Swahili: New Testament

Paite

Mark

4

1Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
1Huan dil piau ah thu a hilh nawnta a. Huan mipi hon tampi tak a kiangah a hongkikhawm ua, huchiin, dil ah longah a tuanga, a tu a, mipi hon tengteng tuh dil piau a leitung ah a om ua.
2Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
2Huan, gentehna thuin thil tampi a hilh a; a thuhilhna ah a kiang uah,
3"Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
3Ngai khia unla, en dih ua; buhchithehpa buhchi theh dingin a kuan a.
4Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
4Huan, hichi a honghi a, a theh laiin a khen lampi sikah a kia a, vasaten a nezota ua.
5Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
5Huan, a khen suangsi lei lakah a kia a; lei a sah louh jiakin a pou pah
6Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
6Himahleh, ni a hong suahin haivuaiin a hongoma, zung a neih louh jiakin a vuai mangta mai hi.
7Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
7Huan, akhen loulingnei lakah a kia a, loupa tuh a hongkhang sanga, a depmangta a, gah himhim a gahta kei hi.
8Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia."
8Huan, a khen lei hoih ah a kia a, a pou a, a khangliana, a gahta a; a leh sawmthum khawng, a leh sawmguk khawng, aleh ja khawngin a pung chiatta uh, a chi a.
9Kisha akawaambia, "Mwenye masikio na asikie!"
9Huan, amahmahin, Kuapeuh jakna ding a bil neiin ja uheh, a chi a.
10Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
10Huan, a tang om laiin a kima omten sawm leh nihte toh gentehna thu tuh a dong chian ua.
11Naye akawaambia, "Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
11Huan, aman tuh akiang uah, Pathian gam thuguk jaw noute kianga piak ahi a, po lam mite a dingin bel bangkim gentehnaa gen ahi; huchiin.
12ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe."
12Muh jaw a mu thei na ua, theihsiam jaw a theisiam louhna ding un; huchilou injaw a kihei nawn ding ua, ngaihdam a honghi kha ding uh, a chi a.
13Basi, Yesu akawauliza, "Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
13Huan, amahmahin, a kiang uah, Hiai gentehna thu na theisiam kei umaw? Huchi ahihin bangchin gentehna thu dang tengtengte na theisiam tuan ding ua?
14Mpanzi hupanda neno la Mungu.
14Buhchithehpan thu a theh ahi.
15Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
15Huan, lam sika thu thehnate tuh hiai bang ahi uh; thu a jak tak un Setanin a lungtang ua thu theh tuh a laksak pahpah a.
16Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
16Huan, huchibangmahin suangsi leitunga theh tuh hiai-te ahi uh; thu a jak phet ua kipak taka pom pahte bang
17Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
17himahleh amau ah zung himhim a neikei ua, sawt lou chik kia a om uh; huai nungin thu jiaka gimthuakna hiam sawina hiam a hongom phetin a kipukpah pah uhi.
18Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
18Huan, mi dangte tuh loulingnei laka theh ahi uh; huaiten tuh thu a zata ua
19lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda.
19himahleh khovel lungkhamnate, thil dang duhgawlnate a honglut chiangin, thu a dep a, gah louin a om nak.
20Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja."
20Huan, lei hoiha tuh bel hiaite ahi uh; thu ja a, poma, a leh sawmthum khawng, a leh sawmguk khawng, a leh ja khawnga gahte ahi uh, a chi a.
21Yesu akaendelea kuwaambia, "Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
21Huan, amahmahin, a kiang uah, Khawnvak a koihnaa koih lou a, loh nuai hiam, lupna nuai hiam a koih dingin a honla ngei ua hia?
22Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
22Thang lou dinga im bangmah a om ngei keia, langlou dinga sel bangmah a om sam kei.
23Mwenye masikio na asikie!"
23Kuapeuhin jakna dinga bil a neih uleh ja uheh, a chi a.
24Akawaambia pia, "Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
24Huan, amahmahin, a kiang uah, Na jak uh bang ahia, pilvang un; na tehna ngei mah ua piakin na om ding ua, a tam jaw bawn piakin na om ding uh.
25Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa."
25Kuapeuh a nei tuh piak behlap in om ding ua, kuapeuh a neilou tuh a neih sun nangawn laksak in om ding uh, a chi a.
26Yesu akaendelea kusema, "Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
26Huan, a mahmahin, Pathian gam tuh min leia chi a tuh bang ahi.
27Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
27Jan chiangin a ihmu a, sun chiangin a thou jela; chi tuh ana pouin ana khanga, himahleh bangchi a pou a bangchi a khang ahia chih a theikei.
28Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
28Leiin amahin gah a honsuah jela; A masapenin a kung, huan, a vui, huan, a vui ah a tang.
29Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika."
29Himahleh, huai a gah a hongmin chiangin, buh lak a hun tak jiakin, kaite in atpah hi, a chi a.
30Tena, Yesu akasema, "Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
30Huan, amahmahin, Pathian gam tuh bangtoh i tehpih dia? ahihkeileh, bang gentehna thin ahia i genteh ding?
31Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
31Ankam chi tang khat leia a tuh un, leia chi tengteng sangin neupen mahleh,
32Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake."
32a tuh nung un a hongpou a, loupa tengteng sangin a honglianzota a, hiang lian taktak a honnei a, huchiin tungleng vasate tuh a lim ah a giak uhi, huchi bangmah ahi, a chi a.
33Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
33Huan, huchi bang gentehna thu tampiin, a jak theih khomkhom un, thu a kiang uah a gen jel a.
34Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
34Himahleh, gentehna lou in a kiang uah thu a gen ngei kei; amah nungjuite kiangah tuh a simin bangkim a hilhchian jel hi.
35Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, "Tuvuke ziwa, twende ng'ambo."
35Huan, huai ni mahin, nitaklam a honghihin, aman, a kiang uah Gal khat lam i kai ding uh, a chi a.
36Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
36Huchiin, mipite pai sanin, amah, a om ngeingei bangin, long ah a paipih pah ngal ua, Long dangte leng a kiangah a om hi.
37Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
37Huan, huihpi thupitak a hongnung a, tuikihawtte tuh longah a hongkihawt lut juajua a, huchiin long a hong dim dek maimah a,
38Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, "Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?"
38huan, amah tuh, lukham khama ihmuin, long mei lamah a oma. Huan, a phawng ua, a kiangah, Heutupa, ka manthat uh khawksa lou na hi maw? a chi ua
39Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, "Kimya! Tulia!" Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
39Huan, amah hongkhanglouta a, huih tuh a taia, dil kiangah leng, Dai inla, om kinken in, achia, Huan, huih tuh a tawpta a, a hong dai dide maimah.
40Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?"
40Huan, aman, a kiang uah, Bangchi a hichi tela lau na hi ua oi? Ginna himhim nei nai lou na hi umaw? a chi a.Huan, lau petmahin a lau ua, Hiai mi kua ahia le, huih leh dil nangawnin a thu aman uh? a kichi khiukheu uh.
41Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, "Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?"
41Huan, lau petmahin a lau ua, Hiai mi kua ahia le, huih leh dil nangawnin a thu aman uh? a kichi khiukheu uh.