
20Huan, aman, a kiangah, Sinsakpa huai tengteng ka naupan laia kipanin ka jui jel, a chi a.
21Yesu akamtazama, akampenda, akamwambia, "Umepungukiwa na kitu kimoja: nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate."
21Huan, Jesun amah a en a, a itta a, a kiangah, Hihding khat nei lai chia; pai inla, na neih peuhmah juak inla, tagahte kiangah pia in, huchiin vanah gou na nei ding; huan, hongpai inla, honjui in, a chi a.
22Aliposikia hayo, alisikitika, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.
22Ahihhangin, huai thu ah a mel a hongmual a, lungkham takin a pai mangta; sum tampi nei mi a hih jiakin.
23Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, "Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!"
23Huan, Jesun a en vialviala, a nungjuite kiangah, Sum haute Pathian gama lut haksat tuak namai e, a chi a.
24Wanafunzi walishangazwa na maneno yake. Yesu akawaambia tena, "Watoto wangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu!
24Huan, nungjuiten a thugen lamdang a sa mahmah ua. Jesun bel a dawnga, a kiang uah, Naute aw, sum muangte din Pathian gama lut a haksa thei ngei.
25Ni rahisi zaidi ngamia kupenya katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."
25Mihausa Pathian gama lut sangin sangawngsau phim bila lutpaisuak a baihlam jaw, a chi a.
26Wanafunzi wake wakashangaa sana wakaulizana, "Ni nani basi, atakayeweza kuokoka?"
26Huan amau tuh lamdang a naksak mahmah ua, a kiangah, Ahihleh, kua hotdam ahi thei dia? a chi ua.
27Yesu akawatazama, akawaambia, "Kwa binadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo, maana kwa Mungu mambo yote huwezekana."
27Jesun amau a ena, Huaijaw mihing din hih vual ahi keia, Pathiana din bel hihvual louh ahi kei: Pathian adin bangkim hih theih ahi ngala, a chi a.
28Petro akamwambia, "Na sisi je? Tumeacha yote, tukakufuata!"
28Peterin a kiangah, Ngai dih, kou bangkim paisanin kon jui ua, chiin, a hon gen pana.
29Yesu akasema, "Kweli nawaambieni, kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au mama, au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema,
29Jesun, Chihtaktakin ka honhilh ahi, kuapeuh keimah jiak leh Tanchin Hoih jiaka in hiam, unaupate hiam, unaunute hiam, nu hiam, pa hiam, tate hiam, gamte hiam, paisante tuh,
30atapokea mara mia zaidi wakati huu wa sasa nyumba, ndugu, dada, mama, watoto na mashamba pamoja na mateso; na katika wakati ujao atapokea uzima wa milele.
30tu dam sung mahmahin, inte, unaupate, sanggamnute, nute, tate, gamte a leh jain, sawinate toh, mu lou ding mahmah a omkei; hun hongtung dinga khantawna hinna toh.
31Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza."
31Himahleh, mi tampi masapena omte tuh nanungpen a honghi ding uh, nanungpente leng masapen a honghi ding uh, a chi a.
32Basi, walikuwa njiani kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa anawatangulia. Wanafunzi wake walijawa na hofu, na watu waliofuata waliogopa. Yesu akawachukua tena kando wale kumi na wawili, akaanza kuwaambia yale yatakayompata:
32Huan, Jerusalem khuaa hohtou dingin lampi ah a om ua; Jesun a ma uh a kai a; amau tuh lamdang a sa mahmah ua; a honjuiten a kihta uh. Huan, aman tuh sawm leh nihte a pi tuam nawn a,
33"Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe na kumkabidhi kwa watu wa mataifa.
33Ngai dih ua, Jerusalem khua ah hohtou ding i hi ua; Mihing Tapa siampu liante leh laigelhmite kianga matsakin a om ding; huan, amau si dingin a tungah thu a hihpuk ding ua, Jentelte kiangah a pe ding uh;
34Nao watamdhihaki; watamtemea mate, watampiga mijeledi na kumwua. Na baada ya siku tatu atafufuka."
34Huan, amau tuh nuihza bawl nan a nei ding ua, chil a siat ding ua, a vo ding ua, a hihlum ding uh; huan, ni thum nungin a thou nawn ding, chiin, a tunga thil hongtung dingte amau a hilhta a.
35Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, "Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba."
35Huan, Zebedai tapa Jakob leh Johanin amah a honnaih ua, a kiangah, Sinsakpa na kianga kon nget ding peuh uh non hihsak ka ut uh, a chi ua.
36Yesu akawauliza, "Mnataka niwafanyie nini?"
36Huan, aman, a kiang uah, Nou adin bang honhihsak leng na ut ua? achia.
37Wakamjibu, "Uturuhusu tuketi mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wa Ufalme wako."
37Huan, amau, a kiangah, Na thupina ah na taklam ah khat, na veilam ah khat hontusak in, a chi ua.
38Yesu akawaambia, "Hamjui mnachoomba! Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa, au kubatizwa kama nitakavyobatizwa?"
38Jesun tuh, a kiang uah, Na nget uh na theikei ua ahi. Ka nou dawn ding na dawn theiding ua hia? ka baptisma tan ding leng na tang thei ding ua hia? a chi a.
39Wakamjibu, "Tunaweza." Yesu akawaambia, "Kikombe nitakachokunywa mtakinywa kweli, na mtabatizwa kama nitakavyobatizwa.
39Huan, amau, a kiangah, Thei e, a chi ua. Huan, Jesun, a kiang uah, Ka nou dawn ding na dawn ding ua, ka baptisma tan ding leng na tang ding ua:
40Lakini ni nani atakayeketi kulia au kushoto kwangu si wajibu wangu kupanga, bali nafasi hizo watapewa wale waliotayarishiwa."
40himahleh ka taklam ah hiam, ka veilam ah hiama tut ding thu jaw kei piak ding a-hi keia, a bawlsakte uh ading ahi zo ding hi, a chi a.
41Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, walianza kuchukizwa na Yakobo na Yohane.
41Huan, sawmten huai a na jak un, Jakob leh Johan tungah a lungkimta kei hial ua.
42Yesu akawaita, akawaambia, "Mnajua kwamba wale wanaofikiriwa kuwa watawala wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, na wakuu hao huwamiliki watu wao.
42Jesun amau a sama, a kiang uah, Jentelte tunga vaihawm dia a sehte uh a tunguah a lal mahmah ua, a mi liante un a tunguah thu a nei mahmah uh chih na thei uh.
43Lakini kwenu isiwe hivyo, ila anayetaka kuwa mkuu kati yenu, sharti awe mtumishi wenu.
43Himahleh, nou lakah jaw huchi bang ahi kei ding; kuapeuh na lak ua mi lian hih ut tuh na nasem un a pang zo ding ahi.
44Anayetaka kuwa wa kwanza, sharti awe mtumishi wa wote.
44Kuapeuh na lak ua masapen hih ut tuh mi tengteng sikhain a pang ding ahi.
45Maana Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, ila alikuja kutumikia, na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi."
45Mihing Tapa hial leng na sepsaka om dingin a hongpai keia, na sem ding leh mi tampi tatna dinga a hinna pe dingin a hongpai ahi zo ngala, a chi a.
46Basi, wakafika Yeriko, naye Yesu alipokuwa anatoka katika mji huo akiwa na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mwombaji aitwaye Bartimayo mwana wa Timayo alikuwa ameketi kando ya barabara.
46Huan, Jeriko khua a hongtung ua; huchiin, Jesu Jeriko akipanin a nungjuite leh mipi tampitak toh a pawt lai un khutdoh mittaw, Timai tapa Bartimai, lam gei ah a natu a.
47Aliposikia kwamba ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita mahali hapo, alianza kupaaza sauti, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"
47Huan, Nazaret Jesu ahi chih a jak takin, Jesu, David Tapa, ka tungah zahngai ve, chiin, a kikouta a.
48Watu wengi walimkemea ili anyamaze, lakini yeye akazidi kupaaza sauti, "Mwana wa Daudi, nihurumie!"
48Huan, mi tampiin dai dingin a tai ua; himahleh aman, David Tapa, ka tungah zahngai ve, chiin, a kinak kou semsem a.
49Yesu alisimama, akasema, "Mwiteni." Basi, wakamwita huyo kipofu, wakamwambia, "Jipe moyo! Simama, anakuita."
49Huan, Jesu a dinga, Amah honsam dih ua, a chi a. Huan, mittaw tuh a sam ua, a kiangah, Khamuangtakin om inla, thou in; a honsam, a chi ua.
50Naye akatupilia mbali vazi lake, akaruka juu, akamwendea Yesu.
50Huan, aman tuh a puan paiin, a ding khia a, Jesu kiangah a hoha.
51Yesu akamwuliza, "Unataka nikufanyie nini?" Huyo kipofu akamwambia, "Mwalimu, naomba nipate kuona."
51Huan, Jesun amah a nahoupih a, Na tungah bangchia ka hih na ut? a chi a. Huan, mittawin, a kiangah, Heutupa, muh thei ka ut, a chi a.Huan, Jesun, a kiangah, Paita in, na ginna dampih hiteh, a chi a. Huchiin, a mu thei pahta a, lampi ah Jesu tuh a juita hi.
52Yesu akamwambia, "Nenda, imani yako imekuponya." Mara huyo kipofu akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.
52Huan, Jesun, a kiangah, Paita in, na ginna dampih hiteh, a chi a. Huchiin, a mu thei pahta a, lampi ah Jesu tuh a juita hi.