1Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
1Huan, dil gal, Gerasin mite gam, a hongtung ua
2Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
2Huan, longa pat a pawt nungin mi khat, dawi nin pai, han akipana hongpawtin amah a natuak pah a
3Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
3huaimin tuh han ah te khawng omna a nei jela; kuamahin sikkhainiang nangawnin a hen theita kei uhi.
4Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
4kol khawng leh sikkhainiang khangin leng a na henhen ta ngal ua; himahleh, sikkhainiang khawng tuh a bottata, kol khawng leng a hihtan jela; kuamahin a hihnem zou kei uhi.
5Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
5A sun a janin han khawng leh tang khawngah a kikoukou a, suang khawng bangin a ki-at jel hi.
6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
6Huan, gamla taka kipana Jesu a muh takin a tai a, chibai a vabuk a
7akisema kwa sauti kubwa, "Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!"
7huan, aw ngaihtaka kikouin, Jesu, Pathian Tungnungpen Tapa, kei leh nang bang ahia i kizolhna om? Hon gimsak lou dingin Pathian minin nget chih takin ka honngen hi, a chi a.
8(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, "Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.")
8Jesun, a kiang ah, Nang, dawi ninpa, huai mi sunga kipanin pawt in, a nachita ngala.
9Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Naye akajibu, "Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi."
9Huan, aman Na min bang ahia? chiin a donga, Huan, aman, a kiangah, Ka min Nuai ahi, tampi ka hih jiakun, a chi a.
10Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
10Huan, huai gama pat amau sawl khe lou dingin Jesu kiangah hahtangpiin a ngena.
11Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
11Huan, huailaia tang pangah vok hon tampi a ta ua.
12Basi, hao pepo wakamsihi, "Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie."
12Huan, dawi ninten, Vok sung khawngah honlutsak in, amaua ka lut theihna ding un, chiin, a kiangah a ngen ua.
13Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
13Huan, aman thu a pia a, Huchiin, dawi ninte tuh a pawt ua, vok sung khawngah a lut ua; huan vok hon tuh, sang nih phial ahi ua, ken ah a tai suk duamduam ua, dil ah a tai lutta ua; huan dilah tuihakin a sita uh
14Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
14Huan, amau vok vulte a tai ua, khua ah leh lou ah khawng a gen ua, Huan, huai thil hongom bang ahia chih endingin mite a hong kheukhou ua,
15Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
15Huan, Jesu kiang a hongtung ua, dawi mat, nuai matpa, a lungsim ngei pu leh puan silha huaia tu a mu ua, huchiin a a lauta uh.
16Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
16Huan, ama ua muten, dawi mat tunga thil tundan leh vok tanchin khawng amaute a nahilh ua
17Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
17Huan, amau amah a gam ua kipan a pawt dingin a ngenta ua.
18Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
18Huan, longa tuang dia a kisak laitakin dawi matkhitpan Jesu kianga om a ngena,
19Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, "Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma."
19Himahleh Jesun a phal keia, a kiangah, Na in ah na lawmte kiangah pai inla Toupan nang dia thila honhihsak a thupidan leh nang a honghehpihdan va hilh in, a chi zota a.
20Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
20Huan, a paia, Dekapoli khua khawng ah Jesun amah dia thil a hihsak thupidan a tangkou pihta. Huan mi tengtengin lamdang a sa mahmah uhi.
21Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
21Huan, Jesu longa gal khat lama a hongkai nawnin mipi tampi tak a kiangah hongpai khawm ua, huan, amah tuh dil geiah a om a.
22Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
22Huan, kikhopna in a vaihawmte laka mikhat, a min Jaira, a honga, Jesu a muh takin a khe bulah a khupboha.
23akamsihi akisema, "Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi."
23Ka tanu naupang chik a si dekdek a; hong halha a hongdam theihna dingin, honga a tunga na khut koih dingin ka honngen hi, chiin, hahtangpiin a thum a.
24Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
24Huchiin, Jesu a kiangah a vahoha. Huan mipu thupi takin a jui ua, amah a boh lutlut ua.
25Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
25Huan, numei khat kum sawm leh kum nih si pawta china a oma,
26Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
26daktor tampi lakah nakpitakin a thuakta a, a neih tengteng leng a zangbei khinta a, phattuam naksangin a se zosop hi.
27Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
27Huai min tuh Jesu tanchin khawng anaja a, a nung ah mipi lakah a hongpaia, a puan a khoih a.
28Alifanya hivyo, maana alijisemea, "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
28A puan kia leng khoih leng, hihdamin ka om mai ding, a lungsimin a chi a.
29Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
29Huan, thakhatin a si pawt tuh a kam pah ngala, a natna tuh hihdam ahi chih a saah a kitheita a.
30Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, "Nani aliyegusa mavazi yangu?"
30Huan, Jesun, a sunga kipan thilhihtheihna pawt jel tuh a pawt chih a hontheia, mi lakah a kihei vialvial a, Kua ahia huai ka puan khoih? a chi a.
31Wanafunzi wake wakamjibu, "Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?"
31Huan, a nungjuiten, a kiangah, Mipin a honboh lutlut uh na mu ngala, Kua ahia honkhoih? bangchi dana chi na hia le? a chi ua.
32Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
32Huan, aman tuh huai thil hihnu tuh muh tumina en vialviala.
33Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
33Huchiin, numeiin a tunga thil a hihsak theiin, lau leh ling kawmin a hongpaia, a maah khupbohin, a kiangah thudik a ngenta a hilh vek ta a.
34Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako."
34Huan aman, a kiangah, Tanu na ginna dampih hi chia, khamuangtakin pai inla, na natna akipan na dam tawngtungta in, a chi a.
35Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, "Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?"
35A pau lai takin kikhopna ina vaihawmpa in a kipan mi a hongpai ua, Na tanu sita hi, bang dia Sinsakpa hihbuai lailai ding na hiam? a chi uhi.
36Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, "Usiogope, amini tu."
36Jesun tuh a thugen uh ngeingaih louin, kikhopna in vaihawmpa kiangah, Lau ken, gingta mai in, a chi a.
37Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
37Huan, Peter toh Jakob toh, Jakob unau Johan toh chih louhngal midang uamahin amah a zuih uh a phal kei.
38Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
38Huan, kikhopna in vaihawmpa in a vatunga, Jesun ana buai vengvung uleh a nakap vengvung uleh a namau vengvung uh a vamu a,
39Akaingia ndani, akawaambia, "Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu."
39Huan, a valuta, a kiang uah, Bang dia bilama, kap na hi ua? naupang si lou hi, a ihmu ahi jaw hi, a chi a.
40Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
40Huan, amau amah a nuihsan maimah ua. Ahihhangin Aman, a vek un a delkhia a, naupang omna ah a valut a,
41Kisha akamshika mkono, akamwambia, "Talitha, kumi," maana yake, "Msichana, nakwambia, amka!"
41Huan, naupang khut a len a, a kiangah, Talitha Kumi, a chi a. Huai tuh, Nungak nou, thou in, ka honchi, chihna ahi.
42Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
42Huan, numei naupang tuh a thou a, a paipah ngala; amah tuh kum sawm leh kum nih mi ahi ta him a. Huan, amau tuh lamdang a sa mahmah uh.Huan, aman, a kiang uah, Hiai kuamahin theikei heh, a chi bilbela, huan, nek ding piak ding thu a peta a.
43Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.
43Huan, aman, a kiang uah, Hiai kuamahin theikei heh, a chi bilbela, huan, nek ding piak ding thu a peta a.