Swahili: New Testament

Turkish: New Testament

Hebrews

7

1Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye akambariki,
1Bu Melkisedek, Salem kralı ve yüce Tanrı'nın kâhiniydi. Kralları bozguna uğratmaktan dönen İbrahim'i karşılamış ve onu kutsamıştı.
2naye Abrahamu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina hili Melkisedeki ni "Mfalme wa Uadilifu"; na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya "Mfalme wa Amani.")
2İbrahim de ona her şeyin ondalığını verdi. Melkisedek, adının anlamına göre, önce `doğruluk kralı'dır. Sonra da `Salem kralı', yani `esenlik kralı'dır.
3Baba yake na mama yake hawatajwi, wala ukoo wake hautajwi; haisemwi alizaliwa lini au alikufa lini. Anafanana na Mwana wa Mungu, na anaendelea kuwa kuhani daima.
3Babasız ve annesizdir, soyunu gösteren bir kayıt yoktur. Ne günlerinin başlangıcı, ne yaşamının sonu vardır. Tanrı'nın Oğlu gibi sonsuza dek kâhin kalacaktır.
4Basi, mwaona jinsi mtu huyu alivyokuwa maarufu. Baba Abrahamu alimpa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyoteka vitani.
4Bakın, büyük ata İbrahim'in ganimetten ondalık verdiği bu adam ne kadar büyüktür!
5Tunajua vilevile kwamba kufuatana na Sheria, wana wa Lawi ambao ni makuhani, wanayo haki ya kuchukua sehemu ya kumi kutoka kwa watu, yaani ndugu zao, ingawaje nao ni watoto wa Abrahamu.
5Kutsal Yasa'ya göre, Levi oğullarından olup kâhinlik görevini alanlara, halktan, yani İbrahim'in soyundan oldukları halde, kardeşlerinden ondalık almaları buyrulmuştur.
6Lakini huyo Melkisedeki hakuwa wa ukoo wa Lawi, hata hivyo alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu; tena akambariki yeye ambaye alikuwa amepewa ahadi ya Mungu.
6Melkisedek ise Levili kâhinlerin soyundan olmadığı halde, vaatleri alan İbrahim'den ondalık kabul etmiş ve onu kutsamıştır.
7Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu zaidi kuliko yule anayebarikiwa.
7Hiç kuşkusuz, kutsayan kişi kutsanandan üstündür.
8Tena, hao makuhani wanaopokea sehemu ya kumi, ni watu ambao hufa; lakini hapa anayepokea sehemu ya kumi, yaani Melkisedeki, anasemekana kwamba hafi.
8Burada ölümlü kişiler ondalık alıyorlar; ama orada, yaşamakta olduğuna tanıklık edilen biri alıyor.
9Twaweza, basi, kusema kwamba Abrahamu alipotoa sehemu moja ya kumi, Lawi (ambaye watoto wake hupokea sehemu moja ya kumi) alitoa sehemu moja ya kumi pia.
9Denilebilir ki, ondalık alan Levi bile İbrahim aracılığıyla ondalık vermiştir.
10Maana Lawi hakuwa amezaliwa bado, bali ni kama alikuwa katika mwili wa baba yake, Abrahamu, wakati Melkisedeki alipokutana naye.
10Çünkü Melkisedek İbrahim'i karşıladığı zaman, Levi hâlâ atasının bedenindeydi.
11Kutokana na ukuhani wa Walawi, watu wa Israeli walipewa Sheria. Sasa, kama huduma ya Walawi ingalikuwa kamilifu hapangekuwa tena na haja ya kutokea ukuhani mwingine tofauti, ukuhani ambao umefuata utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki, na si ule wa Aroni.
11Eğer Levililerin kâhinliği aracılığıyla yetkinliğe erişilebilseydi - nitekim halk bu kâhinlik altında Kutsal Yasa'ya kavuştu - Harun düzenine göre değil de, Melkisedek düzenine göre başka bir kâhinin gelmesine ne gerek kalırdı?
12Maana ukuhani ukibadilika ni lazima Sheria nayo ibadilike.
12Çünkü kâhinlik değişince, Yasa da zorunlu olarak değişir.
13Naye Bwana wetu ambaye mambo hayo yote yanasemwa juu yake, alikuwa wa kabila lingine, na wala hakuna hata mmoja wa kabila lake aliyepata kutumikia madhabahuni akiwa kuhani.
13Kendisinden böyle söz edilen kişi başka bir oymaktan geliyor. Bu oymaktan hiç kimse sunakta hizmet etmemiştir.
14Inafahamika wazi kwamba yeye alizaliwa katika kabila la Yuda ambalo Mose hakulitaja alipokuwa anasema juu ya makuhani.
14Rabbimizin Yahuda oymağından geldiği açıktır. Musa bu oymaktan söz ederken kâhinlerle ilgili bir şey söylemedi.
15Tena jambo hili ni dhahiri zaidi: kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki amekwisha tokea.
15Melkisedek benzeri başka bir kâhin ortaya çıktığından, bu söylediğimiz artık daha da açıktır.
16Yeye hakufanywa kuwa kuhani kwa sheria na maagizo ya kibinadamu, bali kwa nguvu ya uhai ambao hauna mwisho.
16O, Yasa'nın soyla ilgili ön koşuluna göre değil, yok edilemez bir yaşamın gücüne göre kâhin olmuştur.
17Maana Maandiko yasema: "Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki."
17Çünkü, «Sen Melkisedek düzenine göre sonsuza dek kâhinsin» diye tanıklık ediliyor.
18Basi, ile amri ya zamani ilifutwa kwa sababu ilikuwa hafifu na isiyofaa kitu.
18Önceki buyruk, zayıflığı ve yararsızlığı nedeniyle geçersiz kılındı.
19Maana Sheria ya Mose haikuweza kukamilisha jambo lolote. Lakini sasa, mahali pake pamewekwa tumaini lililo bora zaidi ambalo kwalo tunaweza kumkaribia Mungu.
19Çünkü Yasa hiçbir şeyi yetkinleştiremedi. Bunun yerine, aracılığıyla Tanrı'ya yaklaştığımız daha sağlam bir ümit verildi.
20Zaidi ya hayo hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.
20Ve bu, yeminsiz olmadı. Diğerleri yeminsiz kâhin olmuşlardı.
21Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: "Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele."
21Ama O kendisine, «Rab ant içti ve andından caymaz, Sen sonsuza dek kâhinsin» diyen Tanrı'nın yeminiyle kâhin oldu.
22Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
22Böylece İsa daha iyi bir antlaşmanın kefili olmuştur.
23Kuna tofauti nyingine pia: hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.
23Önceki düzende çok sayıda kâhin görev aldı. Çünkü ölüm, görevlerini sürdürmelerini engelliyordu.
24Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake.
24Ama İsa sonsuza dek yaşadığı için kâhinliği süreklidir.
25Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.
25Bu nedenle O'nun aracılığıyla Tanrı'ya yaklaşanları tamamen kurtaracak güçtedir. Çünkü onlara aracılık etmek için hep yaşamaktadır.
26Basi, Yesu ndiye Kuhani Mkuu ambaye anatufaa sana katika mahitaji yetu. Yeye ni mtakatifu, hana hatia wala dhambi ndani yake; hayumo katika kundi la wenye dhambi na ameinuliwa mpaka juu mbinguni.
26Böyle bir başkâhinimiz, kutsal, suçsuz, lekesiz, günahkârlardan ayrılmış ve göklerden daha yücelere çıkarılmış bir başkâhinimiz olması uygundur.
27Yeye si kama wale makuhani wakuu wengine; hana haja ya kutoa dhabihu kila siku, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu. Yeye alifanya hivyo mara moja tu wakati alipojitoa yeye mwenyewe, na hiyo yatosha kwa nyakati zote.
27O, diğer başkâhinler gibi her gün önce kendi günahları için, sonra da halkın günahları için kurbanlar sunmak zorunda değildir. Çünkü kendi kendini sunmakla bunu ilk ve son kez yaptı.
28Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele.
28Kutsal Yasa, zayıflığı olan insanları başkâhin atamaktadır. Ama Yasa'dan sonra gelen yemin sözü, sonsuza dek yetkin kılınmış olan Oğul'u başkâhin atamıştır.