Swahili: New Testament

Paite

Matthew

2

1Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu, mkoani Yudea, wakati Herode alipokuwa mfalme. Punde tu baada ya kuzaliwa kwake, wataalamu wa nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu,
1Huan, kumpipa Herod a lal laia, Judia gama, Bethlehem khuaa Jesu a hongpianin, ngaiin, suahlam a kipan mi pilte Jerusalem khua ah a hongpai ua.
2wakauliza, "Yuko wapi mtoto, Mfalme wa Wayahudi, aliyezaliwa? Tumeiona nyota yake ilipotokea mashariki, tukaja kumwabudu."
2Koiah ahia Judate Kumpipa hongpian? suahlam ah a aksi ka mu ua, amah be dia hongpai ka hi uh, a chi ua.
3Mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, yeye pamoja na wakazi wote wa Yerusalemu.
3Huan kumpipa Herodin huai a jak phetin a lungjing a, Jerusalemte tengteng leng a lung uh a jing sam ua.
4Basi akawaita pamoja makuhani wakuu wote na walimu wa Sheria, akawauliza, "Kristo atazaliwa wapi?"
4Huchiin, siampu liante leh mite laigelhmite tengteng a sam khawm a, Kris pianna ding tuh a dinga.
5Nao wakamjibu, "Mjini Bethlehemu, mkoani Yudea. Ndivyo nabii alivyoandika:
5Huan, amau tuh a kiangah Judia gama Bethlehem khua ah; hichiin jawlneiin a gelh a kei hiam.
6Ewe Bethlehemu katika nchi ya Yuda, kwa vyovyote wewe si mdogo kabisa kati ya viongozi wa Yuda; maana kwako atatokea kiongozi atakayewaongoza watu wangu, Israeli."
6Nang, Judia gama Bethlehem aw, Judia khopite lakah na neupen kei hial, Na sung akipana ukpa hongsuak ding ahi ngala, ka mi Israelte vengpa dingin, chih, a chi ua
7Hapo, Herode aliwaita faraghani hao wataalamu wa nyota, akawauliza wakati hasa ile nyota ilipowatokea.
7Huai nungin Herodin a gukin mi pilte tuh a sama, ngentel takin aksi kilat lai a dong kheta a.
8Kisha akawatuma Bethlehemu akisema, "Nendeni mkachunguze kwa makini habari za mtoto huyo. Mkisha mpata nileteeni habari ili nami niende nikamwabudu."
8Huan, amau tuh Bethlehem khua ah a paisaka, Pai ta unla, naungek thu ngentel takin dong khia un, huan ken leng amah ka hongbiak theih samna dingin, na muh tak un, honghilh un, a chi a.
9Baada ya kumsikiliza mfalme, hao wataalamu wa nyota wakaenda. Kumbe ile nyota waliyokuwa wameiona upande wa mashariki iliwatangulia hata ikaenda kusimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto.
9Huan, kumpipa thu a jak un; a paita ua; huan ngaiin suahlama aksi a muh uh naunek omna tung jawn a tuna a khawl masiah a ma uah a paizel a.
10Walipoiona hiyo nyota, walifurahi mno.
10Huan, aksi tuh amuh un, a kipak lo mahmah ua
11Basi, wakaingia nyumbani, wakamwona yule mtoto pamoja na Maria mama yake; wakapiga magoti, wakamsujudia. Kisha wakafungua hazina zao, wakampa zawadi: dhahabu, ubani na manemane.
11Huan, in sungah a valut ua, a nu Mari kianga naungek tuh a mu ua, a bok ua, a bia ua; huan a gou bawm khawng uh a hong ua, a kiangah kipahna dangkaengte, begawte, murrate a lan ua.
12Mungu aliwaonya katika ndoto wasimrudie Herode; hivyo wakarudi makwao kwa njia nyingine.
12Huan, Herod kianga kik nawnlou dingin a mang ua vauhilha a om jiak un, amau kho lamah lam tuam ah a paita uh.
13Baada ya wale wageni kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto, akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapokwambia, maana Herode anakusudia kumwua huyu mtoto."
13Huan, a pai nung un, ngaiin, Toupa angel Joseph kiangah a mangin a kilaka, Thou inla; naungek leh a nu pi inla, Aigupta gamah taimang in, kon hilh nawn masiah huailaiah om gige in; Herodin naungek hihmang dia zong ding a hih jiakin, a chi a.
14Hivyo, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akaondoka usiku, akaenda Misri.
14Huchiin, a thou a, a jan ajanin naungek leh a nu a pi a, Aigupta gamah a paita a.
15Akakaa huko mpaka Herode alipokufa. Jambo hilo lilifanyika ili neno alilosema Bwana kwa njia ya nabii litimie: "Nilimwita Mwanangu kutoka Misri."
15Huan, Herod sih mateng hualai ah a om gige a; Toupan jawlnei kama, Ka tapa tuh Aigupta gam apat ka sam khia, chia a gen tuh a hongtun theihna dingin.
16Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota walikuwa wamemhadaa, alikasirika sana. Akaamuru watoto wote wa kiume mjini Bethlehemu na kandokando yake wenye umri wa miaka miwili na chini yake wauawe. Alifanya hivyo kufuatana na muda aliopata kujua kutoka kwa wale wataalamu wa nyota.
16Huchihlaiin Herodin mi pilte khem a hih a kitheih tak in a heh mahmah a, mi a sawla, a hun lai tak thu ngentel taka mi pilte a dot khiak bangin, Bethlehem khua leh a kim tengtenga pasal naupang kum nih chiang nuai lam tuh a vek un a that a.
17Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Yeremia:
17Huchihlaiin jawlnei Jeremiain
18"Sauti imesikika mjini Rama, kilio na maombolezo mengi. Raheli anawalilia watoto wake, wala hataki kutulizwa, maana wote wamefariki."
18Rama khua ah husa a ja uh, kah khawng, misi ngaia mau vengvung khawng, Rakelin a tate a kah a, a om nawn louh jiak un a khamuan theih kei, chia a gen tuh a hongtung ta.
19Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri,
19Himahleh Herod a sih nungin, ngaiin, Toupa angel Aigupta gamah Joseph kiangah a mangin a kilaka.
20akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa."
20Thou inla, naungek leh a nu pi inla, Israel gamah pai in; naungek thah tumte a sihtak jiak un, a chi a.
21Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli.
21Huchiin a thou a, naungek leh a nu tuh a pi a, Israel gamah a lut taa.
22Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya,
22Himahleh, Arkelausi a pa Herod sikin Judia gamah a lal chih a jakin, huai lama pai a lauta a; huan a manga vauhilha a om jiakin Galili lamah a paita a;Nazaret kichi khua khatah a va omta a; Amah jaw Nazaret mi a chi ding uh, chia jawlneite nagen a hongtun theihna dingin.
23akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: "Ataitwa Mnazare."
23Nazaret kichi khua khatah a va omta a; Amah jaw Nazaret mi a chi ding uh, chia jawlneite nagen a hongtun theihna dingin.